Saturday, September 21, 2013

muonekano wa jiko dogo

nimefanya utafiti kutaka kujua wasomaji wanavutiwa na nini hasa kwenye blog hii. katika findings  zangu kwa kuangalia nyenzo za trafiki nimegundua kuwa wasomaji wengi wananifikia kwenye blog kutoka search engine za google na yahoo wakitaka kujua zaidi kuhusu jikoni kwa ujumla kwa maana ya makabati, mpangilio wa jiko na kadhalika. kwa hivyo ninakata kiu yao kwa ku share picha hizi chache za at least jiko dogo la kisasa linavyotakiwa kuwa na vitu vyake muhimu. enjoy!
jiko dogo lililokamilika. kila eneo limekuwa utilized. juu ya hii kaunta yenye vyombo kwa chini watu wanaweza kukaa na kula

stovu ambayo yaweza kuwa na pande 2. upande wa kutumia gesi na wa umeme. halafu mwenye jiko lake kaamua kupanga kwa kuweka microwave juu ya stovu. nadhani ni ili kutumia vyema eneo dogo alilo nalo

sehemu ya kuhifadhia viungo vya chakula. kumbuka hivi havina haja ya kuweka ndani ya friji

droo la vitambaa na vitaulo

friji la kisasa

tosta, jagi la miko, vipawa na vijiko vikubwa na vibao vikiwa juu ya kaunta


shelfu za vyombo za wazi zilizo karibu na dirisha, kwenye hizi kabati za chini yake hifadhi masufuria na vikaangio

sinki na kichujio chake cha kati. juu yake kutakuwa na bomba za maji moto na baridi. chini ya kabati zilizobeba sinki weka vifaa vyako vya usafi kama sabuni na sponji

No comments:

Post a Comment