| WAKAZI wa kijiji cha Kidago katika Halmashauri ya wilaya ya Morogoro | |
| ambao walivunjiwa makazi yao kwa kile kinachodaiwa kuvamia shamba la | |
| mwekezaji Martin Shem, wameiomba serikali na vyombo vya usalama mkoani | |
| Morogoro kuwawekea ulinzi. | |
| Wamesema hali hiyo inatokana na kupokea vitisho kutoka kwa mwekezaji | |
| huyo, hali inayowafanya waishi kwa wasiwasi. Januari 10 mwaka huu kaya | |
| 45 zenye wakazi 180 katika kijiji hicho walivunjiwa makazi yao kwa amri | |
| ya Mahakama kwa madai ya kuvamia shamba la mwekezaji huyo. | |
| Wakizungumza katika mkutano wa hadhara mara baada ya kutembelewa na | |
| Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, wakazi wa hao wamemuomba | |
| kamishna wa ardhi nchini kushughulikia kwa haraka mgogoro uliopo katika | |
| shamba namba nne ili iweze kujulikana nani mwenye haki ya umiliki. | |
| Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Morogoro aliwataka wakazi wa kijiji | |
| hicho kutokuwa na wasiwasi na kuwataka waishi kwa amani kwani jambo hilo | |
| serikali inalishughulikia. | |
| Aidha aliwataka wakazi hao kuendelea na shughuli za kilimo katika | |
| shamba hilo wakati Serikali ikiendelea na utaratibu wa kuirudisha ardhi | |
| hiyo mikononi mwa wananchi hao. | |
| Awali katika kikao cha wadau wa ardhi pamoja na makamishna wa ardhi | |
| kilichofanyika mkoani hapa, Naibu Waziri wa Ardhi, George Simbachawene | |
| alishangazwa na kitendo cha mwekezaji huyo kuvunja makazi ya wananchi | |
| hao na hivyo kuziagiza mamlaka husika kushughulikia suala hilo ili | |
| kuondoa mgogoro uliopo. | |
| Mgogoro wa shamba hilo lenye ukubwa wa ekari 1,080 ulianza tangu mwaka 1999 ambapo hadi sasa haujapatiwa ufumbuzi. |
Sunday, February 9, 2014
News Zihusuzo Makazi/Nyumba: Wakazi waomba ulinzi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment