Thursday, March 10, 2022

Ufafanuzi wa Hospitali ya Muhimbili Kuhusu Kusambaa Video ya Mgonjwa Profesa Jay

Hospitali ya Taifa ya Muhimbili imetolea ufafanuzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Joseph Haule maarufu Profesa Jay na kusema kuna video inayosambazwa na mtandao wa Mange Kimambi ikimuonesha Profesa Jay akipatiwa matibabu Muhimbili Hospitali Upanga.

Uongozi wa hospitali unatoa taarifa kuwa video hii haijarekodiwa na kusambazwa na hospitali, tumesikitishwa na tunalaani vikali kitendo hiki cha kumrekodi mgonjwa anayepigania uhai wake ICU na kuisambaza, hiki ni kiwango cha juu cha kukosa utu na maadili.

"Tunafuatilia kwa ukaribu tukio hili ili kubaini chanzo cha video hiyo ili hatua stahiki zichuliwe, wananchi endeleeni kuwa na imani na hospitali ya Muhimbili." imeeleza taarifa iliyotolewa an hosptali ya Muhimbili.

No comments:

Post a Comment