Saturday, January 31, 2015

FROM ME: Kama bado, ni wakati wa kufikiria kuwa na meza za marble

Jiwe la marble limekuwa likitumika kama malighafi ya ujenzi na kwenye sakafu, lakini pia linaanza kushika kasi kuwa sehemu ya juu ya meza. Watanzania wengi wamekuwa wakitumia jiwe la marble zaidi kwa kaunta za jikoni. Linafaa kwa kila aina ya meza unayoweza kufikiria.


Ni fenicha ya kipekee ambayo kila mmoja atapenda kuwa nayo. Kama unafikiria kununua dining table ya marble fahamu kuwa jie hili lina uzuri wa asili. Huwezi kumcha kumfurahisha mgeni yeyote kwa meza ya marble, zaidi ya yote ni kuwa hazipitwi na wakati kutokana na kwamba ni jiwe la asili. Ni imara na kama itatunzwa vizuri meza ya marble inaweza kudumu kuliko fenicha nyingine zote.




FROM ME: I can’t imagine the plans God has for you!



Friday, January 30, 2015

MAHUSIANO: Mzazi anauma jamani, huyu kamlazimisha mchumba wake ameze engagement ring kwa kisirani cha baba yake kuwa na cancer

A member of R&B group Jagged Edge was arrested Thursday morning after he allegedly forced his fiancée to eat her engagement ring.

Police were called to the Atlanta home of Kyle Norman early Thursday, where they were met by an injured woman who introduced herself as Norman’s fiancée. The woman said she and Norman were arguing about details of their upcoming wedding when he attacked and beat her.
From WGLC TV:

Police stated in their report that the victim had a cut to her nose and it appeared as if she had a blood clot in her right eye that had burst.
The victim told police Norman punched and choked her with a scarf and shoved her engagement ring down her throat choking her more. 
According to police, Norman took away the victim’s car keys and broke her cell phone, refusing to let her leave. 
Once he walked away, she ran and grabbed his cell phone and was able to run outside and wake up a neighbor who let her inside. 
Norman told police he was upset about his dad having cancer and that’s the reason he got so mad at his fiance.

FROM ME: Kanuni kuu 3 za kusafisha ndani ya nyumba sakafu ya kusafishwa kwa maji


  • Ainisha maeneo ya kusafisha .Hii inasaidia hata unapokuwa na mtu wa kukufanyia usafi anakuwa anafahamu mwisho wa usafi wake.
  • Hakikisha una zana  na vifaa vinavyotakiwa kwa ajili ya kusafishia, kwa uchache kama unasafisha ndani eneo ambalo ni la kudeki (halina carpet) unatakiwa kuwa na malighafi za kitambaa za aina tatu. Kitambaa cha kwanza ni taulo au mop kwa ajili ya kudekia, cha pili ni kitaulo kilicholoa kwa ajili ya kufutia maeneo yanayopaswa kufutwa kwa maji na cha tatu ni kitaulo kikavu kwa ajili ya kufutia maeneo yasiyopaswa kufutwa kwa maji kama kwenye vioo. Kwa maeneo mengine mengi kitaulo kilicholoa kinafaa zaidi kwa kuwa kwangu mimi sioni kama kikavu kinafanya kazi effective. Mwishoni utahitaji maji, sabuni, all-purpose au glass cleaner au windex. Vifaa hivi vinakupasa kuwa mkononi kwa usafi wa ndani kusikokuwa na carpet.
  • Safisha kuanzia juu kwenda chini na kwa kufuta peleka mkono clockwise (kama saa inavyotembea) na safisha kuelekea nje. Kwa njia hii hutakuwa na vumbi linaloanguka tena juu ya sakafu yako ambayo umeshasafisha.
Unaonaje uka print ukampa dada wa kazi ajifunze kanuni hizi ili akurahisishie kazi ya kuelekeza kila wakati?

Picha ya siku: Watoto wazuri sana hawa, wamependeza kwelikweli

 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mama Salma Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nje Mhe Membe wakiwa na Watoto wa Kitanzania wakati wa Ufunguzi wa Majengo ya Ubalozi wa Tanzania Nchini Ufaransa

Thursday, January 29, 2015

NITAVUKAJE: Huyu anaendesha maisha kwa kufua nguo nyumbani kwa wateja wake

Ukisoma makala hii inaweza kukusaidia wewe au mtu unayemfahamu. Imeandikwa na Joyce Joliga

Kati ya wanawake ambao wanaamini kuwa mafanikio hayaji bila kujituma kwa kufanya kazi kwa bidii ni Salome Sanga (58).

Salome ni mkazi wa Makambi katika Manispaa ya Songea na amekuwa akisifika kwa kufua nguo kwenye nyumba za watu mbalimbali zaidi katika Kikosi cha Polisi FFU na Kikosi cha Jeshi la Wananchi Tanzania, Chandamali mkoani Ruvuma.

Mama huyo wa watoto wanane ambaye awali aliolewa mwaka 1973 na Aloyce Haule ambaye alizaa naye watoto watatu. Haule alifariki mwaka 1982 na miaka miwili baadaye, alifunga ndoa na Vitalis Mumba ambaye alizaa naye watoto sita na mmoja kwa bahati mbaya alifariki dunia hivyo kubaki akiwa na watoto wanane.

