Thursday, October 30, 2014

My article for newspaper: Kupamba ndani nafuu na haraka

Njia za gharama nafuu na haraka za kubadilisha muonekano wa ndani ya nyumba yako.


Watu wengi wanafikiria kuwa kupamba ndani ya nyumba ni jambo kubwa na ambalo linahitaji hela nyingi. Lakini hii sio kweli, mtu anaweza kutafiti njia za kupamba nyumba kwenye mitandao au majarida ya mapambo ya nyumbani  na kuona ni njia zipi zinazoweza kumfaa kwa gharama aliyo nayo. Makala hii ni mojawapo ya vyanzo vitakavyokupa mawazo ya njia rahisi na za haraka zaidi za kupamba ndani ya nyumba yako kwa namna maridadi kabisa.

Kabati la mapambo ni njia mojawapo ya gharama nafuu na ya haraka ya kupamba ndani ya nyumba. Kabati hili unaweza kulitengenezersha kwa fundi kwa mtindo unaotaka wewe mwenyewe iwe ni kwa sehemu kubwa kuwa ni kioo kitupu au mchanganyiko wa mbao nusu na kioo nusu. Linaweza kuwekwa sehemu ya kona ya chumba.
Linapokuja swala la mapambo ya kabati la mapambo, eneo la ndani ndio la kujali zaidi. Pamoja na mtindo wa kabati husika vioo pamoja na taa ya ndani ya kabati vinamaliza kila kitu! Mapambo ya aina mbalimbali huwekwa ndani ya kabati hili na kuleta muonekano wa kuvutia. Na pia wengine hupendelea kuweka glass za kifahari za mvinyo za aina ya crystal na hii inalipendezesha mno kabati kwa kweli. Tunu sio kitu ambacho umenunua karibuni kwa hela nyingi. Ni kitu ambacho kina thamani kwako zaidi ya pesa inavyoweza kununua. Inaweza kuwa ni sanaa uliyopewa toka kwa bibi na imepitia vizazi kadha wa kadha hadi kukufikia wewe au inawezekana ni kitu kilichokuwa sehemu ya maisha yako ya utotoni au kitu maalum ulichopewa na mtu maalum. Ukizungusha macho yako kukitazama kinakupa burudiko la nafsi.

Ndani ya kabati la mapambo waweza weka pia mdoli wako ambao unadhani ni wa kipekee na unafaa kuwepo hapo. Pia waweza weka vitu mbalimbali kutoka sehemu tofauti za dunia. Zingatia kua huna haja ya kusongamani kila sanaa uliyonayo kwenye kabati lako la mapambo. Hakikisha unaacha nafasi kati ya kitu na kitu ili isilete muonekano wa mrundikano. Chochote ambacho unadhani kitafanya kabati lako lipendeze waweza weka humo.

Njia nyingine ya kupamba ndani kwa gharama nafuu na kwa haraka ni kwa kutumia maua ya kutenengeneza (maua mfu). Maua na mimea inafanya muonekano wa mahali uwe wa kuvutia. Mtu anaweza kuweka mimea na maua kadhaa ya kutengeneza katika sehemu tofauti tofauti za nyumba yake. Staili na rangi ya maua na mimea hii iendane na rangi ya chumba cha nyumba. Maua hayo yanaweza kuwekwa sakafuni au juu ya meza vilevile.

Mtu anaweza kutumia vibebeo vya mishumaa kupambia nyumba yake na ikaonekana maridadi. Unaweza kutafuta aina mbalimbali ya vibebeo hivi kwenye maduka ya mapambo ya ndani na unaweza kuchagua vya mbao au vya kioo.

Mito ni njia nyingine ya kupamba kwa gharama nafuu na kwa haraka. Unajisikia burudani ukiwa na mito ya staili na maumbo mbalimbali. Unaweza kutupia mito kadhaa ya  mapambo kwenye seti zako za sofa ambapo zitaleta matokeo makubwa na itakuwa vyema zaidi kama ukitumia mito ya rangi nyekundu na ya chungwa.

