Saturday, March 12, 2022

Nuh Mziwanda Aomba Pambano la Ngumi na Shilole

Baada ya mwanadada Shilole kutamba kumtembezea kipigo mume wake wa zamani Nuh Mziwanda iwapo atazidi kumfuatilia, naye Nuhu amevunja ukimya kwa kuomba pambano na mke wake huyo wa zamani.

"Manake hapo kwanza ncheke, Mziwanda mimi au mwingine? naomba pambano viwanja vipo vingi tu nikuonyeshe show mama Ntilie. Kwanza nina hasira na wewe ulinipiga Leaders club ukijichanganya tu nakufumua vibaya sana," aliandika Nuhu

Kwenye mtandao wa instagram mara kadhaa Nuhu amekuwa akimtuhumu Shilole ambaye kwa sasa ni mke wa mpigapicha Rommy 3D, pia mwanamuziki na mfanyibiashara ya kupika chakula kuwa alikua anajihusisha na mambo ya kishirikina enzi ya penzi lao.

No comments:

Post a Comment