Anasema walitengana na Vitalis kwa kuwa hali ya maisha ilikuwa ngumu na kila kukicha alikuwa akipigwa na mumewe huyo ambaye hata hivyo alikuwa haihudumii familia yake.
“Niliachana naye nikaenda kupanga chumba na nilianza maisha  ya upweke nikiwa na wanangu wanne ambao tayari wameolewa wawili wako Dar es Salaam na wengine wawili Majengo Songea na wengine wanaendesha maisha yao vijijini.

Anasema anajivunia kufanya kazi hiyo ya kufua nguo katika nyumba za watu na wala hajutii kufanya kazi hiyo na hatishwi na maneno ya watu ambao hudharau kazi za watu.

Salome anasema kupitia kazi hiyo, imemsaidia kufahamiana na watu mbalimbali pamoja na kujipatia kipato kikubwa kinachomsaidia kuendesha familia yake bila msaada kutoka kwa ndugu zake ama jamii inayomzunguka.

Kwa sasa Salome anaishi na mama yake mzazi naye amezeeka pia  ni mgonjwa hivyo anamtegemea kwa mahitaji mbalimbali.
Anasema anaifanya kazi hiyo kutokana na kukabiliwa na dhiki kubwa na amekuwa akikabiliwa na matatizo mbalimbali, hivyo akaona njia ya kujikwamua ni kujishughulisha na kazi hiyo ili kupata fedha za kujikimu na kulipa pango la nyumba anayoishi.

“Unajua sikwenda shule kwa kiasi kikubwa, nimeishia darasa la saba, sasa ninatumia nguvu zangu kama mtaji,” anasema.
Anafafanua zaidi kuwa, kazi ya kufua nguo za watu ni ngumu ingawa inampatia kipato kikubwa.

“Nimekuwa nikikutana na vikwazo pamoja na  vitu mbalimbali ambavyo si vizuri kuvizungumza lakini bado sijakata tama…Nimekuwa nikiendelea kufanya kazi hiyo kwa uaminifu mkubwa niwaridhishe wateja wangu,” anasema.

Anasema uaminifu ndiyo unaomfanya apate kazi nyingi na wakati mwingine anazikimbia kwa kuwa zinamwelemea.

Anataja changamoto nyingine kuwa ni baadhi ya wateja kutomlipa fedha zake kwa wakati , “Utakuta  umefua na ukimaliza kazi mtu anakukopa lakini nashukuru Mungu wengi ni waaminifu wamekuwa wakinilipa baada ya kumaliza kazi na wanaokuwa hawana pesa siku hiyo, wakitoa ahadi siku inayofata  wanaitekeleza,” anasema.

Anasema: “Changamoto nyingine ni kulipwa fedha kidogo tofauti na nguo za kufua na utakuta kwenye hoteli kubwa nguo moja mtu analipa Sh1,000 hadi Sh2,500 lakini kwa sisi tunaofua nyumbani wateja wetu wanatukadiria wenyewe utakuta anatoa rundo la nguo na kukupatia Sh7,000 basi huwa tunaridhika na kupokea.

Kutokana na kazi hiyo, anasema kwa siku anaweza kufua nguo katika nyumba tatu hadi nne kutegemea na upatikanaji wa kazi anazopata.

“Ninaanza kufua kwa kuanzia Sh3,000 hadi 15,000 na kujipatia pesa za kununua mahitaji yangu madogo madogo…,” anasema.

Anasema pamoja na kujishughulisha na kazi ya kufua nguo nyumbani  pia anajishughulisha na biashara ya uuzaji wa supu nyumbani kwake  eneo la Makambi na hata hivyo biashara hiyo haijampa faida kama inavyompatia  biashara ya kufua nguo nyumbani kwa watu.

Anasema kwa sasa anajitahidi kuendelea kufanya kazi yake ya ufuaji nguo kwa ufanisi mkubwa na anatamani siku moja kama Mungu atamjalia. Pia, akipata wafadhili wa kumjengea  nyumba ya kisasa ya kuishi  na ataweka mashine za kisasa za kufua nguo hivyo itamsaidia kutoa huduma kwa wananchi wengi zaidi ambao watakuwa wanahitaji huduma yake badala ya kuendelea kuzunguka kwenye nyumba za watu.



MAHUSIANO: Hivi visa kama vinafanana fanana, ni kuogopa majukumu au ni nini

Ukisoma post yangu ya nyuma ya huyo mama wa mapacha sita mume wake alimkimbia. Ona tena na huyu, nini mbaya jamani hawa wanaume wanakimbia?:
'My Husband Went Out For A Coke And Never Came Back'
Cathy Meyer knew her 17-year marriage had its shortcomings, but she never dreamed that her husband would one day walk out the door, never to come back.
In a conversation with HuffPost Live's Nancy Redd, the mother of two recalled her abrupt divorce.

"On January 1st, our anniversary, he was madly in love and told me he couldn't live without me," she said. "On January 10th, we were getting ready to go to church, and we had a little tiff and he said 'I'm going to go get a Coke' and he picked up his car keys and quite literally never came home again."

MAHUSIANO: Watoto wanapompenda zaidi dada kuliko mama inaleta shida

 The ex couple are pictured in 2012 with twins Moroccan and Monroe. Ila Mariah hiki kigauni kimemtoa sana
Mariah and Nick Nanny Sues

Their Kids Liked Me Too Much

Mariah Carey and Nick Cannon are being sued by their former nanny, according to reports.
New York Daily News claims that Da Costa has filed a lawsuit after allegedly being forced to work 100-hour weeks, without being paid overtime.

Da Costa is said to have filed court documents in Manhattan Federal Court, where she describes being on duty all day every day, and often being unable to sleep, eat or take a break.

