Thursday, March 27, 2014

my article for newspaper: kuanzisha na kuendeleza bustani

Utaijua bustani yenye afya wakati unapoiona: laini, kama vile ni zulia la kijani limetandikwa chini, ukitembea humo hamna majani makavu yanayojaa miguuni kukufanya uchafuke miguu na viatu vyako. Sasa, kwa nini bustani yako haionekani hivyo? Kupata muonekano maridhawa wa bustani huenda ikatakiwa ubadili fikra zako, anasema mtaalamu na mbunifu wa bustani Hadija Adam. “Unajua jinsi wanavyosema utamu wa ngoma uingie ucheze? Vyema, unatakiwa ugeuke ukoka. Unatakiwa ufikiri ni nini ukoka unahitaji,” anasema Hadija. 
Vitu vya msingi anasema ni vya kawaida sana: jua, maji na mbolea. Ukishapata hivyo hapo ni furaha tu - kwako na kwa bustani yako.

Kuanzisha bustani mpya ni mchakato wa raha na changamoto pamoja. Inabidi maandalizi na mipango. Unatakiwa kuandaa eneo kwa kuondoa magugu yote na kujaza udongo kama itahitajika. Sasa hapa nikisema kujaza udongo kumbuka sio kila udongo unafaa. Bi Adam anasema hatua ya muhimu sana ambayo watu wengi wanaruka ni hii ya kujaza udongo. Ni muhimu sana kuweka udongo unaofaa na mbolea ya ng’ombe (sio ya kuku kwa kuwa ina tindikali kali kwa hivyo haifai kwa kuoteshea ukoka). Bi Hadija anashauri kama kiasi cha udongo ni robo tatu basi mbolea iwe robo. Katika kuchanganya na kusawazisha kwa kureki usilazimishe sana tambarare fuatilia ardhi ilivyo na mwelekeo wa maji ili usijesababisha kuweka dimbwi kwenye bustani yako wakati wa masika. Kuwa makini sana kwa kuwa ukishaotesha ukoka wako hutarudi nyuma tena na kuanza kung’oa kwa ajili ya makosa yaliyofanyika mwanzo.

Kuna aina nyingi za ukoka (majani) unazoweza kuotesha kwenye bustani yako. Nyingine ni laini na nyembamba sana (fikiria uwanja wa golfu na wa mpira wa miguu), wakati ukoka nyingine unaweza dhania umekanyaga nyasi kavu miguuni. Majani ni mengi na yanagundulika kila mwaka. Kwa majani haya yote hali ya hewa inachangia unawiri wake.

Hakuna swali ya kuwa kuweza kupata zulia zuri la ukoka lililofunga kila mahali kwa wakati mmoja ni kwa kuotesha mbegu kila mahali wakati wa mwanzo. Lakini hii inaweza kuwa gharama hasa kama unataka kufunga eneo kubwa. Badala yake unaweza kununua mbegu chache ukaotesha kitaku nawe ukaanza kujipatia mbegu zako kwenye kitalu hicho. Kumbuka hii ni kama kununua mbegu za kuweza kutosha eneo lako ni gharama sana. Kwa mfano, tukichukulia huu ukoka unaoitwa Canadian; mbegu za kujaa mfuko mmoja wa saruji zinauzwa kati ya elfu 30-40. Sasa kama eneo lako utahitaji mbegu mifuko hamsini kwa mfano, inaweza kuwa ni gharama kubwa kwako. Kwa hivyo nunua mifuko michache uoteshe kitalu uvune mbegu mwenyewe.

Sasa ukoka wako umeshaota na umeshafunga kila mahali na umerefuka kiasi ya kuwa unahitaji kuukatia. Inapokuja kwenye swala la kukata ukoka wa bustani wenye nyumba wengi wanashindwa kujua urefu sahihi. “Watu wengi wanakata ukoka wao kwa kuuacha mfupi sana, kitu ambacho kinayasababishia majani msongo,” anasema Bi Hadija. Anashauri usetie mashine  ya kukatia kwenye alama ya juu kabisa. Majani yakibaki marefu yanafanya mizizi ikue vizuri na pia inasaidia ardi isichomwe na jua la moja kwa moja na kuwa kavu kwani utaingia gharama ya kuongeza umwagiliaji. Na usiamini kuwa ukiacha majani yawe marefu ina maanisha kuyakata mara kwa mara kila baada ya muda mfupi, anasema Hadija. “Lakini hii ni uongo kabisa "kuna upotofu kwa watu wengi kuwa kama wakiyakata yakawa mafupi hautakata mara kwa mara, huu ni uongo; yanaota haraka mno kiasi kwamba hayakupunguzii muda wowote wa kukata tena.

