Thursday, November 1, 2012

My article for newspaper: Muonekano wa jiko



Muonekano wa Jiko

Jikoni huenda ni mahali ambapo panadharaulika sana kwenye nyumba za watu wengi; wanafikiria jiko kama ni mahali au chumba cha kupikia chakula tu kwa hiyo mapambo mahali hapo hayahusu. Hawawezi wakawa wanakosea zaidi ya kufikiria hivi; jiko linaweza kuwa mahali pazuri kuliko pote katika nyumba unayoishi kama una staili na unajua jinsi ya kupamba.

Jikoni ni moja ya sehemu muhimu sana kwenye nyumba yako. Ni sehemu ambayo pia inatembelewa mara nyingi zaidi kwa siku kuliko sehemu nyingine yoyote hapo nyumbani. Unatakikana kwenda jikoni mara kadhaa kwa siku, kuandaa chakula au hata kuchukua glasi ya maji baridi. Hutataka kuona jiko lako likiwa limejaa uchafu mavumbi na mafuta. Zaidi ya yote jiko linatakiwa kupambwa na kuonekana maridhawa na linalohuisha nafsi.

Chumba cha jiko la kawaida la kisasa kinakuwa na vitu kama jiko, sinki la maji moto na baridi, jokufu, makabati, kipasha chakula na vifaa vingine vya umeme. Yapo majiko makubwa kwa wenzetu wa magharibi ambapo kwao zaidi ya chumba cha jiko kuwa ni mahali pa kuandaa chakula pia ni mahali pa kufulia, kulia chakula na stoo ya kuhifadhia vyakula. Kubuni jiko la kukidhi mahitaji yako iwe ni kwa nyumba mpya au kubadilisha muonekano wa jiko la zamani inabidi kutembea na kutafiti kwa kuangalia aina mbalimbali za majiko ambayo tayari walau yanakidhi mahitaji ya jiko la kawaida ndipo nawe ukaweza kujiamulia la kwako. Kuna wataalamu ambao wanaweza kubadili jiko lako na kuwa la kisasa kuendana na mahitaji yako.

Chumba cha jiko kinahitaji vyombo ambavyo ni vya kawaida kwa walau kila mtu au familia. Sasa unamsaidiaje mtu ambaye anaanza maisha na anahitaji jiko. Lengo la makala hii ni kuongelea muonekano wa jiko la kisasa la kawaida kabisa sio hayo yenye sehemu ya kulia hapo hapo na sehemu ya kufulia.
Ingawa kuna aina mbalimbali za majiko kwa kila kaya, bado unaweza kujaribu kitu kipya na cha kisasa kwa ajili ya sehemu hiyo ambayo inatembelewa kuliko zote katika nyumba yako. Jiko lako ni mahali panapotakiwa kuwa na mvuto na pia kufanyia kazi kwa uhuru kwa kuwa na vifaa vinavyohitajika.
Vyombo kama sahani, vijiko, glasi na vikombe vinategemea zaidi ladha ya mtu binafsi hivyo sitaviongelea hapa. Vitu vifuatavyo vitafanya jiko lako liwe nadhifu:
  • Makabati
Aina ya makabati utakayochagua na mpangilio wake unatoa picha kubwa ya jiko kwani makabati yanachukua nafasi kubwa zaidi katika chumba cha jiko. Unaweza kuchagua makabati ya mbao hadi ya chuma ila ya mbao yanapendeza na yanadumu kuliko yote. Ya chuma yamekaa kiviwandani zaidi sio kwa ajili ya nyumba za kuishi. Kama una vyombo ambavyo ungependa vionekane basi weka makabati ya mbao ila yenye milango weka vioo. Vitasa na  mikono ya makabati na madroo na hata bomba la sinki visiwe vya urembo mwingi ila tu hakikisha ni imara na vina usalama kwa mfano visiwe na ncha za kumkwaruza mtumiaji. Vitu vyenye urembo mwingi vinaharibu muonekano wa jiko.

  • Sakafu
Jikoni kunatumika na kila mwanafamilia hivyo inatakiwa kuwa na sakafu ambayo ni imara na isiyoharibika kirahisi. Kama una watoto wadogo basi ni vyema kuwa na sakafu isiyoteleza, ambayo pia ni rahisi kusafisha kwa ajili watoto wana tabia ya kuokota vitu chini na kuweka mdomoni. Haishauriwi kuweka zulia jikoni kwa kuwa kuna mafuta na majimaji yanawagika chini wakati wa kupika na kusafisha vyombo na jiko lenyewe.
  • Hifadhi
Kama unahitaji sehemu ya ziada ya kuhifadhia zaidi ya makabati basi unaweza kuweka vitundikio vya masufuria au viraki kwenye kona ambayo unaweza kuweka vitu vidogovidogo.
  • Mwanga
Jiko linahitajika mwanga mwingi kwa kuwa shughuli nyingi na vifaa vingi vinatumika hapo kwa ajili ya kuandaa vyakula. Pia dirisha la kupitishia mwanga na hewa liwe kubwa kwa kuwa joto jingi linazalishwa jikoni na kwa mfano hapa kwetu watu hawana mazoea pia ni wachache sana waa uwezo kifedha wa kuweka kiyoyozi jikoni. Feni ya jiko kwa ajili ya kunyonya mvuke ikiwepo itakua vyema.
Mapambo ya jikoni sio kama ya chumba kingine kwa mfano chumba cha kulala au sebule, jiko linaweza kupambwa kipekee bila kuhusisha muonekano wa vyumba vingine. Nyumba yako bado itakuwa inavutia hata kama jiko limepambwa tofauti kabisa na vyumba vyote. Yote kwa yote, muonekano wa jiko lako unaweza ukavutia zaidi ya unavyofikiri kama una ladha ya staili na mitindo  basi unaweza kufanya jiko lako likawa ni sehemu kila mwanafamila anapenda kutembelea na pia kurahisisha kazi ya mpishi. Muhimu zaidi ya yote jikoni napo papambwe kama ilivyo vyumba vingine ndani ya nyumba yako.
Makala hii imeandaliwa na Vivi O. Machange. Kwa maoni niandikie viviobed@yahoo.co.uk au simu 0755 2000 23