Badilisha muonekano wa madirisha kwa kubadilisha pazia na fimbo. Hii sio usumbufu kama ambavyo unaweza kufikiri kwani kuna maduka mengi yanayouza pazia ambazo zimeshonwa tayari. Na kwa swala la fimbo zake kwa ajili tayari kuna vishikizo vilivyotobolewa,  ni kiasi tu cha kuondoa fimbo ya mtindo mmoja na kupachika nyingine ya mtindo tofauti bila ya kutoboa ukuta tena.

Hizo ni njia za gharama nafuu na haraka zaidi za kupamba nyumba yako. Jaribu mojawapo na utarudi kunishukuru. 


Makala hii imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ni mjasiriamali  upande wa usafi wa nguo, mazulia na magari; pia ana mapenzi makubwa ya muonekano wa nyumba. Kwa maoni au maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com

Wednesday, October 22, 2014

...the Big Man is taking care of us...


yani huu mchakamchaka unanifanya nashindwa hata kuwa na muda wa ku post. napata ukakasi nikiona watu 100 hadi 200 wamenitembelea lakini sijaweka post mpya, najua kuwa siwezi kuwa na close friends 100 na kuendelea hivyo wote hawa ni watu wangu ambao mngependa kuona na kusoma chochote toka kwangu...hata hivyo msijali wapendwa..soon nitafanya mambo..echuuuuuuuu...

Monday, October 13, 2014

---vitu vizuri---Je, unatumia hii unaponyoosha nguo zako?

spray starch inakuwezesha kunyoosha nguo zako kirahisi zaidi, kwani inaondoa mikunjo iliyokomaa, inafanya nguo zisitepete, inazipa harufu nzuri na kuzifanya zionekane mpya kila wakati. Utakapoanza kuitumia kumbuka kurudi kunishukuru...auchiiiii


Sunday, October 12, 2014

...my gifts from the Big Man...

...tumeshakula dinner, tumeshavaa pajama...tunamshukuru Mungu atupe usingizi mwororo...

Thursday, October 9, 2014

my article for newspaper: umuhimu wa kuondoa mrundikano


Majira haya ya kipupwe upepo ni mwingi na kazi ya usafi inaongezeka kwa ajili takataka nyingi kwa mfano majani makavu na vumbi zinapeperuswa kila mahali na wengi wanaofanya usafi hasa wa nje ya nyumba wanalalamika kuwa mazingira yanachafuka muda mchache tu baada ya kusafisha. Wengi wetu wanaliona hili na huku jua likiwa kali. Haijalishi unajali mazingira kiasi gani bali kuwa eneo ambalo limesafishwa vizuri kunakupa hisia za ukaribisho na kuhuisha nafsi na ni muonekano chanya kwako. Kuwa mazingira safi kunaongeza nguvu chanya kwenye mwili na mazingira yako. Ukiweza kudumisha usafi kwa kipupwe hiki basi utakuwa umeweza kutengeneza nguvu hii.

Lengo ni kuishi burudani na mazingira yako, ili nguvu iliyopo kwenye mazingira hayo ifanye kazi upande wako kuliko kinyume chako. Kwa jinsi tunavyoguswa na mazingira yetu ndivyo pia tunavyoakisi maeneo haya.Wengi wetu tulishaingia ndani ya jengo au chumba na mara hiyohiyo tukajihisi kuchefukwa. Kinyume na hapo, vilevile wengi tulishaingia maeneo na kutufanya kujisikia burudiko na utulivu wa nafsi. Kuwa katika eneo safi na tulivu kunaleta uwiano na starehe ndani ya mazingira hayo.

Katika mazirngira kitu nambari moja kinachozuia utengenezwaji wa nguvu chanya ni mrundikano. Mrundikano unaweza kutufanya kujisikia kuelemewa, msongo, kuchanganyikiwa na kukwama. Mrundikano ni pamoja na kitu chochote ambacho hakipendwi tena au hakitumiki, hakiko kwenye mpangilio, vitu vingi mno kwenye eneo dogo, ujazo na ujazo, miradi ambayo haijakamilika, kila kitu kilichopo kwenye hali ya kuvugu na/au kila kitu kichafu.