Maji, maji, maji kila mahali. “Maji mara mbili kwa wiki ila maji mengi” kwa Hadija hii ndio kanuni ya msingi. Maji ya kuzama yanasaidia mizizi kupenya kina kirefu ardhini, wakati  maji kidogo kidogo kila siku yanasababisha vishina kukauka na kuzalisha majani makavu (ambayo ndio yanachafua miguu). Kumwagilia kwa kina pia kunafukuza wadudu wanaojishika kwenye majani. Kwa bustani mpya iliyooteshwa ukoka mwagilia maji mengi kila siku hadi mizizi ishike.

Bustani, hata ile unayoiona ina afya inahitaji chakula imara na hewa. Mara mbili au tatu kwa mwaka wakati wa masika wataalam wanashauri ndio wakati wa kuiwekea bustani mbolea. Kwa wakati huu mbolea ya kuku ndio inafaa zaidi hasa kuweza kutunza ule ukijani wa ukoka unaohitaji.

Magugu kwaheri, sio ajabu kuwa karibia kila bustani itakuwa na magugu. Njia nzuri ya kuangamiza magugu kwenye bustani ni kuchagua ukoka unaofunga kiasi kwamba utayazuia magugu kushamiri. Yale machache yatakayopenya dawa yake ni kuyang’oa.
Zingatia kanuni hizi za uanzishwaji na uendelezaji wa bustani na kila mmoja atakuwa na furaha -- wewe na bustani yako.

Makala hii imeandaliwa na Vivi O. Machange. Vivi ni mjasiriamali na ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa makazi. Kwa maoni au maswali tuma kwenda 0755 200023 au viviobed@yahoo.co.uk

Thursday, March 20, 2014

my article for newspaper: kaunta za jiko

Mambo ya kuzingatia kabla ya kununua kaunta za jiko

Kaunta za jiko zinahusika mno katika muonekano wa chumba hicho, lakini pia ni kwa umuhimu mkubwa wa kuwa na sehemu ya kufanyia kazi. Kaunta nzuri zinatakiwa ziwe imara, kuweza kuhimili matumizi ya kila siku, kumwagikiwa na vitu na kuhimili mgusano na vyombo vya kupikia vyenye moto kuwekwa juu yake.

Ukiondoa sakafu, kaunta ya jiko ni sehemu inayotumika zaidi ndani ya nyumba. Ni sehemu tunayoandalia chakula, tunayoweka funguo, barua na bili zilizoingia nyumbani na hata wakati mwingine tunaweka hapo magazeti. Hatuwezi kukataa umuhimu wake hasa kwa matumizi. Hata hivyo kwa ajili ni kitovu basi, muonekano wa kishirika na vifaa vingine hapo jikoni kama makabati, jokofu, jiko na sakafu unahusu. Lakini ni kaunta zako za jikoni ndio zinakuwa kipaumbele kwa ajili ni eneo ambalo macho yanaelekea moja kwa moja.

Kabla ya kununua kaunta za jiko hatua ya kwanza ni kufanya utafiti. Kuna aina lukuki sokoni kwa maana ya mitindo na vifaa vilivyotengenezea, kwa hiyo chukua muda wako kuchunguza aina mbalimbali. Kila aina inawakilisha faida na hasara, kwa hivyo sio vyema kukurupuka.
Kama ni swala la umaridadi au uimara, utunzaji au gharama, kila vifaa vilivyotengenezea kaunta vina faida na hasara zake. Nunua kaunta inayokubaliana na mahitaji yako kwa maana ya staili na matumizi. Kujifunza jinsi ya kununua kaunta ya jiko ni mchakato muhimu pale unapojenga au kurekebisha chumba cha jiko. Kaunta sahihi itakubaliana na bajeti yako , mtindo wako wa maisha na muonekano wa mapambo yako ya ndani.
Zifuatazo ni baadhi ya aina za vifaa vinavyotengenezea kaunta za jiko kama zinavyoelezewa na mtaalamu wa maboresho ya nyumbani Bwana Deo Minja. Na anaelezea faida na hasara ya kila aina.

