Saturday, February 28, 2015

----nitavukaje----Kutoka Sales Manager hadi Business Owner

Solar panel ikifungwa juu ya paa
Benard ni mmliki wa kampuni ya vifaa vya kufunga umeme wa jua kwenye majengo ya makazi na ya biashara. Anasema alichosomea yeye ni Environmental Science na alipotoka shule aliajiriwa kama sales manager kwenye kampuni iliyokuwa ikihusika na solar energy. Baada ya miaka sita akaamua kujiajiri.

KAPTENI JOHN KOMBA AFARIKI DUNIA JIONI HII DAR ES SALAAM

Marehemu Komba akiongea na wanahabari nyumbani kwake 2012
MBUNGE wa Mbinga Magharibi, Kapten John Komba amefariki dunia jioni hii jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amethibitisha kutokea kwa kifo hicho, hata hivyo hakuwa tayari kuelezea kwa undani kwa madai kuwa taarifa hizo zimemfikia sasa hivi.
Mmoja wa watoto wa Komba ambaye aliyejitambulisha kwa jina la Herman amethibitisha kutokea kwa msiba huo na akasema, huku akilia, msiba wa baba yake upo nyumbani kwake Mbezi Tangi Bovu, Dar.

Mtoto wa Sokoine ataka jimbo la Lowassa

Namelock Sokoine
Mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametangaza nia ya kutogombea tena jimbo hilo, hali ambayo imeibua mvutano kwa makada kadhaa wa CCM wilayani Monduli. Namelock alikuwa mmoja wa watoto kipenzi cha hayati Sokoine.

Usiamini kila unachosoma kwenye mitandao, gauni la Lupita halikuwa la lulu (pearl) na wala sio thamani iliyosemwa ya $150,000

Gauni la Lupita lililoibiwa limerudishwa kwa ajili wezi wamegundua halina thamani. Mbunifu Calvin Klein hakuwahi kusema thamani ya hilo gauni wala hakusema kuwa zile shangashanga ni lulu ila stylist wa Lupita ndiye aliyewaambia watu. Endelea kusoma

FURAHISHA GENGE: Kabla ya social networks tulikosa mengi


Rejea post yangu ya jana ya mashabiki wa Beyonce wanaoitwa Beyhive waliovamia account ya Kidrock na kugeuza kila post kuwa na vipicha vya nyuki. Basi Kidrock naye kaamua kuwaletea Raid kuua hao nyuki. 

Hivi ukisoma vitu kama hivi unavyocheka mwenyewe unajiuliza ni kwa vipi tulikosa raha ya maisha kabla ya mitandao ya kijamii? Sijui huko mbeleni teknolojia imebeba nini kwa walimwengu..

DC Makonda kutinga kortini kwa kosa la kutukana na kudhalilisha wenzake

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.
Viongozi wawili wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wanakusudia kumfikisha mahakamani Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, Jumatatu ijayo kwa madai ya kuwakashifu, kuwadhalilisha na kuwatukana.

Friday, February 27, 2015

FURAHISHA GENGE: Usithubutu kumgusa queen wa Beyhive

Mwanamziki Kidrock alikuwa anapromoti albam yake kwa kumponda Beyonce kuwa yeye Bey si lolote kwenye mziki. Basi mashabiki wa Bey instagram wanaoitwa Beyhive wakachukia wakashambulia account yake  ya Kidrock ambapo kila post imekuwa kama hivi kwenye picha. Hawa Beyhive hawana mchezo na wana muda, kabla mtu hajamponda queen wao inabidi afikirie mara 2 . So interesting!

PICHA: Sanaa ya ukutani ya mchoro

Picha ya ukutani ya mchoro wa maua huwa haipitwi na wakati kwakuwa maua daima dumu yanapendezesha nyumba.

PICHA: Uko tayari kubadili rangi ya makabati ya jikoni?

Kitu cha pale bluu unakionaje? Kinafanya jiko lionekane tulivu. Halafu huyu ukuta wake mfupi kwahivyo kabati zake za juu zimeenda hadi zikagusa ceiling. Imependeza ..

Kilimanjaro waongoza kwa kutelekeza familia

Mkuu wa mkoa wa kilimanjaro, Leonidas Gama.
Jamani ya kweli haya? Wachaga tunaenda kuhangaika kutafuta masha na sio telekezo...

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza kwa ukatili wa kijinsia wa utelekezaji familia kutokana na waume kufukuza wake zao na watoto na kuchangia ongezeko la watoto wa mitaani.

