Monday, June 1, 2015

MWENYEKITI WA CCM ATUHUMIWA KWA KUMLEWESHA KIJANA BIA MBILI KISHA AKAMLAWITI

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Uyui, Musa Ntimizi amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumlawiti kijana mmoja (jina linahifadhiwa) mkazi wa Manispaa ya Tabora.

Mwenyekiti huyo alifikishwa mbele ya Hakimu Jocktan Rushwera na kusomewa mashtaka hayo, ikidaiwa na Wakili wa Serikali, Juma Masanja kuwa alitenda kosa hilo nyumbani kwake eneo la Bachu.

Mahakama ilielezwa kuwa mshtakiwa alimrubuni kijana huyo kwa kumnunulia bia mbili kwenye baa moja mjini Tabora kabla ya kutenda kosa hilo.

Wakili Masanja alidai kuwa baada ya kijana kulewa na kupoteza fahamu, mshtakiwa alimpeleka nyumbani kwake eneo la Bachu na kumlawiti.

Mshtakiwa alikana mashtaka na yupo nje kwa dhamana, Hakimu Ruchwera aliahirisha kesi hiyo hadi kesho itakapoanza kusikilizwa.

MWANANCHI

No comments:

Post a Comment