Saturday, September 28, 2013

hapa na pale

ni mwaka mmoja na ushee tokea niamue kuwa mjasiriamali. kuna rafiki niliyekuwa nafanya naye kazi na imefikia muda anarudi makwao hivyo akanialika jana kwenye kimnuso cha kumuaga. nilichoshangaa hadi kwenye mabaa wanacheki mabomu siku hizi kutokana a janga la westgate. pia katikati ya kimnuso wacha nyoka aanguke toka kwenye mti...



hiki kiblauzi cha huyu mrembo ni mchanganyiko wa kanga na linen. kilinivutia hadi nikawa najiuliza hiyo nyeupe imeunganishwa ama ni kanga ikoje? ikabidi nimuulize. akaniambia mwanzo kabisa kilikuwa ni linen nyeupe tupu, hakukifurahia kuwa rangi nyeupe blauzi nzima. ndipo akaamua kukikata na kuweka kanga juu. nilifarahia mno ubunifu wake!



tuwe makni tunapokuwa mahali kwenye miti, nyoka huyu alianguka toka mtini!

nikiwa na mwenyeji wangu Sabina.

No comments:

Post a Comment