Marble ni jiwe muhimu la asili linalotumika kwa wingi kutengenezea kaunta za jiko. Jiwe hili kiasili lina michoro mbalimbali inayolipa jiko kiwango na hisia za asili. Hata siku moja kaunta ya aina hii haikuangushi jikoni. Utunzaji wake na usafishaji ni rahisi ila unashauriwa kutokata vyakula kwa kisu juu ya marble moja kwa moja kwani inaweza kukwaruzika hivyo kuharibu muonekano. Kaunta hizi ni laini, rahisi kusafishika na haipitishi maji wala joto. Ukitembelea kwenye kila nyumba zenye majiko la kisasa, nyingi zitakuwa na kauta za jiko za aina ya marble.

Jiwe lingine maarufu kwa ajili ya kutengenezea kauta za jiko ni granite. Jiwe hili linafanya jiko lionekane la kifahari na huwa linakuja kwa rangi zaidi ya 3000, anasema Minja. Linadumu maisha ni ni la pili kwa ugumu baada ya almasi. Changamoto yake kubwa ni kuwa ni gharama kubwa

Kaunta za jiko za marumaru ni imara na rahisi kusafishika. Marumaru kwa kawaida inaongeza uhai wa mahali. Pia sio gharama na kuna aina na rangi mbalimbali kwa nyumba za kawaida. Changamoto yake ni kuwa kwa vile zile marumaru ni kipande vidogodogo vinavyounganishwa pamoja, basi wakati mwingine kaunta inakosa levo na pia ni rahisi kuwa na mipasuko na ile grout inayowekwa katikati ya mistari huwa inashika uchafu kirahisi mno

Kaunta nyingine za jiko ni zile za kujaladia kwa mfano formica. Ziumetengenezwa kwa vifaa vya plastiki vyenye sehemu ya juu  laini ambayo inakuwa rahsi kusafisha. Faida yake ni kwamba ni bei rahisi na zipo za rangi mbalimbali. Hasara yake ni kuwa mikwaruzo na mipasuko hairekebishiki.

Kaunta za mbao zinaleta muonekano mzuri na zipo za mitindo na rangi mabalimbali. Mbao ngumu kama vile mkongo na mninga ndio zinazotumiaka zaidi kwa ajili ya kaunta. Ni rahisi kusafisha na changamoto yake ni kuwa zinahitajika kufanyiwa maboresho ya mara kwa mara. Ubaya wa kaunta za mbao ni kuwa zinaharibiwa na maji na baada ya muda zinashika madoa.

Kaunta za chuma kisichoshika kutu kwa jiko lako nacho ni chaguo zuri. Zinahimili joto na ni imara. Na kwa sababu zinajengewa kwa matakwa yako inawezekana pasionekane viungio vyovyote kwenye kaunta yako. Zinafaa kuwekea sufuria za moto na ni rahisi kusafishika. Changamoto yake ni kuwa zina kelele, zinaweza kubonyea na huwezi kukatia juu yake.

Kama una  chumba cha jiko chenye umbo lisilo la kawaida hasa kona, zege inaweza kuwa chaguo zuri kwa ajili ya kaunta za jiko lako. Faida zake ni kwamba zinahimili joto na mikwaruzo. Na hazihitaji utunzaji kivile, zinaweza kuwekwa rangi na urembo wa aina mbalimbali ila changamoto yake ni kuwa  kama tunavyojua zege ni saruji kwa hivyo nyufa zinaweza kutokea na ule muonekano wa zege chumba kinaonekana kama cha kiwandani zaidi.

Baada ya kujua aina zote hizi za vifaa vya kutengenezea kaunta za jiko kama tulivyoelezwa na Bwana Minja kifuatacho ni kuangalia bajeti yako. Bajeti ndio kikwazo namba moja kwenye kuchagua kaunta za jiko. Kwa mfano kaunta za granite na marble zinaweza kuwa gharama mara 3 zaidi ya zile za kujaladia.

Jambo la pili la kuzingatia kabla ya kunua vifaa vyako vya kujengea kaunta za jiko ni umaridadi. Kaunta zote zinatakiwa zitimize lengo la msingi ambalo ni kuweza kuwa na eneo la kufanyia kazi wakati wa kuandaa chakula, hata hivyo kuna upande wa umaridadi. Kama huna uhakika wa muonekano wa kaunta unayotaka basi angalia maeneo mengine ya jiko kama vile makabati ili kuweza kuleta uwiano na kaunta.

Jambo la tatu na kubwa kuliko ni kuamua sasa kununua kifaa cha aina hii ili kutengenezea kaunta za jiko lako. Gharama, uimara na muonekano unatofautiana kwa kila aina ya vifaa vya kutengnezea kaunta.

