Thursday, January 23, 2014

buriani Mhe. Bwa'mdogo; tuta miss biashara uliyokuwa unatupa

jana nilishtushwa kujua kuwa Marehemu Mheshimiwa Saidi Bwanamdogo kumbe ni aliyekuwa mteja wangu wa kufua nguo. toka nianze kufanya DC & Laundry sijawahi kupata biashara kubwa kwa wakati mmoja kama nilivyokuwa napata kwa Mheshimiwa Bwa'mdogo, kiasi kikubwa kabisa cha nguo alichowahi kuniletea ni kanzu 500. kwa mara ya kwanza alipokuja ofsini kwangu kama mteja nilimuuliza jina la kwenye risiti niandike nani? akaniambia Bwa'mdogo, nikadhania kama ananitania kwa ajili hata muonekano wake alioneekana mdogo mdogo nikadhani ndio maana kajiita hivyo; ila baada ya kifo chake jana nilipoona picha du! ndio nikajua kuwa lilikuwa jina lake rasmi. sikuwahi hata kufahamu kuwa alikuwa mbunge tena wa Chalinze. buriani Bwa'mdogo..you will be missed! 
Ian DC & Laundry

No comments:

Post a Comment