The nanny worked for the singer and the comedian from October 2013 until January 2014, looking after their twins Moroccan and Monroe, now three.

She claims that she was fired shortly after being berated by Carey for ‘expressing too much affection for their children’. 
Da Costa allegedly states in the lawsuit that she was regularly called on in the middle of the night by Carey and required to ‘attend her every demand, spontaneous or otherwise’

MAHUSIANO: Kwanini asimfunge kizazi?


‘Mume kanikimbia kisa nazaa sana’
“Sitasahau siku niliyokimbiwa na mume wangu baada ya kumzalia pacha kwa mara ya tatu mfululizo.” Hii ni kauli ya Salome Paul Mhando, mama wa watoto sita ambao ni pacha, aliowazaa kwa nyakati tofauti katika kipindi cha miaka sita iliyopita, wakipishana miaka miwili miwili.

Salome, alitelekezwa nyumbani na mumewe huyo baada ya kujifungua pacha kwa mara ya tatu, huku wakiwa hawana sehemu maalumu ya kuishi, achilia mbali njaa iliyotokana na umaskini wa kipato.
Baada ya kutelekezwa, msamaria mwema alijitolea kumhifadhi katika shamba lake lililopo eneo la Mabwepande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, kabla ya kupata msaada wa nyumba ya kuishi.

Mama huyo anayekumbuka tukio hilo kwa uchungu, anasimulia kuwa mumewe aliyemtaja kwa jina moja la Ali, alimtoroka saa saba mchana na kumwacha akiwa na pacha hao.
Anabainisha kuwa tukio hilo lilitokea baada ya familia hiyo kukaa na njaa kwa siku kadhaa kutokana na umaskini wa kipato.

“Siku hiyo, ambayo tarehe yake siikumbuki, mume wangu alirudi nyumbani akiwa tena hana chakula na kunieleza kuwa anaumwa. Nilipomwuuliza sasa tunafanyaje kuhusu chakula, alitoka nje,” anaeleza mama huyo na kuendelea:
“Nikaamua kumfuata na kuanza kumsema nikimdai chakula. Baadaye (mumewe) akaniuliza mbona unanisema? Mimi nikamjibu; naulizia masuala ya chakula, tunafanyaje leo? Akasema; basi niache naenda kukitafuta.”
Salome anaeleza kuwa kinyume na ahadi hiyo, tangu wakati huo alipoondoka hajaonekana nyumbani hadi sasa. “Niliamua kwenda kulala, lakini nikiwa na wasiwasi kuhusu usalama wake. Nikapatwa na hofu nikijiuliza; nini kimempata mwenzangu na kuanza kuwapigia simu ndugu zake ambao pia hawakupatikana.”

Salome anasema jitihada za kuwatafuta ndugu wa mumewe ziligonga mwamba na hadi sasa hana mawasiliano yoyote na familia hiyo ya mumewe.
Anaeleza kuwa kutokana na mumewe huyo kutorudi tena nyumbani, alilazimika kwenda kwenye vyombo vya habari kuomba msaada wa malezi ya watoto hao.
“Nilikwenda kwanza ITV ambako mbali na kunisaidia katika mahitaji ya msingi ya chakula, walinitangaza pia kwenye luninga kuwa ninahitaji msaada na tukio hilo ndilo limenisaidia kupata msaada wa kudumu.

Hali ikoje?
Salome anahusisha kutoroka nyumbani kwa mumewe na ugumu wa maisha unaoikabili familia hiyo.
“Nina watoto pacha sita; wawili wana umri wa miaka sita, wawili wengine wana umri wa miaka minne na wawili wa mwisho wana umri wa miezi 12. Nasikitika kukimbiwa na mume kwa sababu ya ugumu wa maisha, lakini zaidi akidai kuwa ninazaa sana. Maisha ni magumu na ninashukuru kwa misaada ninayoendelea kuipata kutoka kwa jamii, hasa kupatiwa msaada wa nyumba ya kuishi na wanangu,” anasema.

Akifafanua kuhusu ugumu wa maisha, Salome anasema ameshindwa hata kuwapeleka shule watoto wake wakubwa... “Hakuna anayesoma, wote bado wako nyumbani.”

Msaada wa nyumba
Hata hivyo, ugumu wa maisha wa Salome umeigusa Benki ya Covenant ya jijini Dar es Salaam, ambayo imejitokeza kumnunulia nyumba ya kuishi na watoto hao eneo la Mabwepande.

Mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo, Sabetha Mwambenja anasema mbali na msaada huo, anatamani kuona mume huyo aliyemtelekeza anapatikana na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Anasema benki yake ilitambua mahitaji ya mama huyo kupitia vyombo vya habari na kuamua kumpa msaada wa kumnunulia nyumba ya kuishi yenye thamani ya Sh25 milioni, ambayo alikabidhiwa juzi.

“Tumemkabidhi, nyumba, tukamnunulia magodoro, vitanda vinne, mashuka na taa za sola na familia nzima tumeikatia bima ya afya itakayowawezesha kutibiwa katika hospitali yoyote inayotoa huduma kupitia bima hiyo,” anaeleza mkurugenzi huyo.

