Monday, September 23, 2013

poleni sana Wakenya: kwa jirani ni kusafi

inasikitisha ambapo mtu unaamka mzima na kujiendea zako kufanya shopping mall lakini kwa kisirani unakutana na kifo au ukilema kama ilivyotokea kwa jirani zetu Kenya kwenye westgate mall ambako kwa uchache watu 68 wameuawa na 75 kujeruhiwa. hata hivyo kwa ajili tunajifunza kila siku nimekuwa nikiangali tukio hili na kuona jinsi jirani yetu alivyo msafi kwenye jiji lake. haijalishi kuna kiongozi gani mashuhuri duniani anayemtembelea..tehe tehe teh bali ni makazi yake kila siku ndivyo anavyoishi. poleni sana Wakenya ila waTz tuna cha kuiga kutokana na unadhifu wa mazingira ya jirani. 
ona bustani zilivyo kuwa pruned vizuri, chini hamna hata sisimizi. hapa wabongo hawakawii kujitetea oh hali ya hewa ya Nairobi inaruhusu...hamna lolote siasa nyingi kuliko kazi

ona palm zilivyonawiri, ukijani unafurahisha

unaweza desa hizi grill, ukapeleka kwa mchomeleaji akakutengenezea kama hivi

kila mahali ni nadhifu! big up jirani

No comments:

Post a Comment