Yako machache sana wahi kwenye rangi hii na dark green. 0755 200023
Wednesday, May 10, 2017
Sunday, May 7, 2017
Optimals Lotion ni suluhisho kwa wenye ngozi zenye mafuta
Kuna Optimals white na Optimals seeing is believing.
Optimals white inatumika na mtu wa jinsia na wa umri wowote kwa ngozi ya uso yenye mafuta ili kuondoa mafuta usoni. Seti hii ina bidhaa 4 ambazo ni Cleanser, Face toner, Face day lotion na Face night lotion.
Cleanser ni sabuni maalum ya kusafisha uso ili kuondoa uchafu wote kwenye ngozi ya uso na vishimo vyake. Bei ni 27,000
Face Toner husaidia kusafisha ngozi ya uso kwa kuipa nafasi ya kupokea lotion. Bei ni 27,000.
Face day lotion ni kwa ajili ya kupaka ngozi wakati wa mwanga wa jua iliyojaa mafuta usoni. Bei ni 38,000
Face night lotion ni kwa ajili ya kupaka ngozi wakati wa usiku. Bei ni 38,000
Optimals seeing is believing ni kwa kuondoa weusi kuzunguka macho na vilevile kundoa makunyanzi. Bei ni 29,000
Kwa mahitaji piga 0755 200023
Saturday, May 6, 2017
Friday, May 5, 2017
Sketi na blauzi..aka Omotola Dress bei ni 35,000
Njia 7 za kupendezesha meza ya chakula
Ndani
ya nyumba kuna meza za aina nyingi kama vile meza ya kahawa, meza ya kwenye
korido, meza ndogo za pembeni mwa makochi na
pembeni mwa kitanda bila kusahau meza ya kuvalia na pia wapo baadhi
wenye meza katikati ya jiko. Kati ya meza hizi zote meza ya chakula ndio ina
changamoto kubwa katika kuipendezesha kuliko hizi nyingine. Hii ni kwasababu ya
Gauni nzuri ndefu za nguva
Iko kwenye rangi hii (maroon), bluu na nyeupe kwa size Large, XL na XXL
Bei ni 28,000. Tuko mchikichini, ukitaka unaletewa ulipo hata kwa size tofauti ujaribu. 0755 200023
Thursday, May 4, 2017
Gauni nyeupe za kwenye shughuli zipo
Wakikuambia dress code ni nyeupe usibabaike. Hii niliyovaa ni Medium, zipo pia Large na XL dukani na online. Jumla na rejareja. Bei ni 28,000
0755 200023
Wednesday, May 3, 2017
Gauni la mtoko lipo.
Gauni hili linafaa kwa ajili ya mtoko wa usiku. Liko kwenye rangi nyekundu na nyeusi Kwenye saizi Medium, Large na XL. Bei ni 38,000. Tupo online na dukani. 0755 200023
Tuesday, May 2, 2017
LOTION YA LOVE NATURE TEA TREE NI KWA AJILI YA WENYE NGOZI ZENYE MAFUTA
Love nature tea tree ni seti ambayo hutumika kwa watu wa jinsia zote. Ni maalum kwa watu wa umri wowote wenye ngozi zenye mafuta.Husaidia kuondoa chunusi na mapele. Seti hii ina bidhaa za aina tatu ambazo ni cleanser toner na lotion.
Cleanser ni sabuni maalum ya kusafishia uso, huondoa uchafu wote kwenye ngozi ya uso ambapo ni pamoja na make up. Ina ujazo wa ml 150 na hupatikana kwa 19,000
Toner husaidia kusafisha vitundu vya ngozi ya uso na kuifanya kuwa tayari kupokea lotion.. Ina ujazo wa ml 150 na inapatikana kwa 19,000
Lotion hutumika kutibu ngozi iliyoshambuliwa na mapele na chunusi na pia kusaidia kuondoa mafuta usoni, Ujazo wake ni ml 50 na inapatikana kwa 19,000.
Endapo unasumbuliwa na ngozi yenye mafuta bidhaa hizi ni kwa ajili yako. Tuwasiliane kwa 0755 200023 na inawezekana kuletewa au kutumiwa hadi ulipo.
Karibu
Monday, May 1, 2017
Uzoefu wangu wa safari ya kutembelea Saadani National Park
Habarini wapenzi,
Bila shaka wapo wengi wanaotaka kutembelea vivutio nchini mwetu lakini hawajui waanzie wapi au japo hawapati mwongozo kutoka kwa waliokwisha tembelea maeneo hayo.
Hivyo basi nimeamua kuwashirikisha japo kwa uchache juu ya safari yangu ya siku 3 kutembelea hifadhi ya Taifa ya Saadani.
Kutokana na uwepo wa sikukuu ya mei mosi ambayo ingefanya mapumzikoni ya mwisho wa wiki kuwa marefu, kama kawaida yangu nilifikiria kitu cha kufanya wakati wa mapumziko hayo.
