Friday, March 11, 2022

Skendo kwenye Ep Ya Diamond Nawaza Kutishia Ndoa Ya Lulu na Majizzo?

EP mpya ya Diamond Platnumz FOA aliyoiachia usiku wa jana kuamkia leo imeibua skendo ya kuwepo kwa clipu za mapenzi kati ya Elizabeth Michael "Lulu" na Rayvanny hali iliyopelekea maswali mengi kwa mashabiki.

Wakati huohuo Majizzo ambaye ni mume wa Lulu kafuta posts zake kwenye ukurasa wake wa instagram akizokua amemsifia mkewe huyo ikiwemo ile ya siku ya wanawake na ya anniversary ya mwaka mmoja wa ndoa yao.

"Nawaza Vanny na Eliza clip zao zikivuja, ndoa itaimarika eti au wataivunja?" hii ni vesi iliyozua gumzo.

Aidha pia kuna baadhi ya video zinazosambaa kwenye mitandao zinazoonyesha kuwepo kwa uhusiano wa karibu kati ya Lulu na Ray.

No comments:

Post a Comment