Monday, March 14, 2022

Mama Diamond Azima Kelele za Kuwa Hapendi Mahusiano ya Mwanae na Zuchu

Ingawa ni muda kiasi toka kumekuwepo na gumzo mitandaoni ya tetesi za mahusiano ya mapenzi kati ya Diamond Platnumz na msanii wake Zuchu, baada ya kutoka kwa wimbo wa Mtasubiri ambao Diamond kaimba kwa kumshrikisha mwanadada huyo uliopo kwenye EP FOA ya Diamond wadau wanaona ni kama umethibitisha tetesi hizo.

Wawili hao wamezungumziwa sana kuhusu mahusiano ya mapenzi yaliyodaiwa kuwepo huku mashabiki wengi wakiamini kwamba wimbo huo umethubitiaha uwepo wa penzi.

Wadau wa mitandaoni wakawa wanadai Diamond anashindwa kujiachia kwa kipenzi chake Zuchu kwa kuweka mambo peupe kwa ajili anamuogopa mama yake almaarufu Mama Dangote kwa ajili tetesi zinadai hayapendi mahusiano hayo. 

Na tetesi hizo zikapaliliwa zaidi na kitendo cha Mama Dangote kutom follow instagram msanii huyo wa kike pekee kwenye lebo ya mwanae.

Leo jumatatu March 14 Mama Dangote amepost video ikimuonyesha Diamond na Zuchu wakiimba wimbo wa Mtasubiri ambapo wadau wa mambo wanatafsiri kama ni ameamua kukata mzizi wa fitna.

Mdau nini maoni yako je kwani kuna nongwa yoyote endapo mzazi anaingilia penzi la mwanae?

No comments:

Post a Comment