Diwani adaiwa kumpiga mjamzito wilayani Kinondoni

DIWANI wa Kata ya Saranga wilayani Kinondoni, Ephraim Kinyafu (CHADEMA) anadaiwa kumshambulia kwa mateke na fimbo, Aisha Mosses, ambaye ni mjamzito akimtuhumu kuwa ni mamluki.

PICHA: Ajali iliyoua watatu Mikese barabara kuu ya Morogoro-Dar

Askari wa Kikosi cha Zimamoto, wakizima moto baada ya lori la mafuta kupinduka kisha kuwaka moto na kusababisha watu watatu kufariki dunia eneo la Wedi, Kijiji cha Maseyu, Tarafa ya Mikese katika Barabara Kuu ya Morogoro-Dar es Salaam jana. Picha na Juma Mtanda, Mwananchi

PICHA: Wewe mume ambaye humpetipeti mkeo jifunze hapa. Kila mke anahitaji kuonyeshwa malavidavi

Picha nyingi za Kanye huwa anamshika mkewe kama vile anamzuia asianguke au kujikwaa kama vile mzazi anavyokuwa makini na mtoto anayejifunza kutembea. Mi nadhani ni malavidavi haya, we unaonaje?

FURAHISHA GENGE: Hii sweta ni panya au?


Polisi inamsaka mwanaume wa Rombo aliyemuua mkewe na kumfukia kwenye zizi la ng'ombe

POLICE here are looking for a 43-yearl-old man, Peter Mroso, a resident of Ubetu village in Rombo district who reportedly killed and buried his wife inside the family cowshed.

PICHA: Na predict fashion inaelekea huku. Mafashionista mpoo

Jamani maceleb wetu watakavyoanza kutinga vivazi kama hivi msiwaseme kwa ajili hata wenzao wa mambelez wanajimwaga kama hivi.

 Draya Michelle
Irina, model wa zamani wa Victoria secret na pia ex- girlfriend wa Cristano Ronaldo

Thursday, February 26, 2015

Eti lile gauni limeibiwa hotelini!!

Oh no, jamani isiwe kweli, Lupita Nyong'o's now-famous Oscar dress -- adorned in pearls -- was stolen right out of her hotel room ... TMZ has learned.

Beyoncรฉ And Jay Z Are Paying $150,000 A Month To Rent This L.A. Mansion

Beyoncรฉ and Jay Z have called New York City home for years, but it looks like the celebrity couple will be spending a lot more time on the West Coast after signing a one-year lease for a stunning mansion in Los Angeles.

Mwanaume ajitolea kutoa ubikira siku ya wanawake

Kwani wanaume huwa wana bikira?
Kutoka BBC:
Mwanamume mmoja amejitolea kutoa ubikira wake wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake.

Dawa ya kupaka ili kuzuia HIV haifai

BBC inaripoti kuwa:
Dawa iliyokisiwa kupunguza uwezekano wa mwanamke kupata virusi vya HIV wakati wa tendo la ngono haifai,kulingana na utafiti mkubwa uliofanywa na shirika la Follow on Africa Consortium for Tenofovir kutoka Afrika kusini.

Kesi ya madawa ya kulevya: Chid Benz huru, alipa faini laki 9


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imemwachia mwanamuziki Rashid Makwilo 'Chid Benz' baada ya kulipa faini ya sh. 900,000 kufuatia kukamatwa akiwa na madawa ya kulevya.
Chid Benz alikamatwa mwaka jana katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akiwa na madawa ya kulevya, ikiwemo misokoto ya bangi.

Mwanamuziki huyo ambaye alikiri kosa hilo wiki iliyopita, alikamatwa uwanjani hapo akiwa anajitayarisha kupanda ndege kwenda Mbeya kwenye tamasha la muziki.

Unavyoweza kuboresha sebule yako haraka na kwa gharama nafuu

Kama unatafuta njia rahisi na haraka ya kuboresha sebule yako basi makala hii inakuhusu. Utapata mawazo hapa ya kubadilisha muonekano wa sebule uwe bora zaidi kwa haraka, bila gharama kubwa na bila wataalam.

Hongereni Kevin & Elizabeth kwa kutimiza miaka minne ya ndoa

Kevin ni mshindi wa BBA toka Nigeria ambaye alimuoa mshiriki mwenzie Elizabeth toka Tanzania ambapo walikutana mjengoni 2009 na wakaoana 2011, wana watoto wawili pamoja wa  kike na wa kiume. Hongereni big time.

Kijana mtoto anatafuta mke. Usijali umbilikimo wake kwakuwa ana utajiri wa mifugo ...inapendwa pochi sio mtu...joke

Lebohang Tlahali with his cousins Lefa and Lucky Tlahali. Photo by Modiri Michaels
Kutoka Dailysun:
LEBOHANG Tlahali has a big problem. He’s 33 years old but he has the body of small boy!