Monday, October 29, 2012

Wednesday, October 24, 2012

My article for newspaper: Unatokea ofsini kwenda kimnuso



Jinsi ya kuvaa ukiwa unatokea ofsini kwenda kwenye kimnuso

Ni saa kumi na moja jioni lakini sio muda wa kwenda nyumbani. Badala yake, kuna kimnuso na wanawake wengi walivyo ni tukio ambalo linaweza kukuacha ukihangaika juu ya nini huku duniani cha kuvaa kazini siku hiyo ili uunganishe na mtoko wako huo wa usiku.

Mbaya zaidi ni kuwa huna muda wa kwenda nyumbani kubadili ni lazima utokee kazini ulikokuwa umekaa mbele ya komptyuta moja kwa moja kwenye usiku wa tafrija na shampeni. Lakini kabla hujaumia kichwa zaidi, vitupio vinaweza kubadili kabisa muonekano wa vazi fulani kutoka muonekano wa kiofisi kwenda kwenye usiku wa sherehe.

Sasa ni wapi pa kuanzia? Anza siku yako kwa kuvaa sketi  fupi ya rangi yoyote na koti la rangi isiyofanana na sketi na kiblauzi ndani mwake. Usisahau mchuchumio wako kuonyesha umbile na urembo wako. Baada ya saa za kazi wakati wa kuelekea kwenye tafrija kama hutaweza kwenda nyumbani kubadili nguo unaweza kubaki na kiblauzi cha ndani ya koti na kuacha koti lako kwenye gari na beba pochi na sio ule mkoba mkubwa wa kazini.

Siri ya kuvaa nguo zile zile ila mionekano tofauti kutoka mchana kuingia usiku ni mpangilio wa  nguo na vitupio vyako. Changanya mavazi yako na vitupio kuendana na shughuli ya wakati husika ili mavazi yale yale yawe na mionekano tofauti. Jenga taswira mbalimbali kwa mfano kiatu hichi hicho ila na pochi tofauti tofauti inaonekanaje. Taswira ni msingi wa mafanikio yako.

Hereni zina nguvu kubwa ya kubadili muonekano wa mavazi ya kiofisi kwenda kwenye mg’ao wa muonekano wa usiku. Kama huwa huvai hereni kazini au unavaa vile vidogo sana basi usiku ni wakati wa kuvaa hereni kubwa zinazong’aa ambazo huwa zinabadilisha hata mavazi rahisi kabisa. Jaza shingo yako na mkufu au hata mtandio wenye rangi za kuwaka utabadili muonekano wa ofsini kuwa wa sherehe. Hii itasaidia kuleta mwanga na rangi usoni mwako na hivyo kubadili muonekano wako mzima. Kuendana na mtindo uliopo kuna wakati vidani, mikufu au shanga zinavaliwa zaidi ya mmoja na unaweza basi ukaongeza na bangili.

Pete kubwa yenye jiwe kubwa kati  iliyovaliwa kwenye kidole chochote inabadilisha muonekano wa kiofisi kuwa wa kisherehe zaidi. Pete hii moja tu inatosha usivae zaidi. Hakuna kitu kinachoonyesha unaelekea kazini kama mkoba wako. Mkoba unaweza kuharibu kabisa muonekano wako wa vazi la sherehe. Kwanye sherehe beba pochi (ile ndogo ambayo mara nyingi si ya kutundika) na weka vile vitu muhimu sana ambavyo ni lazma unavihitaji popote uwapo kama vile leseni ya udreva, pesa taslimu kidogo, kadi ya ATM, simu na funguo. Wakati wa kutoka kuelekea kwenye mnuso unaweza kufungia mkoba wako kwenye droo la ofsini na kuuchukua kesho yake. Kumbuka mkoba usiache kwenye gari kwani ni kishawishi kwa wezi wa kwenye magari.