Nikaamua nataka kwenda na kuona ambapo sijawahi kwenda. Kwanza kabisa nilitafuta watu ambao wana organise safari kama hizi. Nilipowapata nikafanikiwa kununua tiketi ambayo ilijumuisha usafiri, malazi, chakula na kiingilio cha mbugani. Nikawa mmoja wa wateja na huku kukiwa pia na wateja wengine ambao wote tulisafiri pamoja. Kumbuka kuwa unaposafiri kwenye kundi ni gharama nafuu kuliko kusafiri mmoja mmoja.
Safari ilianzia Dar, Afrika Sana ambapo waandaaji walifanya kazi nzuri na mipangilio mizuri na tukaanza safari saa kumi juu ya alama.
Kuna njia mbili za kuweza kufika Saadani, ya Bagamoyo na ya Wami. Kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha njia ya Bagamoyo haikufaa hivyo tukapita ya Wami.
Kutoka barabara kuu ile ya lami pale Wami hadi Saadani kwa mwendo wa kasi ni masaa mawili.
Kwenye saa mbili kasoro tukaingia Saadani. Tukakaribishwa vyema kwa chakula cha usiku na malazi. Malazi yanaweza kuwa kwenye lodge, rest house au tents kuendana na hela yako/waandaaji.
Endapo utataka kwenda huna haja ya kubeba shuka kwani taulo na malazi yapo, kwa bafuni utatakiwa kubeba mswaki na dawa ya meno, chanuo na vipodozi vyako tu. Pia wakati wa dinner na tukapewa muongozo kesho yake.
Tukaambiwa kuwa kwa vile kipindi hiki ni cha mvua (kwa profession yao wanaita low season) wanyama wana kawaida ya kujificha kwahivyo by saa moja asubuh tunatakiwa tuwe tumeshaingia porini ndipo turudi kwenye saa nne kwa ajili ya kifungua kinywa. Hii ya mapema hivi ni ili kuwahi wanyama kabla hawajajificha.
Tukaenda porini tukafanikiwa kuwaona baadhi ya wanyama kama vile twiga, nguruwe pori, ndege mbalimbali na nyumbu. Baada ya hapo tukarejea restaurant ambapo ilikuwa ni wakati wa chai na baada ya chai tukaanza utalii wa beach.
Tafadhali fahamu kuwa hii ni mbuga pekee Afrika ambayo inaunganika na bahari. Kama ni mpenzi wa kuogelea utakapoitembelea kumbuka kubeba swimming costume.
Hakika niliifurahia sana beach kwa michezo mbalimbali pamoja na wenzangu, kuogelea pamoja na kwamba mvua zilikuwa zinaendelea kunyesha.
Baada ya dinner na some drinks na socializing tukaenda kujipumzisha hadi kesho yake ambapo tuliamkia supu ya mbuzi na capati. Kwa misosi waandaaji nisiwe na hiyana walijiaanda vyema sana. Baada ya supu hii na chai tukarudi vyumbani kwenda kupaki kwa ajili ya safari ya kurudi.
Kwenye saa sita mchana tukaanza safari ya kurejea Dar na hapo ukawa ndio mwisho wa safari yangu.
Ndio hivyo wapenzi! Ukiwa na swali kuhusu safari hii au unataka kununua kati ya viwalo kama nilivyovaa unaweza nicheki kwenye 0755 200023. Asante kwa kusoma!
Sunday, April 30, 2017
Blauzi za shifoni na za kiutamaduni zipo
25,000
Top hizi za culture ni free size
22,000
Blauzi za shifoni zenye vifungo mbele hadi kifuani zipo size Medium, Large na XL.
Zinapatikana kwa jumla na rejareja kwako wewe unayetaka kuvaa au wewe unayetaka kwenda kuuza.
0755 200023
Friday, April 28, 2017
Blauzi za shifoni zipo
Top hii ya shifoni ina kitabaa kingine cha ndani (lining) cha shifoni pia. Kwa wadada wanaojipenda kwa ajili ya kuvalia jeans,tight na sketi za kuendea kazini.
Kwa saizi na bei click kwenye vinavyozwa. jumla na rejareja zipo za kutosha
0755 200023
Kwa saizi na bei click kwenye vinavyozwa. jumla na rejareja zipo za kutosha
0755 200023
Haya magauni mawili ndiyo yaliyouzika zaidi
Haya magauni mawili ndio best seller so far. Yapo hadi XXL, zawadi sahihi kwa mother's day
0755 200023
0755 200023
Thursday, April 27, 2017
Wednesday, April 26, 2017
Gauni hili linafaa kanisani au harusini
Gauni hili naliita ni la mdada wa heshima anayeenda sehemu aheshimike kutokana na muonekano wake. Linafaa kuvaliwa kanisani, harusini na kadhalika. Kitambaa chake ni cha lace iliyojishikilia humohumo. Yaani haina vitambaa viwili. Kulinunua bonyeza kwenye vinavyouzwa. Simu 0755 200023
Friday, April 21, 2017
Namna ya kuchagua mtindo wa wallpaper
Tunaweza kusema
kuwa wallpaper ndio habari ya mjini kwa sasa kwa ajili ya kupendezesha vyumbani
kwenye nyumba nyingi za kisasa hasa sebule. Tatizo lililopo ni changamoto ya
mtindo upi ndio sahih kutokana na
uwepo wa wallpaper za rangi na michoro mingi mno. Hadi zile flati yaani zisizo
na mchoro wowote.