“Sisi hatuna kitengo wala idara inayojishughulisha na matatizo ya jamii, tumeguswa tu na tatizo la mama huyo aliyekimbiwa na mumewe sababu ya kumzalia pacha. Natoa wito kwa benki nyingine na wadau mbalimbali wa maendeleo kuguswa na matatizo ya jamii inayowazunguka na kusaidia pale inapowezekana,” anasema.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Balozi Salome Sijaona anasema baada ya kuona mateso aliyokuwa akiyapata mwanamke huyo kwa kukosa makazi, chakula na mahitaji mengine ya kibinaadamu, waliona ni vyema kujitolea kumsaidia ikiwa ni moja ya kutimiza majukumu yake kwa jamii.

“Tumeguswa na mateso aliyokuwa akipata Salome Mhando, yeye pamoja na watoto wake, baada ya kutelekezwa na mumewe kwa kigezo ha kuzaa watoto pacha mfululizo. Tuliguswa na kuamua kujitolea kumnunulia nyumba ambayo ataimiliki mwenyewe,” anasema Balozi Sijaona na kuongeza:
“Nyumba hii tumemkabidhi pamoja na samani za ndani ambazo sasa zitamwezesha kuishi maisha ya amani na furaha akiwa kama wanawake wengine na kufurahi pamoja na watoto wake.”

Shukrani
“Ninaishukuru Benki ya Covenant kuniwezesha kumiliki nyumba yangu, ninawashukuru na ninaomba waendelee na moyo huo wa kuwasaidia kina mama wenye matatizo kama haya kwa sababu siko peke yangu,” alisema Salome na kuongeza:

“Kina mama tumekuwa na wakati mgumu katika ndoa zetu hususan katika masuala ya uzazi. Ninawashukuru watu wote ambao walijitolea kunisaidia chakula na nguo katika wakati wote nilipokuwa sina sehemu maalumu ya kukaa, hadi sasa ninamiliki nyumba yangu.”

MAHUSIANO: Huyu kaepuka matatizo ya kuishi na mume? kichekesho kweli kweli, kaamua kujioa mwenyewe

Bi Eleby
Yasmin Eleby hakupata mchumba wa kumuoa mtu ambaye alitaka awe mume wake atakapofikisha miaka 40--kwa hivyo akafanya kitendo ambacho kimewashangaza wengi, aliamua kujioa mwenyewe.
Kwa mujibu wa mtandao wa MySanAntonio.com,Eleby aliahidi kwamba ikiwa hatapata mchumba wakati atakapokuwa ametimiza miaka 40, basi atafanya harusi ya mtu mmoja yaani atajioa ili kusherehekea miaka yake 40.
Duru zinasema kuwa mwanamke Eleby alifanya harusi yake mwenyewe katika makavazi ya Houston akiambatana na jamaa na familia yake na wageni wengine waalikwa.

Kwa sherehe hii, dadake Eleby ndiye aliendesha sherehe hio, kwani ni kinyume na sheria kwa mtu kujioa mwenyewe. Harusi ya kawaida ni kati ya watu wawili.
Katika picha za kanisani sherehe ilionekana kuwa ya kawaida bila ya mchumba.
Kulingana na John Guess Jr afisaa mkuu wa makavazi hayo, sherehe hiyo ilionekana kuwa bila tashwishi na kuonekana kama jambo la kawaida kwani makavazi hayo huwakumbatia watu wa jinsia mbali mbali kuendesha harusi zao hapo.

Aliposikia kwamba Eleby, ambaye anaishi na kufanya kazi ugenini alikuwa anapanga kujioa mwenyewe, aliharakisha kwenda katika eneo hilo kujionea mwenyewe.
"Eleby alipofikisha umri wa miaka 40 bila ya kupata mpenzi na mtu mwenye nia ya kumuoa, aliamua angejioa mwenyewe,''alisema Guess Jr ambaye anasema harusi hiyo imewashangaza wengi na kuwa gumzo katika mitandao ya kijamii.

Anasema anakubaliana na Eleby na mtazamo wake wa mapenzi kwamba mtu anaweza kujipenda na kujioa kwa kukosa wa kumuoa kwani cha muhimu ni mtu kujipenda kwanza kabla ya kupendwa.
"watu wengu huolewa bila ya kutafakari mara mbili kuhusu yule anayemuoa, '' Guess Jr alisema.

Anadhani kwamba pindi watu watakapomuona Eleby anavyojishughulikia mwenyewe, huenda akapata ushindani.
"ni mrembo, anafanya kazi kwa bidii na anasifika duniani na pia anaona uamuzi wake umewapa gumzo watu wengi. ''

Wednesday, January 28, 2015

Ni kawaida kwa mzazi kujisikia upweke mwanae anapoenda shule boarding au collage

Mwanamuziki Madonna akiwa na watoto wake wanne, wapo wawili wa kuasili na wawili wa kibayolojia (kibongokibongo wa kuwazaa) kama unavyoona
'I was a mess': Madonna says she felt like she'd lost a part of herself when her eldest daughter Lourdes left home for college
Her eldest daughter Lourdes, 18, flew the nest to enroll in the University of Michigan last year.
And queen of pop Madonna, 56, says the emotional milestone left her 'a mess'.

During an interview with Australia's Today Show on Wednesday the mother-of-four spoke of the landmark occasion to entertainment editor Richard Wilkins: 'It's hard letting them go out into the world but when she left home to go to college I was a mess.'

Jinsi ya kuendelea kuwa na morali wakati wa kusafisha


Kwanza kabisa acha niseme kuwa roughly asilimia zaidi ya 90 ya watu kusafisha sio kazi ya burudani. Lakini ukweli ni kwamba, inatakiwa kusafisha kila siku katika maisha yetu, kwa ajili itaboresha maisha yako. Kwahivyo nikiwa nimeshasema hayo, ni muhimu kutopoteza mwelekeo.

