Friday, March 11, 2022

Kuhusu Diamond Kumuoa Zuchu Haiwezekani - Sallam

Siku ya jana kwenye uzinduzi wa EP ya Diamond Platnumz meneja wake Sallam alitoboa siri kwamba Diamond na Zuchu hawawezi kuoana kwasababu wao wanafanya biashara na Diamond ni boss wa Zuchu.

Ishu nzima ilianza hivii: Wakati Diamond alipokuwa anatumbuiza kwenye ngoma yake mpya ya Nawaza, katikati ya tukio meneja wake Bwana Salaam akasema kila mtu atoe dukuduku lake aseme anawaza nini. Ndipo kaka wa Diamond, Romy Jons akachomekea kuwa nawaza Diamond atamuoa Zuchu na ndipo Sallam akajibu kwamba haiwezekani kwasabbau yeye Diamond ni bosi na wanafanya biashara.

No comments:

Post a Comment