Tuesday, April 27, 2021

FAHYMA ATANGAZA RASMI KUACHANA NA RAYVANNY: Namna ya Kusonga Mbele Pale Penzi Linapoisha

 follow instagram @vivinavisavyake



Kifo cha mahusiano yaliyokuwa ya maana na ya muda mrefu hakina tofauti sana na kifo cha binadamu. 

Tena unaweza kusema huenda kifo cha binadamu kina angalau kwa kuwa baada ya kuomboleza ni kwamba hautawasiliana wala kumuona tena binadamu huyo duniani. 

Kifo cha mahusiano na mtu ambaye mmezaa kinauma kwa wote wawili yani muacha na muachwa au hata iwe ni kuachana yaani wote kukubaliana kwamba hapa mambo hayaendi tena hivyo tusambaratike tu.

Hivyo basi, inawezekana vipi kusonga mbele baada ya kifo cha mapenzi. Fanya yafuatayo

1. Omboleza. 

Yani omboleza hadi umalize ukitoka hapo ni baibai mbele kwa mbele na maisha

2. Jijenge zaidi kiuchumi. 

Hii itakusaidia kuwa busy na shughuli zako hivyo kutokupa muda wa bure wa kumuwaza mpenzi mlieachana.

3. Usimsema vibaya kwa watu na mbele ya jamii. 

Hii inahusika sana hasa kama mmezaa kwani mnahitaji bado kuwa na mawasiliano na mahusiano mazuri kwa ajili ya mlezi wa mtoto wenu.

Mbinu nyingine njoo tuongee ili uweze ku move on mazima. Simu0755200023

Monday, April 26, 2021

Dida Achumbiwa

follow instagram @vivinavisavyake




Mtangazaji wa kipindi cha mashamsham mrembo Dida Shaibu wa radio wasafi amechumbiwa.

Dida amekua ni mrembo mwenye bahati ya ndoa ambapo ameshapitia ndoa kadhaa kama pia ilivyo kwa watu wengine maarufu mfano Shilole na Hadija Kopa. 

Mdau je, ni muda gani ukiwa na mpenzi ukiona hamvalishani pete utabwaga manyanga?

NIMEREJEA WAPENZI

Nifollow instagram @vivinavisavyake

Hatimaye viblog vyetu na vi you tube vya kupost kazi zetu vimerejea tena. Karibuni tena wapendwa wangu tuyadadavue mahusiano na visa vyake vyote.