Elimika na dondoo
hizi za namna mnunuzi anayetaka kupamba kwa
Wednesday, April 5, 2017
Maandalizi ya ukuta kabla ya kubandika wallpaper
Wanasema
kila safari moja kubwa inaanza na hatua moja ndogo. Na hata katika swala la
kubandika karatasi za kupendezesha kuta zijulikanazo kama wallpaper, hatua ya
mwanzo ndio yenye umuhimu mkubwa. Wallpaper hazishiki au kudumu kwenye kuta
zenye mafuta, chafu au rangi inayobanduka. Na ndio maana siwezi kuchoka
kusisitiza ni kwa kiasi gani ni muhimu kuandaa kuta vyema kwa ajili ya ubandikaji
wa wallpaper.
Kwa kuta
zilizopakwa rangi zamani
Hizi
ni zile kuta za zamani, yaani nyumba ambazo zilishapakwa rangi kitambo na
tayari watu wanaishi.
Endapo
lengo ni kubandika wallpaper kwenye kuta za aina hii hazitakiwi kuwa na rangi
zilizobanduka na wala maeneo yenye vinundunundu, nyufa au vishimo. Endapo maeneno
hayo yapo inabidi kuyaondoa kwa kukwangua na kurekebisha kwa kufuata hatua kama
zile za uandaaji kuta wakati unapotaka kupaka rangi ila unaishia kwenye hatua ya
primer ambayo huwa ni ya mwisho kabla ya kuanza kupaka rangi yenyewe. Kwa maana
hiyo panatakiwa pawe nyororo kabisa. Baada ya hapo ukuta wote usafishwe kwa
sponji au kitambaa kilicholoa ili kuondoa vumbi. Mara ukuta huu unapokuwa
umekauka ndipo ubandikaji wa wallpaper unapoweza kuchukua hatua.
Kwa kuta zenye
wallpaper ya zamani
Kuta
nyingi ni rahisi kufanyiwa maandalizi kuliko ambazo zilikuwa na wallpaper
tayari na unataka kuibandua ili kubandika mpya. Kwanza kabisa ni vyema ufahamu
kuwa ni lazima uondoe kwanza ile ya zamani. Mafundi wengi wanaobandika
wallpaper wanajua pia jinsi ya kubandua.
Kuta zenye ukungu
Ukungu unaweza kuonekana kwenye kuta
kwa rangi ya njano, kijani, kijivu au nyeusi. Kama hali hii ipo kwenye ukuta
unaotaka kubandikwa wallpaper paoshe kwanza kwa maji ya moto yenye blichi.
Paache pakauke kabisa halafu papake primer kabla ya kubandika wallpaper.
Pakishabandikwa wallpaper ukungu hauwezi kuota tena kwani wallpaper zilivyotengenezwa
haziruhusu ukungu kuota juu yake.
Kuta mpya
Endapo kuta/nyumba ni mpya na
umefikia kwenye hatua ya kupaka primer (kama tulivyosema huko juu katika
maandaliza ya kupaka kuta rangi) unachotakiwa ni kuepuka gharama mara mbili za
kupaka ukuta rangi ya mwisho halafu wakati huohuo unataka tena kubandika
wallpaper juu yake. Badala yake
unachotakiwa ni kuishia kwenye ngazi ya primer tu kwenye ukuta wowote unaotaka
kubandika wallpaper halafu badala ya ngazi inafuata ambayo ni ya mwisho yaani kupaka
rangi ndipo unabandika wallpaper.
Natumai msomaji
wangu umeelewa vizuri kabisa namna ya kuandaa kuta za aina mbalimbali endapo
unataka kuzibandika wallpaper.
Tunazo wallpaper za michoro zaidi ya 100. Wasiliana
nasi kwa namba 0755 200023
VITANDA, MEZA YA CHAKULA NA KABATI LA VYOMBO VIPO
Kitanda 6 kwa 6 bei ni 1.3m
Meza ya chakula ya watu 6 bei 1.3m
Kabati la vyombo very classy 1.2m
Kitanda 5 kwa 6 bei ni 1.2m
Mawasiliano kwa biashara tu ni
0755 200023
Subscribe to:
Posts (Atom)

















