Tembea kuzunguka nyumba yako – nje na ndani. Fungua milango ya makabati, angalia kila mahali. Je una mlima wa makorokoro nyuma ya nyumba yako?  Kwa sababu tu huuoni mrundikano huu kila siku, haimaanishi hauko pale! Vitu vinavyokuzunguka vinakusemea ulivyo iwe vinaonekana au havionekani. Kuepuka kuelemewa wakati ukiwa unajaribu kuondoa mrundikano ni vyema kufanya zoezi hilo hatua kwa hatua. Hatua ya kwanza ni kuigawa kazi kwenye mafungu madogo dogo. Chagua kabati moja au shelfu kama hatua yako ya kuanzia. Jipongeze pale unapomaliza. Halafu nenda eneo linalofuata.Unaweza ukawa na muda maalum wa kushughulikia eneo moja kwa siku. Jambo la muhimu ni kuwa weka mikakati ya kazi ambayo itawezekana. Kama ukisubiri muda wa kutosha kufanya kazi yote pamoja, hautakaa upatikane – na hicho ni kisingizio cha kutokuanza kabisa.

Wakati ukianza kazi yoyote ya kuondoa mrundikano, panga kuchambua vitu hapo hapo ulipo. Kusanya (au weka kwenye maboksi) vitu vya kundi moja; kwa mfano, vitu vya kutupa, vitu vya kupeleka stoo, vitu vya kugawa, vitu vya kuuza, vya kuweka masijala na kadhalika. Ukishakuwa umechambua, sasa ni wakati wa kupeleka kila kimoja kunakohusika (vya kuuza unaweza kuhifadhi stoo kwa muda!). Sasa tafuta makao ya vile unavyohitaji. Huenda ni wakati wa kununua mifuko au vikontena kwa ajili ya vitu hivyo. Ndiyo njia pekee kwamba ni vyema kununua vikontena baada ya kujua ni nini unataka kuweka ndani. Baadhi ya watu wanafanya makosa kwa kununua kontena kabla ya kuchambua vitu na  hii inafanya visiwe na ukubwa sahihi au pia navyo kuwa mrundikano vilevile.

Je, unakuwa na wakati mgumu wa kuachilia vitu? Unahifadhi vitu kwa labda “lolote litatokea”? Je, unahifadhi zawadi ambazo hujawahi kutumia kwa sababu hutaki kuwavunja moyo waliokupa? Je, unajisikia vibaya usipozungukwa na vitu vingi? Je, unahifadhi nguo ambazo hazikutoshi kwa miaka 10 kwa wazo kwamba utazivaa tena baada ya kupungua kilo 7? Je, umehifadhi vitabu vya hadithi ambazo huzikusisimui tena? Utakapojibu maswali haya kwa uaminifu utaanza kufahamu ni wapi mrundikano ndani ya makazi yako unapotokea.

Kuachilia vitu ambavyo hatuvitumii tena, hatuvihitaji wala hatuvipendi ni hatua muhimu ya kuondoa mrundikano na kuanza kusafisha. Inaweza kuwa ngumu sana kwa baadhi. Kama unahitaji msaada kwenye huo mchakato, shika kifaa ambacho kwa namna yoyote ile hakikusaidii tena, kiambie asante kwa namna ambayo wakati fulani kilikusaidia kwenye maisha yako, na baada ya hapo kiachilie. Kumbuka kua kuachilia vya zamani kunaleta nafasi ya vipya. Inaonyesha imani ya yatarajiwayo.
Kuna wengi wanaoweza kufaidika na usivyohitaji. Je ni vyema kushikilia kitu ambacho hutakaa ukitumie lakini unakiweka kwa kuwa nyanya yako alikupa miaka 15 iliyopita ,au ni busara kumpa mtu ambaye atakitumia na kukithamini? Kwa kuachilia vitu kwenda kunakohitajika, unaondoa mrundikano na unajisikia vizuri kwenye jambo hilo.

Kipupwe ni msimu mzuri wa kuondoa mrundikano. Kwa jinsi unavyyoondoa mrundikano kwenye mazingira yako ndivyo unavyotengeneza nguvu chanya kukuzunguka. Badilisha maisha yako kwa kuondoa mrundikano!