Kwangu mimi moja ya kiburudisho kinachoniongezea morali wakati wa kusafisha ni mziki. Nasikiliza mziki wangu huku nafagia, na kinachofuata ni nini ujue? Mtu anashangaa nacheza huku nimeshika ufagio. Kusema kweli inaleta mabadiliko. Ulishawahi kuosha vyombo sehemu ipo kimyaaa, inaboa, unasafisha huku unawaza nitamaliza saa ngapi. Kwanini usiweke kiredio japo kidogo jikoni? Unaosha vyombo huku unakula mziki taratibu, mara unashtukia umemaliza.

Asante kwa kusoma na tutakutana kwenye tip nyingine.


Suluhisho la vifaa vya kuhifadhia kwenye sebule za kisasa

Eneo la kutosha la kuhifadhia kwa wamiliki wengi wa mijengo ni issue hasa pale familia inapoanza kukua, na ni tatizo hasa sebuleni. Kama tunavyojua sebule (zilizo nyingi) hazina closet au stoo lakini ni mahali ambapo familia nyingi zinatumia muda mwingi zaidi . DVD, matoy, game na vitabu ni baadhi ya vitu  vinavyotakiwa kuwa karibu pale mnapokuwa kama famili pamoja sebuleni mki enjoy family time. Kuwa na sehemu ya kuhifadhi vitu hivi vya ziada inaweza kuwa changamoto.


Suluhisho hili la kuhifadhi linaweza kuwa la kisasa zaidi na kuoana kabisa na muonekano wako wa sebule. Hizi ni vitu vinaitwa ottomans, na kwa vile vina matumizi zaidi ya moja, ni sahihi hata kwa sebule ndogo.
Zaidi ya kuongeza eneo la kuhifadhia vitu vidogodogo, ni rahisi kukisogeza na mgeni aliyezidi akakalia. 
Nilishatembela nyumba moja nikakutana na kama hiki, kina zipu kwa chini (huwezi kuiona kikiwa kimekaa kama hivi). Wenyeji walikuwa wanahifadhia nguo zilizowaruka watoto zikisubiri kuwa donated na wenyewe walikuwa wanakiita benki ya nguo. Kikaptula cha mtoto kikimruka unasikia kiweke kwenye benki ya nguo. Wakati huohuo mtu anakikalia sebuleni. So nice...
Pia unaweza ukaweka trei juu yake kutengeneza eneo flat ukasevu vitafunwa au vinywaji au kadi za kuchezea karata.

Tuesday, January 27, 2015

Interesting: Wanawake na wanaume wanapogombana twitter


Maelfu ya wanaume nchini Saudia wanajaribu kuwatoa wanawake katika mtandao wa twitter ,lakini juhudi hizo zinaonekana kuambulia patupu.

Ukandamizaji wa kijinsia nchini Saudi Arabia ni swala la kawaida na inaonekana baadhi ya watu wanajaribu kulipanua wazo hilo kufika katika mitandao ya kijamii.
Maneno yaliosema ''hatutaki wasichana katika mtandao wa Twitter'' yalitajwa takriban mara 400,000 wikendi iliopita.

Hata hivyo chimbuko la maeneo hayo halijulikani.
Lakini ajenda ya wazo hilo haikufanikiwa kwa kuwa wengi waliojiunga walikuwa wakipinga ukandamizaji huo wa kijinsia.
Wanawake walijibu nao kwa kusema ''kwa nini? Tumefanya nini''? .
Mwingine aliandika kwa kusema ''iwapo kungekuwa hakuna wasichana katika Twitter hakuna mwanamume ambaye angejisajili''.

Wanawake wengine pia walianza kusambaza ujumbe uliosema ''hatutaki wanaume katika twitter'', ili kulipiza kisasi lakini ilipata ujumbe 1,500 pekee.

Kama haya ni ya kweli huyu mama inabidi apimwe akili maskini, watoto wavyolia kweli wa kwanza na wa pili!!

    Mama aua watoto wake wawili kwa kuwanyonga 

JESHI la Polisi mkoani Tabora linamshikilia mwanamke aliyetajwa kwa jina la Zuhura Sudi (26) kwa tuhuma za kuwaua watoto wake wawili kwa kuwakaba shingo hadi kufa kisha kuwafunga kwenye sandarusi na kuwazika ndani ya nyumba yake.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Suzan Kaganda, alisema tukio hilo lilitokea juzi katika Mtaa wa Bakari, Kata ya Chemchem Manispaa ya Tabora.

Kamanda alisema, Zuhura anashikiliwa na Polisi kwa kosa la kuua watoto wake wawili Mwamvua Mrisho (miaka 4) na Sudi Mrisho (miezi minne).

"Mtuhumiwa aliwakaba shingoni hadi kufa kisha aliwafunga kwenye sandarusi na kuwafukia katika mashimo mawili tofauti aliyochimba ndani ya nyumba anayoishi," alisema Kamanda Kaganda.

Aliongeza kuwa mtuhumiwa amekamatwa kwa mahojiano zaidi na upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani. Alisema Jeshi la Polisi linalaani vikali kitendo kilichofanywa na mwanamke huyo.

Monday, January 26, 2015

Jinsi ya kuhamasika kusafisha



Kuhamasika kusafisha sio kitu rahisi eti. Baada ya ku practice kwa miaka mingi nimeweza kupata dondoo bomba za kukuhamasha kusafisha. Hapa ni tatu ninazozipenda zaidi:
 
Safisha asubuhi – Anza siku yako kwa kuweka mazingira safi ili uweze kuifurahia siku iliyobaki. Anza na ule usafi mgumu ili kukufanya usirudi kitandani.
 
