Wataalamu wa kichunguzi  na wanasayansi  wa
Mazingira, wameelezea kuwa  visiwa vilivyopo ndani ya bahari ya
Hindi  vinatarajiwa kutoweka duniani kutokana na mabadiriko ya tabia nchi
inayoikumba dunia kwa sasa ikiwemo upungufu wa kimo cha bahari, ukame na hali
ya joto sehemu mbalimbali duniani.
Hayo yameelezwa jijini hapa katika mafunzo juu ya kuripoti
habari za mazingira na mabadiriko ya tabia nchi (Climate Change) mafunzo
yaliyoanza jana Juni 1, 201a5 ambayo ni maalum  kwa wandishi wa habari
wanaoandika katika mitandao ya kijamii blog na tovuti kutoka nchi mbalimbali za
Afrika, zikiwemo Tanzania, Rwanda, Madagasca, Kenya  na Ufaransa ambaoyo
ni ya wiki mbili ambao pia ni mkutano wa maandalizi kuelekea katika kongamano
la mazingira litakalofanyika jiji la Paris, Ufaransa, Julai  na Desemba
mwaka huu.
Akielezea hali hiyo, Mchambuzi wa mambo ya mazingira katika
ukanda wa bahari na mwandishi mwandamizi wa habari  nchini Kenya, Wanjohi
Kabukuru, alibainisha kuwa, visiwa vingi ndani ya  bahari ya Hindi ikiwemo
Mombasa, Comoro na Madagasca vimo hatarini kutoweka kabisa duniani kutokana na
tabia nchi (Climate Change).
“Utafiti mbalimbali umefanyika na kutokana na mabadiliko ya
tabia nchi  Dunia itaingia katika matatizo makubwa.  Hasa kwa 
upande wa bahari ardhi iliyo ndani yake kuja kumezwa ikiwemo visiwa vya
Zanzibar, Madaga” alieleza Kabukuru ambaye pia ni mchambuzi na mtafiti wa
masuala ya mazingira ya ukanda wa bahari anayefanya kazi zake nchini Kenya.
Kwa Tanzania tayari athari mbalimbali zimeanza kujitokeza
kutokana na tabia nchi ambapo kwa sasa mmomonyomko wa radhi  umeweza
kukumba maeneo zaidi ya 148 ambayo yanaingia maji ya chumvi huku wakulima
wakishindwa kuendelea na kilimo cha kawaida.
Mkutano huo ulioanza leo Juni Mosi, umeandaliwa na Media
Coperation CFI kutoka nchini Ufaransa ulio na lengo la kutafuta njia mbadala
juu ya kuripoti habari za mabadiliko ya tabia nchi kwa ushirikiano wa Ubalozi
wa Ufaransa Kenya  na shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), kwa
washiriki wa Tanzania,wanawakilishwa na Andrew Chale mtandao wa modewjiblog na
Dotto Kahindi  mwandishi wa habari wa kujitegemea.
 

 
No comments:
Post a Comment