Mwanafunzi amuua mwenzake darasani wakigombea daftari

Mara kadhaa nimeshasikia au kusoma mtu kuangukia kisogo akafa, inasikitisha kwakweli.

MWANAFUNZI wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Ilola, Wilaya ya Shinyanga Vijijini, Mkoa wa Shinyanga, Veronica Venance (12), amefariki dunia baada ya kupigwa na mwanafunzi mwenzake wakati wakigombea daftari darasani.

KUTOKA KWANGU: Jinsi unavyoweza kuipa sebule yako identity

Kama wewe ulivyo na kitambulisho na sebule yako vilevile yaweza kuwa na kitambulisho chako. 

Zifuatazo ni njia chache kwa ufupi sana unazoweza kukamilisha kitambulisho chako kwa sebule yako.

Weka vitu vya ladha yako, yaani vile unavyopenda wewe bila kufuata kanuni uliyosoma popote. Hii inaweza kuwa ni fremu za picha za familia au kama ni mpenda sanaa za ukutani basi tundika. Unaweza pia kutundika nukuu (quotes) unazozipenda. Nukuu hizi labda ulizisikia kwa mwalimu wako wa primary, au popote ziandike, zitengenezee fremu zitundike, kumbuka pia hata rangi ya hizo fremu inahusu utambulisho wako, labda unapenda orange, nyekundu nk.

Kama unasafiri sana sehemu mbalimbali za dunia, unaweza kujumuisha sebuleni kwako chochote toka nchi hizo ulichonunua ulipokuwa huko.

Polisi Arusha wakodishwa kuvunja mikono ya mdaiwa wa sh 250,000/

Mkazi wa Loksale, Samweli Shani (47), akiwa amefungwa POP baada ya kuvunjwa mikono yake na polisi, kushoto ni ndugu yake Gabriel Shani akionyesha picha za X-ray alizopigwa zikionyesha jinsi mikono ilivyovunika.

Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas, amekiri kupokea malalamiko ya mkazi mmoja wa Loksale wilaya ya Monduli, Samwel Petro Shani (47) ya kuvunjwa mikono yake miwili kutokana na kipigo cha askari Polisi wa kituo cha Leskale.

Wanaume watatu waoana Thailand

Wanaume watatu waliofunga ndoa siku ya wapendanao (Valentine) nchini Thailand wamepata umaarufu katika mtandao baada ya picha za maandalizi ya harusi hiyo kuenea mitandaoni.

Kanye West akijibusu mwenyewe!!

Photoshop hapa imetisha, kama ulikuwa unashangaa hii imetokea wapi, original hii hapa chini.

Wednesday, February 25, 2015

PICHA: Miaka 20 pamoja na bado mapenzi motomoto

 nimezipenda nywele za Jada

BIZARRE: Wadada wazuri bila bra na gundi imeachia, boobs zimebaki nje nje

 Sehemu ya pembeni ya titi la Christina Milian imeonekana sana


Unaona hapo karibia na vifungo kuna gundi imeshikilia shati, ikitoka ndio upande wa titi unabaki wazi

Stara Thomas akana kufumaniwa na mpenzi wake

Aliyekuwa mwimbaji muziki wa gospel na baadaye kurudi kwenye bongo fleva Stara Thomas, amekana habari zilizoenea hivi karibuni kuwa amefumaniwa na mpenzi wake nyumbani kwake.

SHILOLE: Marafiki ndio chanzo cha migogoro yangu na Nuhu

MSANII wa muziki na mwigizaji wa filamu za Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, ameamua kuweka wazi chanzo cha migogoro yake na mumewe mtarajiwa, Nuh Mziwanda kuwa ni marafiki.

H. Baba: Tunazaa kwa mipango na Flora

STAA wa Bongo Fleva, Hamis Ramadhan ‘H. Baba’, ni kama amejibu maneno yaliyokuwa yakizungumzwa na mashabiki wake juu ya ujauzito wa mkewe, baada ya kudai kuwa wanazaa kwa mipango.

PICHA: Unavyoweza kupanga sanaa za ukutani

Eneo dogo artwork nyingi, ndio ladha ya mkaaji na mwenyewe anapenda, sisi hatuna cha kukataa kilichopo ni ku enjoy picha.


BIZARRE: Nguo zinaficha mengi japo huyu kavaa..

Picha inasisimua, kama vip usifungue...

Hatari za kuweka picha za mtoto mtandaoni

Nimekutana na article hii ambapo mwandishi anatahadharisha  tabia ya kuweka picha za watoto mtandaoni, ni kweli kuwa wengi tunafanya hivyo. Je, wewe unaona ni poa tu kuweka picha ama sio sawa.

