Wednesday, October 9, 2013

mid week stuff

nilipata wakati mgumu (wanasema usiseme shida..ha ha haaa) wakati naanzisha bustani zangu kwa kutaka kujua ni maua/mimea ipi inafaa zaidi kwenye jua na ipi inashamiri kwenye kivuli. nilitembelea bustani mbali mbali za wauza maua na kuwadadisi ma gardener kadhaa. nikafanikiwa na kama wewe ni mmoja wapo mwenye changamoto kama yangu wakati huo wacha nikusaidie upate mawazo. tazama picha hizi hapa chini za maua yanayoshamiri kwenye jua kali kwa maana ya kwamba yanastawi na rangi zake zinakolea zaidi kwenye jua kali. ukiyaotesha kivulini tu yanadoda yanapoteza rangi rangi zake nzuri na yanageuka kuwa kijani. kijani ni kizuri ila kwa wakati huo wewe unachokuwa unataka ni rangi rangi ili kupunguza ukijani kwenye bustani yako.
hili ua nililoshika wanaliita kitenge. yapo ya aina mbili; la kijani na hili la pinki. ukiondoa hili la pinki juani ukaliotesha kivulini linageuka rangi huwezi amini lote linakuwa kijani kwahivyo linafanana na yule ndugu yake. hili la mbele yake lina majani yaliyojisokotasokota. ukiliotesha kivulini nalo mambo ni yaleyale nyekundu yote na njano inapotea
 unaona hayo majani ya njano? ukiyaweka kivulini tu yanageuka kijani


 hili ukiliotesha kivulini linakufa
hiki chekundu hiki ukikiona live utapenda. kina nyekundu nzuri mno na kinapopigwa na jua ndio kinazidi kuwaka

No comments:

Post a Comment