Haijalishi ni aina gani ya kaunta ya jiko utakayoamua kuweka nyumbani kwako, mara zote hakikisha kuwa unapitia kwa mtaalam. Inatatiza, inakula muda, na kama nia yako kuu ni kufanya eneo hili lionekane maridadi wakati huo huo likitumika, unataka kuwa na uhakika wa usimikaji sahihi.

Makala hii imeandaliwa na Vivi O. Machange.  Vivi ni mjasiriamali  upande wa usafi wa nguo, mazulia na magari; pia ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa nyumba. Kwa maoni au maswali tuma kwenda 0755 200023 au viviobed@yahoo.co.uk

Tuesday, March 18, 2014

house tour: jinsi ya kuandaa meza ya mahanjumati

uma zinakaa kushoto na kisu kulia na hata wakati wa kula uma inashikwa na mkono wa kushoto na kisu kwa mkono wa kilia

hapa napkin imefanana na table runner..mambo ya color neighboring tu


tembea uone...

ona jinsi hii cabbage inavyopikwa nzima nzima. inafungwa kabisa na uzi ili isiachie ikatawanyika wakati wa kupikwa..

news: ukwepaji gharama huchangia kuwepo majengo yasiyo na ubora

UKWEPAJI wa gharama za ujenzi wa nyumba, unadaiwa kuchangia kuwepo majengo yasiyo na ubora katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
 
Katika ukwepaji wa gharama, wengi hukwepa kutumia wataalamu wa majengo, hususan wabunifu wa majengo na wakadiriaji majenzi waliothibitishwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi.

Msajili wa Bodi ya Usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi nchini, Jehad Abdallah Jehad alisema hayo leo Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habar.
Alikuwa akizungumzia semina endelevu ya Bodi itakayofanyika jijini Mbeya Machi 20 na 21. Alisema ni nyumba chache zilizojengwa kwa ubora. Jehad alisema wananchi wanatakiwa kufahamu kuwa ujenzi wa nyumba ni gharama kubwa tofauti na wengi wanavyodhani.
“Ujenzi wa nyumba ni sawa na mgonjwa anayehitaji tiba hospitali. Usipomuona daktari kwa ajili ya vipimo badala yake ukaenda duka ladawa watakuandikia dawa tu lakini ugonjwa bado utakuwa palepale,” alisema.
Alisisitiza, “wananchi wasiogope gharama za kutafuta wataalamu. Hawa ni watu waliosomea kwa muda mrefu taaluma hiyo, hivyo tunawaasa wawatumie wataalamu hawa ili kupata majenzi yenye ubora.”
Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Dk Ambwene Mwakyusa alisema wameandaa utaratibu wa semina endelevu kwa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi katika miji mbalimbali nchini .

Wednesday, March 12, 2014

my everyday life: marekebisho madogo getini

basi geti lilikuwa linagoma nikasema ni betri imekufa ama ni motor. bahati nzuri fundi akagundua ni gurudumu zinaleta shida labda zimechakaa ama na mvua zilizonyesha nazo zilichangia. nimesema bahati nzuri kwa ajili motor au betri ni ghali zaidi ukilinganisha na gurudumu. twende pamoja katika picha uone zoezi lilivyofanyika..
fundi akinionyesha tairi mpya
reli imeonekana ipo poa
reli zimekubali

geti liko bomba limeshatulia

Friday, March 7, 2014

birthday pics from my first miracle





somo la kujifunza: usiamini kila unachokiona...


'Keeping Up With the Kardashians' Fake House for Saleew photo




.

An exterior shot of the house used in 'KUWTK' (MLS/Getty Images)
The fake Kardashian-Jenner mansion can be yours for $6.25 million!
Let's back up for a minute. You didn't actually think the exterior shots of the Italian-style home featured on "Keeping Up With the Kardashians" belonged to Kris & Co. did you?
Reality TV's first family chose not to depict the outside of their true house on the show for security purposes. The mansion that is often featured on E! is actually located in Studio City's Fryman Estates. The 7,043-square-foot home boasts seven bedrooms, eight bathrooms, and is known as the "Palazzo di Sono."