Makala hii imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com

living heaven on earth..

kuna baadhi ya binadamu wenzetu kweli wanaishi....hebu cheki nyumba hii mpya ya actor Mark Wahlberg......ina ukubwa wa square foot elfu 30. Mark haishi peke yake ana mke na watoto wanne, kwahivyo kwa mahesabu ya haraka haraka kila mwana Wahlberg anamiliki square foot elfu tano...hapo bado uwanja eneo la nje ya nyumba.....je mdau, wewe pia ungependa kuwa tajiri ??



Tuesday, October 7, 2014

hawa wadudu hawa...watu na tamaduni zao na mapenzi yao kwakweli..

yani nisivyopenda kumfuga huyu mdudu hata nje sembuse kumweka ndani ya nyumba..jamani..haya maisha kweli kipenda roho.. poop yake kama ya binadamu..si unajua misosi yake ni kama ya mtu... ni ile ile. bottom line ni kuwa anayetaka kumfuga na awe tayari kufagia poop.
ukute imechanganyika na minyoo sasa...waweza taapika yani.

halafu sasa, wakianza kubweka usiku kucha wakiungana na wa huko nje ya fensi hata hakulaliki...hapo ni kabla hawajaleta viroboto...lahaula! niwe tu na ulinzi wa aina nyingine lakini sio huyu mdudu.
 ndani ya dabodeka mdudu katulia na kitabu chake pembeni
 madai eti anajenga bond na mwenye nyumba
mdudu anatumia mto kiubwete kabisa

Monday, October 6, 2014

--nitavukaje--kutoka muajiriwa kwenye NGO hadi ufugaji

Bw. Peter ana masters ya kilimo toka SUA, nimechat naye mawili matatu kuhusu kuvuka kwake toka kuwa mwajiriwa hadi kujiajiri. Ananiambia alikuwa ameajiriwa kwenye NGO lakini alifika mahali akajiuliza kuwa kwa nini asitumie elimu yake kujiajiri. Na hii ilitokana zaidi na rusha roho ya wafadhali ku withdraw na hivyo kutokuwa na uhakika wa ajira. Ameamua kutumia elimu yake ya kilimo kwa kufuga kuku, kwale, bata mzinga na bikini kwenye sehemu ya shamba lake la heka 2 alilonunua mpiji magohe ambapo ameligawa viwanja vinne. Kimoja ameweka makazi yake, cha pili ameweka nyumba za wapangaji, cha tatu ameweka mifugo yake (ambapo anasema kutokana na uzio anafuga free range system) na cha nne ameweka ofisi yake. Nikamuuliza kwale ni nini, akaniambia ni ndege wadogo ambao mayai yake yanatafutwa na wazazi wengi kwa ajili ya kuwapa watoto wao kuongeza grey matter ya kwenye brain, mayai hayo pia ni dawa na huwa yanaongeza hata kiwango cha CD4 kwa waathirika wa Ukimwi. Anasema yai moja la kwale ni sh 600. Anajivunia kujiajiri kwenye kilimo kwani anasema amekuwa na uhakika na kipato kwa mfano bata mzinga mmoja anamuuza hadi sh 100,000 wakati bikini ni sh 250,000.

Umehamasika na stori hii? Kaa standy kwa itakayofuata kukuwezesha  kukuvukisha au pengine kukupa wazo la biashara...

--vitu vizuri-- i cant believe it's October already!

October ndio hiyo na upepeo wake mkali, nimemtembelea rafiki yangu makongo nikakuta kaotesha apples na embe fupi kwenye nyumba yake mpya. Miche hiyo ya ameichukua SUA na ananiambia kwa mi apple inachukua miaka minne hadi mitano ndio uone tunda lake. 

Ninadhani ni vyema zaidi huyu kuotesha miche hii badala ya mti ni mti tuu kwani anafaidi vyote, muonekano wa apple nyekundu ambao ni kama maua, kivuli na tunda lenyewe..na nadhani hata ukiwa unafaidi kivuli likakudondokea kichwani halikuumizi bali ni kudaka na kuosha na kula. Heee he..nisisahau kukujuza kuwa kwenye kula apple usimenye matunda yake kwani utakosa zile fibers.
lazima umeze mate...