Wednesday, January 21, 2015

MAHUSIANO: Hili sijui lina ukweli kiasi gani, soma hapa sentensi 4 ambazo single women hawataki kuzisikia

1. "Kwanini bado upo single?"
Bibie Mary ni single lady na alikuwa na haya ya kusema:
Yani ni kuwa hamna jibu zuri lolote kwa swali kama hili. Kwanini niko single? Sijui. Labda….Kwasababu tu nipo…Kusema kweli sina cha kukujibu.
Na unataka mtu akujibu kwa undani ni nini kinawakimbiza wanaume pale tu wanaponijua kwa undani? Yani unataka nirudi hatua nyuma kwenye mahusiano yangu yaliyopita kuanza kutafuta makosa ambayo yamenifanya nisiwe nimeshavaa shela? Au unaniuliza tu hili swali kwa kudhani kwamba mimi  mwenyewe hajiulizi?
Pengine labda umeniuliza hili swali kwa kutaka kunisifia kuwa nina mvuto au hata pleasing personality (hii ni ile tu kuwa yeyote akikuona hata kama hujaongea au kufanya chochote anavutiwa nawe), basi kama hoja ndio hiyo nisifie tu bila kuuliza swali hili, inatosha.
2. "Muda unakutupa mkono/miaka inaenda."
Unajuaje kama ninatamani kuwa na mtu, kwani inakuhusu?

3. "Unachagua sana."
Hii inatokea kwa wale wanaojidai kuwa wanamjua sana mhusika na kumbe hawamjui hata kivile. Hoja kwamba watu wawili wa jinsia tofauti wako single haiwafanyi kuwa wataweza ku mingle wawe pamoja, moja ongeza moja ni 2 lakini moja mara moja sio 2…vigawe vingine pia vinatumika sio jumlisha tu!

4. "Unatakiwa kujichanganya zaidi."
Mary anakuambia, nimehudhuria chuo, sekondari, kanisani, makongamano na hadi party za singles, nimesaini online site za dating, nilienda kwenye first dates nyingine mwaka uliopita kuliko mtu yeyote anavyoweza kwenda. Tafadhali usiniambie tena eti bado nipo single kwa ajili sijichanganyi.


Utafiti unasema kuwa 63 percent ya wanandoa walikutana kupitia marafiki. Wanandoa wengi walikutana kwa ajili marafiki zao waliwa introduce kwa waliokuja kuwa wenzi wao. Kwahivyo siko single kwa kuwa nimezubaa ila huenda niko single kwa sababu yako. Itasaidia zaidi, badala ya kuwaambia wanawake single wajichanganye zaidi, host nyama choma au dinner nyumbani kwako na uwa introduce warafiki zako wa kike walio single kwa eligible bachelors unaowajua.

No comments:

Post a Comment