Nianze kwa kukuuliza wewe mzazi; unapoweka picha ya mtoto wako kila hatua tangu akiwa mchanga hadi anaanza kutembea na kuanza shule, alikuomba au ulipata ruhusa yake?

Mama amnyanyasa mtoto wake wa kumzaa huko Mwananyamala

Mtoto wa takriban miaka miwili kutoka eneo la Msisiri Mwananyamala jijini Dar es Salaam anayedaiwa kuteswa na mama yake mzazi anapata matibabu katika hospitali ya Mwananyamala kutokana na kile kilichotajwa na muuguzi wa wodi ya watoto hospitalini hapo kuwa ni utapiamlo mkali na majeraha.

MAHUSIANO: Kumbe wivu wa kupindukia ni sababu inayoweza kufanya mahakama ikavunja ndoa

Sikuwa nafahamu hili.., 

GPL inaripoti kuwa: NDOA ya staa wa filamu nchini, Salim Mbegu ‘Slim’ na mkewe Asia Morgan imevunjwa rasmi na Mahakama ya Mwanzo ya Magomeni jijini Dar kufuatia mgogoro wa muda mrefu.

Kimenuka Iringa

*Raia wachoma magari ya polisi, wapora silaha
*Wawafungulia mahabusu, wateketeza nyaraka
*Mmoja afariki, mabomu ya machozi yatumika


Jambo leo linaripoti kuwa MAPAMBANO makali yameibuka katika Kata ya Ilula mkoani hapa, kati ya raia na polisi, hali iliyosababisha Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), kulazimika kutumia mabomu ya machozi kutuliza vurugu hizo zilizoibuka kutokana na kifo chenye utata cha mwanamke mmoja.

BIZARRE: Makalio yanapobadilika completely...

inkibinda nkoi imechenji...booty bado ni fashion

Tuesday, February 24, 2015

PICHA: Wapendanao deseni pozi hilo..


Mitandao inasema pesa ya Kriss ndio Nick aliyokuwa anamendea ndio maana sasa anaanza kulalama cashflow imekatwa..familia hizi....sijui kuna ukweli kiasi gani.

Hajafikisha hata 18 lakini yuko juuuuu! Hongera zake

Ila hii bustani mbona kame tu kama za jua la bongo...
Kylie Jenner is 17. She's buying a $2.7 million house.
Sources tell TMZ, Kylie has inked a deal to buy this 4,900 square foot house in The Oaks, an exclusive gated community in Calabasas.
The house -- which is a block from Kourtney and Khloe -- has a sick home theater, a pool, 5 bedrooms, an awesome kitchen, and on and on.
Kylie has made a lot of money on Keeping Up With The Kardashians.


Mwanaume jela miaka 1,535 kwa kubaka wanawake 29

Hii miaka itakuacha ucheke na maandishi..
Mahakama ya Afrika Kusini imemfunga jela miaka 1,535 mwanaume mwenye umri wa miaka 35 ambaye alibaka wanawake  katika kipindi cha miaka mitano, vyombo vya habari viliripoti jana.

Mwanamke mbaroni akiuza binadamu

Ya walimwengu ngumu kuyaelewa..
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma linamshikilia mwanamke mmoja, Sophia
Chambo (30), mkazi wa Mtaa wa Polisi, Kata ya Lizaboni Manispaaya Songea, akituhumiwa kujihusisha na biashara ya kuuza binadamu kwa wafanyabiashara kwa ajili ya zindiko.

KUTOKA KWANGU: Aina ya taa za chumbani

OK, hiyo picha nzuri hapo juu ni mfano wa taa za bedroom. Ndani ya bedroom unahitaji mchanganyiko wa taa kwa ajili ya kufanikisha kila unalofanya ukiwa chumbani. Kwa ajili kama tujuavyo sio kuwa ukiwa bedroom umefumba macho tu, kuna wakati unasoma kitabu au gazeti, kuna wakati unaangali muvi na kadhalika.

BIZARRE: Kama dada kama mdogo wake..


PICHA: Unapoamua mandhari ya nyumba yako iwe ni maua maua inakuwa kama hivi

Ujue unapokuwa na kwako unaamua kuweje kwa taste yako mwenyewe. Kuna mwingine anasema, mimi ni mwendo wa zebra, mwingine labda maroon na hapa ni endapo utaamua mauamaua. Kwahivyo ni mwendo wa floral kila mahali, pazia, sofa nk. Tazama picha:
viti, cushion vyote maua


fremu za ukutani nazo picha za maua
vyombo maua


table mats maua

comforter maua