Monday, September 23, 2013

fenicha za nje ya nyumba

fenicha za kwenye bustani kwa hapa kwetu zaweza kuwa za mbao ngumu kwa maana ya mkongo na mninga kwa vile zitaweza kupambana na shurba nyingi kama jua kali, mvua na upepo. pia zaweza kuwa za chuma ili mradi ukipake dawa ya kuzuia kutu ama zaweza kuwa za aluminium. fenicha kama hizi hapa chini japo picha ni ya mazingira ya nje ya TZ lakini nawe waweza kuwa nazo kwenye makazi yako kwani malighafi zote za kutengenezea zinapatikana hapa nyumbani. mradi kitu roho ipende..
hivi viti waweza kutengeneza kwa mbao ya mninga ama mkongo. mito inapatikana kirahisi kama kufumba macho na kufumbua. wakati mito haihitajiki toa hifadhi stoo, rangi zake za kuwaka zinasaidia kuongeza rangi na kufanya sehemu ivutie. hiki kimeza tengeneza kwa chuma na juu yake weka kioo kwa urahisi wa kusafisha na ili kidumu kama hapa alivyoweka..

No comments:

Post a Comment