Instead, Kris, Kim, Kanye, Kendall, and Kylie live several miles away in a private gated community in Calabasas, California. Their real home has six bedrooms, eight baths, and is 9,000 square feet. However, the interior shots you see on "KUWTK" all take place inside the family's actual residence.
"My old home in Beverly Hills was really my home & I would get people showing up at all hours ringing my gate & had to call the police on several occasions. People hoping the gate & scaring me," Kim explained on Twitter when asked about the house. "It was so unsafe. The hollywood star tours would stop by too, bc they recognized my home from our show. After that we realized how unsafe it is to show the exterior of our homes. So now we use different homes for the outside for security purposes. When we film inside, thats obviously our real home."
One way to easily tell that there were two different houses being featured on the show is that the faux home's design was inspired by a Medici castle in Florence, while Kris's tastes are clearly much more modern.
And if you are a true Kardashian detective, you may have also noticed that the front doors and fountains don't match up while watching the show.

Tuesday, March 4, 2014

NEWS: haya makazi hayo Goba


jipatie dondoo za namna ya kuondoa madoa kwenye carpet

soma katikati ya mistari. kakupa aina za madoa na jinsi ya kuyaondoa..enjoy!

How to Clean Any Carpet Stain

You can handle any carpet-cleaning emergency with stuff you already have in your cupboard. We've cleaned enough old carpets to know! 

Wall-to-wall carpetingWall-to-wall carpeting
Oops! Whether it be grape juice, a little present from Fido, or finger-paint artwork from your 3-year-old, it seems whatever is not supposed to get on the carpet always does. Here are a few tips on how to clean your carpets using products you can find around your house.
What You Should Know Before You Start. To remove a stain, simply blot the spot and dry working from the outside in, rinse thoroughly with clean water, then blot again. Never scrub the carpet, or you risk ruining the carpet fibers or letting the spill soak through to the carpet pad.
For more specific advice, find your type of stain below. In addition to these methods, there are several spot removers on the market; before you try one, test it out in an inconspicuous spot to make sure it doesn't discolor your carpet.
Water-Soluble Stains
alcoholic beverages
berries
colas
excrement
food dyes
gravy
ice cream
jelly
milk
mud
washable ink
wet or latex paint
Use a simple cleaning solution made up of 1/4 teaspoon of nonbleach detergent (or white vinegar) mixed with 32 ounces of water. 
Special Water-Soluble Stains
blood
chocolate
coffee
mustard
tea
vomit
wine
kwa madoa haya tumia sabuni ya unga uliyoweka kwenye maji ya uvuguvugu
Fat, Oil, and Wax. Place a paper towel over the carpet and iron on warm setting. The wax, fat, or oil should come up off the carpet and stick to the paper towel.
Cigarette Burns. These can be removed by gently rubbing the pile with the edge of a hard and flat surface, such as a dull knife.
Glue. Moisten a cotton ball or soft cloth with rubbing alcohol and press it on the affected area. Once the glue residue is thoroughly moistened, gently wipe it off and repeat until the carpet is clean.
Wax and Gum. Use ice to freeze the wax or gum, then shatter it with a blunt object, such as a spoon. Vacuum before the pieces soften, and blot the carpet with a white towel.
Nail Polish. Blot the area with a rag dipped in nail polish remover.
Urine. Absorb as much as possible with white towels, then blot with a damp, cool cloth. Next, spray or blot with a solution of one part white vinegar to one part water. Finally, apply a solution of 1/2 teaspoon of clear, mild, nonbleach detergent mixed with 32 ounces of water, rinse, and blot dry.

mbolea ya kuku na canadian grass ni kama mgonjwa na uji

basi baada ya kijimvua cha hapa na pale asubuhi hii nikaangalia bustani yangu jinsi kijani kilivyoshamiri baada ya kuweka mbolea ya kuku. kiumande kwa mbaali na wingu bado lipo. mdau wakati huu wa mvua ni mwake kuweka mbolea kwenye bustani..

Monday, March 3, 2014

my everyday life: mpangilio wa eneo la nje ya nyumba

mara kadhaa napata cha kupost kwa kuangalia ni nini wasomaji wangu wanataka kufahamu. baadhi wameniomba kufahamu mpangilio wa nje ya nyumba. kwa maana ya kwamba labda mtu kashajenga nyumba yake sasa anahamia kwa hivyo anauliza nje akugaweje gaweje. kwa uzoefu wangu nje kuwe na maeneo manne. eneo la sakafu ngumu ambalo ni la drive way na la pili la walkway, la tatu liwe ni sehemu ya majani, maua miti yani kwa ujumla ni lile eneo la udongo ambalo unaweza kuotesha chochote. eneo la nne ni lile la maji kwa mfano kama una uwezo wa kuweka swimming pool au fontain. ongezea mdau..