Tenga muda wa kusafisha- Weka muda mchache pembeni kila siku kwa ajili ya kusafisha.
 
Epuka distractions wakati wa kusafisha- Kwa mfano zima simu na usikatize hadi umalize usafi wako, labda iwe ni kwa jambo muhimu sana. Usideki nusu ukasema ngojea ninywe chai kwanza.

Kwa hili gauni utadhani watu hawagombani kwenye ndoa

Kwakweli tokea nianze kufua gauni hili ni my favorite. Ikiwa ni ndoa ya wasiwasi hili hununui ( ni kwa mawazo yangu tu dho...)
 rangi yake ni off white
 shepu free kwahivyo hamna cha namba 8 wala 7. bibi harusi yeyote alilitinga atanoga
 kiunoni, unaweza dhani ni 2pieace kumbe sio

 kifuani utapenda
 kitambaa cha nje na cha ndani yake vyote quality sawa
 hata hiki kitambaa cha ndani kingekuwa cha nje ni sawa tu ubora wake
 lesi ya ndani
lesi ya nje

Saturday, January 24, 2015

Jamani muwape wadada wa kazi muda wa kutoka, soma anachofanya huyu

Msaidizi wa nyumbani mwenye umri wa miaka 18 katika mtaa wa Zimmerman, jijini Nairobi anakabiliwa na mashtaka baada ya kukiri kumlazimisha mvulana wa miaka mitatu kuramba sehemu zake nyeti.
Kwa mujibu wa jarida la The Nairobian nchini Kenya, mamaake mtoto huyo anasema kuwa mwanawe alionekana kuchanganyikiwa kila mara alipotoka kazini swala lililomlazimu kufanya uchunguzi.
Alipomuuliza mwanawe,alisema kwamba msaidizi huyo wa nyumbani alikuwa akimnyanyasa kijinsia.
Inadaiwa kuwa msichana huyo alikuwa akimlazimisha mvulana huyo kumramba sehemu zake za siri wakati mama yake anapoondoka.
Mfanyikazi huyo wa miaka 18 alikiri kufanya kitendo hicho kwa kuwa hakupewa mda wa mapumziko lakini akaomba kusamehewa.
Kwa sasa anakabiliwa na mashtaka ya kunajisi na amewachiliwa kwa dhamana ya shilingi millioni moja.Kisa hicho kinajiri baada ya kijakazi mwengine nchini Uganda kufungwa jela baada ya kupatikana katika kanda ya video akimnyanyasa kwa kumpiga mtoto mdogo.

Nyumba safi ni ipi?



Naulizwa hili swali mara nyingi. Nyumba safi ni ipi? Na acha nianza kwa kusema kuwa hakuna jibu sahihi!

Kila nyumba ina upekee wake na mahitaji tofauti kuendana na wakaaji.

Kwa mimi najibu kuwa nyumba safi ni ile ambayo hakuna vyombo vinavyoachwa vichafu iwe ni kwenye sinki, karo, beseni, ndoo, popote pale pa kuoshea vyombo kuendana na maisha unayoishi na nguo chafu hazijazagaa kila mahali sakafuni. 

Nina ratiba yangu ya mambo ya kufanya kwa siku kwa wiki na kwa mwezi kufanya mazingira yaonekane safi, maridadi na nadhifu bila kufanya kazi kubwa kwa wakati mmoja.

Kuna usafi wa kufanya kwa kipindi (sio kila siku) kwa mfano ndani ya friji na microwave. Najitahidi kupambana na uchafu palepale unapotokea ikiwa ni pamoja na kupitisha fagio na kushughulikia doa hasa palepale linapotokea. 

Hata kama sipo nyumbani huo ni utaratibu uliopo na unaeleweka kwahivyo sitegemei kuja nikute doa kwa mfano kwenye carpet.

lla ukweli ni kuwa hakuna aliyekamilika. Kwangu mimi nyumba safi ni nyumba nadhifu. Kila kitu kina eneo na kimerudishwa eneo lake mara baada ya kutumika. Haimaanishi kuwa sakafu zinadekiwa tena baada ya chakula cha usiku – hapana sina muda huo kwakweli. 

Tafuta ratiba ambayo itawezekana kwako. Na kama una mwezni au watoto set “house rules” na mshirikishe kila mmoja hapo nyumbani.


Kadri ninavyopata muda nitakuwa nawashirikisha vidondoo vya jinsi ya kusafisha mahali unapoishi.

Super saturday for the boys


Friday, January 23, 2015

Jinsi ya kujiweka mazingira bora ya mafanikio kimaisha (1)

Nimekutana na makala hii na nikaamini kuwa nikiiweka hapa wapo watakaojifunza kitu hivyo kuwawezesha kuvuka kwenda level ya juu, tunajifunza kila siku. Mwandishi wake ambaye ni Dr. Chris pia ni marriage cousellor

Na DK Chris Mauki

Mafanikio ya kweli ya binadamu yanahusisha maeneo kama  mafanikio ya kiuchumi, kama vile kuwa na uwezo wa kujikimu na kumudu gharama za maisha ya kila siku.
Tunapozungumzia mafanikio binafsi, tunalenga kwa upana maisha ya mwanadamu. Unaposema mafanikio, wengi wanaelekeza mawazo yao kwenye kuwa na fedha, nyumba, magari na utajiri.

