Friday, July 11, 2014

housekeeping: kisulisuli kimepamba moto

kwakweli upepo wa kipupwe hiki umetisha. Kwa wanaoacha milango wazi, kwa kipindi hiki ni bora tuu kuifunga kwani mavumbi yanajaa ndani na kwa wenye miti inayododosha ukifagia ama kuokota baada ya nusu saa ni vululuvlulu kila mahali.
 mti huu inaitwa Dodoma tree, huwa ni kijani kipindi chote cha mwaka. inadondosha majani machache mno hata pamoja na kisulisuli hiki.
Dodoma tree inafaa sana kuoteshwa eneo unalotaka lifunge na unaweza kuielekeza utakavyo. Kwa mfano unaweza kuikatia urefu fulani ili isiende juu zaidi au kuicha ikawa mikubwa kabisa, yote hayo ni wewe tu na jinsi roho yako ilivyopenda. Kama uko karibia na barabara vumbi, dodoma tree inasaidia kudaka vumbi lote na pia mizizi yake huwa ni midogo sana kiasi kwamba haipasui kuta nyufa. Ukiiotesha hutajuta, inapatikana kila mahali kwenye bustani za maua ila kuwa makini usibambikiwe. Ukishafanya hivyo urudi kunishukuru kwa desa!

No comments:

Post a Comment