Linapokuja swala la vipodozi, ukiwa unatokea ofsini kwenda moja kwa moja kwenye sherehe usijaribu kujipaka tena uso mzima. Badala yate tumia vichache tu kama lipstiki, ongezea mascara kidogo na kimguso cha poda kuondoa mngao kwemye uso wako na ongeza vipodozi kwenye mashavu.  Weka shedo za macho zenye rangi za silva na dhahabu. Vipodozi vya kwenye mashavu vizidi kidogo usiku kulinganisha na wakati wa kuwa ofsini.
Kwa nywele za chap chap chana ulizonazo kama ni fupi ama funga kifagio kama ni ndefu na kuongezea kibanio. Hizo hereni zako kubwa tayari zitakuwa zinashirikiana na nywele kuleta mvuto.

Mtandio ama skafu inasaidia sana kubadili muonekano wa mavazi toka siku ya kazi kwenda usiku wa kimnuso. Kwa ofsini funga kitambaa chako hicho shingoni wakati usiku  unaweza kufunga mtandio au skafu yako kiunoni kama mkanda.
Rangi zinaweza kuvalika kutokana na uamuzi wako ila nyeusi na nyeupe bado ni maarufu kwa wanawake. Vaa rangi kazini lakini zigeuze kuonyesha urembo wako nyakati za usiku.

Harufu yako ni muhimu kukamilisha muonekano wako mzima; inakupa utambulisho, wakati wa mchana tumia pafyum zenye ladha za maua ila usiku tumia pafyum yenye harufu kali zaidi kusisitiza utu wako.
Kama una mtoko utakaokugharimu kutokea ofisini moja kwa moja fuata dondoo hizi na zitakuongoza kupata muonekano wako wa kazini na usiku siku hiyo.
Makala hii imeandaliwa na Vivi O. Machange. Kwa maoni niandikie barua pepe viviobed@yahoo.co.uk au  simu 0755 2000 23.





Sunday, October 21, 2012

ni kama jana tu

ukiona kitu kizuri cha kumfaa mwanao hata kama ni hapo miaka 10 ijayo usiache kumnunulia kwa ajili siku hazigandi. utashangaa mara anakitumia. nakumbuka baba mwenye nyumba alikutana na buti nzuri za mvulana kama wa miaka 12 akamchukulia mwanae wa miaka 2 watu wakamcheka na kumshangaa sana. lakini soon huyo kijana atazitinga..

Saturday, October 20, 2012

nikumbuke kwenye ufalme wako wa kuosha gari

tunapenda usafi. hutajutia hela yako. hatuna presha wala papara tunakusafishia gari yako tukiwa tumetuliza akili...karibu Ian CAR WASH survey karibia kabisa na pub le maarufu sana BRAJEC. tuonane weekend hii...xo

Friday, October 19, 2012

ukifanya haya utakuwa kwenye mahusiano yenye afya



Njia 3 za kufanya kuwa mahusiano mazuri zaidi
Mimi sio expati wa mahusiano. Ila nimegundua kuwa japo kila mahusiano ni ya kipekee na yanatofautiana ya kati ya  mtu na mtu kuna vitu vitatu ambavyo mahusiano yoyote yakivifuata vitaboresha uhusiano wa mtu na mwenzie.  Nakualika kujua hivi vitu vitatu tu: Kuwa mkweli. Kuwa tayari kukubaliana kutokubaliana . Kuwa tayari kukimbia.

Kuwa mkweli

Kutokuwa mkweli katika mahusiano ni sumu. Ni ngumu sana kukumbuka uongo wote uliowahi sema na ni nani ulimwambia. Kudanyanywa kunaumiza, Kuna faida nyingi ukiwa mkweli kwa patna wako. Kuna uhuru unaokuwa  ndani yake na ulinzi wa kujiamaini kuwa unaambiwa ukweli daima.


Kuwa tayari kukubali kutokubaliana


Inapokuwa ulikuwa singo kwa muda, una maono fulani kichwani kwako juu ya mambo fulani kuwa ndivyo unavyotaka yawe. Mara anakuja huyu mtu ambaye umempenda lakini ana mawazo tofauti na yako kwa labda kila unachotaka. Unajikuta inabidi ulegeze msimamo wako kiasi. Na unaona ni sawa tu. Lakini vinakuja vile vitu ambavyo unajisikia kabisa lazma viwe hivi na sio vile, unatakiwa kuwa na uhakika kuwa patna wako amekubaliana na wewe. Kwa hiyo ukiweza kulegeza msimamo kidogo na kuweka wazi kwa patna wako mnaweza kuja na solution ambayo itakuwa bora zaidi na wote mkaifurahia.


Kuwa tayari kukimbia


Fuata moyo wako. Unajua wakati mambo hayaendi sawa au jambo fulani patna wako alilofanya halileti heshima kwako. Ujue nini, unatakiwa ujipe raha mwenyewe. Kama unahisi kuwa hufurahii mahusiano yako ni sawa kukimbia hata kama ni kwa muda ili utulize kichwa uamue ni nini hasa unataka. Usijali watu watasema nini: chukua maisha yako mikononi mwako. Saa nyingine kujiondoa kwenye uhusiano ni kitu chema zaidi unachoweza kufanya kwako na kwa huyo mtu mwingine.