Mafanikio ya kijamii ni kama vile kuwa na mahusiano bora na wanaokuzunguka.
Mafanikio ya kiroho ni kama vile kuwa thabiti kwenye mambo ya kiimani.
Mafanikio ya kihisia ni  kama vile kuwa na uwezo wa kujimudu kihisia na kadhalika.

Ili kujiwekea mazingira bora katika kuyaelekea mafanikio yetu binafsi ni vyema ufahamu na kuweza kufanya yafuatayo.
Kutambua umuhimu wa muda na jifunze kuukomboa na pia kuwa na malengo na kuyatumia katika kuyatekeleza.
Jambo hili ni lazima kufahamu kuwa kamwe huwezi kuukomboa muda kama hujui umuhimu wake. 

Labda tuuangalie muda katika mitazamo tofauti.
Mtazamo wa kiimani ama kiroho, kuukomboa muda kumezungumziwa ndani ya vitabu vitakatifu kwa namna mbalimbali.
Baadhi ya maandiko yanaonyesha kuwa hata ibilisi mwenyewe anatenda kazi akijua kuwa wakati wake ni mchache sana.

Maeneo mengine katika misahafu imeeleza kuwa kati ya hatua za juu za busara ya mwanadamu ni  kujua umuhimu wa muda na kuukomboa.
Tukiangalia mtazamo wa kimaisha, watu wengi wameshindwa kufikia malengo yao waliyoyatamani kwa sababu ya kufikiri kuwa muda upo tele na kwa hivyo wangeweza kufanya walichokitaka wakati wowote na wakisahau ukweli kuwa muda ni mchache katika kila tunachotaka kukifanya.
Wenzetu Waingereza wana msemo usemao “There is little time for everything” wakiwa na maana kwamba kila sekunde, dakika inapaswa kutumiwa vizuri.

Kwa kutofahamu umuhimu wa muda wengi wetu wamekuwa wakifikwa na kihoro pale wanapokaribia kustaafu maana hamna walichokifanya wakiwa kazini.
Mara nyingi ninawashauri watu kuanza kuelekeza mawazo katika ile siku ya kustaafu mara tu unapoajiriwa.

Ukisubiri uwaze na kujiandaa kustaafu muda mchache kabla utajikuta unachanganyikiwa. Hii itakuwezesha kuelewa umuhimu wa muda mdogo ulionao kazini na namna ya kuukomboa ili usije kukuathirika baadaye.
Ni vyema ukifahamu ukweli kuwa uko vile ulivyo na jinsi ulivyo kwa kulingana na vile unavyoutumia muda wako.

Tumia muda wako kuwekeza katika busara na ufahamu, mfano; shule na kazi.
Katika  kutafuta kuwa na busara ni  lazima kufahamu kuna wakati wa kila jambo chini ya  jua na  lahitajika kutendeka au kufanywa katika muda wake mwafaka.
Wengi wetu tumepata hasara katika miradi mbalimbali maana tumeshindwa kujua muda mwafaka wa kuanza au kumaliza shughuli fulani au biashara  fulani.


Wiki ijayo tutaendelea na mada hii ya jinsi ya kujijengea mazingira bora kwa maisha ya baadaye kwa kuingia sehemu ya pili ya ‘Jifunze kuongozwa na malengo.’

MAHUSIANO: Tofauti ya kipato baina ya watarajiwa inaweza kusababisha haya mbeleni?

Kisa cha wapenzi wawili waliozua gumzo nchini Kenya
Sarika na mume wake Timothy wameachana baada ya Sarika kudai kwamba mume wake amekuwa akimdhulumu
Msichana mhindi Sarika Patel kutoka familia tajiri na Timothy Khamala mbukusu kutoka familia maskini kutoka Magharibi mwa Kenya kuoana? wakati yao mapenzi yao yalijulikana kama Bukusu Darling, sifa kwa wanakoishi wawili hao.
Taarifa sasa ni kwamba mapenzi yao yamefika kikomo. Familia ya msichana Sarika ililaani sana mapenzi hayo kwani Timothy alikuwa anafanya kazi kwao kama mfanyakazi wa nyumbani.
Na Sarika alipoamua kwenda kuishi na Timothy kama mume na mke familia yake ilimfukuza na kisha kumfuta kazi Timothy.
Wawili hao walioana kinyume na matakwa ya familia ya Sarika ambayo kwao ilikuwa ni kama aibu kubwa sana kwa mtoto wao kutoka familia tajiri kuolea na kijana asiyekuwa na mbele wala nyuma.
Wakati taarifa ya wawili hao ilipogonga vichwa vya habari nchini Kenya, Sarika na mume wake walipata kazi katika kiwanda cha kutengeza Sukari kutoka kwa wahisani.
Lakini sasa kuna madai kwamba ndoa yao imevunjika baada ya Sarika kulalamika kwamba Timothy amekuwa akimdhulumu na kumtusi kila mara hali iliyosababisha wawili hao kutalakiana.
Mtandao wa Standard Digital umemnukuu Sarika akisema: "nilipokuwa mgonjwa , hakuwa hata na muda wa kunipeleka hospitalini badala yake wazazi wake ndio walionipeleka kutafuta matibabu. Mbali na hayo amekuwa akinichapa, '' alisema Sarika huku akibubujikwa na machozi.
Kwa sasa inaarifiwa anajuta sana kwa nini alikaidi amri ya wazazi wake.
''Ninajuta sana kwa nini sikuwasikiliza wazazi wangu na kuolewa kinyume na mapenzi yao. Ninaomba radhi, natumai watanikubali kurejea nyumbani. ''
Sarika ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano, ameamua kurejea nyumbani na kusema kamwe hatawahi kuwa na uhusiano wa kimepenzi tena. Lakini wazazi wake wamempa masharti, mwanzo aishi na rafiki yake huku akifanya uamuzi wa mwisho kuhusu anakotaka kuishi.
Anasema anahofia kwamba jamii ya wahindi haitamkubali tena kwani hakuwasikiliza wakati walipomshauri kutoolewa na mwanamume mwafrika.

