Friday, January 9, 2015

magugu ni adui wa bustani yako

ukiyalazia macho magugu yanaharibu bustani nzima...... leo nimestuka jinsi mvua ilivyoyafanya yashamiri kwenye bustani yangu. halafu usijidanganye kuwa nitakapokata majani hayataonekana, bila kuondoa mizizi gugu lipo pale pale...
aina hii ya  magugu yana majani mapana kuliko majani ya bustani ambayo ni aina ya canadian
 haya ni magugu aina nyingine ambayo kwenye jua yanafanana kabisa na canadian grass, jinsi ya kuyagundua tu ni asubuhi wakati wa umande, huwa yenyewe magugu yanakuwa yameweka ukungu wakati canadian zinakuwa hazina, kwahivyo ukiona hivyo unajua eneo hili lina magugu.
hizi ni canadian grass ambazo hazina magugu kabisa, raha ya majani haya ya bustani huwa yanashona na ni ngumu kweli kwa gugu geni kuota, yanayokuwepo ni yale tu ambayo toka mwanzo wa kuotesha bustani mizizi ya hilo gugu ilibaki ardhini
 gardener wangu Claud aking'oa mzizi wa gugu
finally nimebakiwa na gugu free bustani

No comments:

Post a Comment