MAHUSIANO: Majivu kwa ajili ya kuzuia mimba?! Wanayalamba??


Baadhi ya wanawake wanaamini kwamba wakitumia njia za kisasa wanaweza kuharibu maumbile yao ya mwili ya asilia pamoja na kupata ulemavu.
Wapo wanaoamini kuwa uzazi wa mpango upo kwa ajili ya kupunguza idadi ya watu kwa kuua mayai ya uzazi pindi watakapotumia dawa za kisasa kama kuchomwa sindano, kumeza vidonge, vipandikizi na kuwekewa kitanzi.
Kutokana na kuamini njia za kisasa zina athari kwa afya zao, baadhi ya wanawake hususan waishio vijijini wanatumia majivu kama njia ya kuzuia kupata mimba.
Hali hiyo imekuwa ikichochewa na waume zao kutowaruhusu kutumia njia za kisasa za uzazi wa mpango. Wapo wengine wanakoroga bluu na kunywa pindi wanapohisi wamepata mimba ikiwa ni imani ya kwamba mimba itaharibika.
Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ina hospitali moja iliyopo Mwadui  maeneo ya mgodini. Wilaya hii pia ina vituo vya afya  vinne, zahanati 45 za Serikali na  nne za  watu binafsi.
 Wanawake katika vijiji vya Ilebelebe, Ikoma na Itilima wanaeleza kuhusiana na mikanganyiko hii ya njia za uzazi wa mpango.
Wanawake wanasema nini?
Mkazi  wa Kijiji cha Ilebelebe, Suzana Mhoja (37) mwenye watoto sita anasema baadhi ya wanaume  wamekuwa chanzo cha wanawake kushindwa  kutumia  uzazi wa  mpango kwa kuhofia kuvunja ndoa zao  kutokana na kutoruhusiwa kwa imani kuwa wataua mayai  ya  uzazi.
Anasema yeye ni miongoni mwa wanawake waliowahi kutumia majivu kama njia ya kuzuia kupata mimba baada ya kupata taarifa kutoka kwa wanawake wenzake.
Anasema licha ya kutumia majivu, alibeba ujauzito kabla ya muda wa miaka miwili aliokuwa amepanga uwe na wa kupumzika ili kutoa nafasi ya kulea aliyetangulia.
“Sitamani tena kuendelea kuzaa lakini wanaume hawataki kabisa kusikia suala hilo la njia za mpango wa kisasa. Ningeweza kutumia kwa siri lakini nahofu ya kuvunja ndoa yangu,” anasema.
Wakazi wa Kijiji cha Ikoma, Sophia Maige (29) na Salume Mshamindi (33) wanabainisha kuwa kama huduma za afya zingekuwa katika kila kijiji, uzazi wa mpango ungefanikiwa vizuri kwani elimu ya uzazi wa mpango ingewafikia wanaume kwa urahisi tofauti na ilivyo sasa.
Chanzo: Mwananchi

Hizi ni mifano ya sofa mbalimbali kwa watu wa lifestyle mbalimbali

Kuanzia kulala wakati unatizama TV hadi "kufanya" kazi zako za ofsini, sofa ni fenicha ambayo inatumika sana nyumbani kwahivyo kununua  ya kudumu na kuendana na maisha unayoishi ni big deal. Kuna vigezo vya msingi vya kutafiti kabla ya manunuzi (fikiria: fremu, spring na cushion, kama utataka kujua zaidi tembelea GoodHousekeeping.com kwani sio lengo la post hii kwa sasa).

Sasa basi lengo ni kuangalia sofa mbalimbali kwa lifestyle mbalimbali:
 Sofa kama hili ni kwa wale wanaopenda rangi, wanaopenda kupamba yani akiona decor item yoyote colorful anasuuzika moyo.
 sofa hii ni kwa couple inayochukua muda mwingi kuangalia TV pamoja, na mara nyingine kunakuwa na argument za hapa na pale, hadi miguu wanaiweka juu ya meza
 Hii ni kwa yule anayependa kupata kiusingizi cha mchana kwenye sofa
 Sofa mfano huu utamfaa mwenye sebule ndogo.
 Kama una wageni wengi sofa ya rangi hii inakuhusu, kuna wageni wanafikia hadi kunyanyulia miguu kwenye sofa, mwingine katoka alikotoka na vumbi limemjaa miguuni lakini kwake sio issue.
Wewe bachelor ambaye hujajua kama mke wako mtarajiwa atapenda ulivyo navyo ama laa sofa kama hii ni sahihi kwako. Yenyewe iko simple kwahivyo hata kama akiidis mwenyewe hutajuatia mnanunua tu nyingine.

Kicheko cha kuanza furahi day

Marafiki zangu wa ukweli wakielekea shule asubuhi hii. Wenyewe wanafurahi kwamba kesho hawaaamki na giza.