Thursday, September 25, 2014

--vuka--kutoka architect muajiriwa hadi kujiajiri

Vijana wetu wengi mara wanapomaliza chuo wanaanza kusaka ajira. Wengi wanashindwa kuamini kuwa wanaweza kujiajiri kwa kufanya kile ambacho tayari wameshakuwa na ujuzi nacho. Leo nimechat na Caleb ambaye ni architect, nikamuuliza ni kwa vip ameweza kujiajiri. Alichoniambia ni kuwa mara baada ya kumaliza chuo aliajiriwa kwa miaka miwili. Wakati huo alikuwa anafanya vikao na wateja wake binafsi nyakati za jioni baada ya kazi za mwajiri wake. Mambo yalivyochanganya akajiajiri. Nikamuuliza maana ya mambo kuchanganya ni nini? Akasema alipata mradi wa mwaka mmoja kwenye kazi yake hiyo ambapo alijiaminisha kuwa akijiairi wakati wa mradi huo itakuwa ni wakati muafaka kwani hata kwa miaka miwili mbele asingepata mradi, mwingine mkubwa bado angeweza ku survive kwa zile kazi ndogondogo. Anasema ana uhuru zaidi wa binafsi na kipesa alivyo sasa kuliko alivyokuwa ameajiriwa. Umepata cha kujifunza hapo? Nawe waweza vuka ulipo kwenda upande wa pili ulio bora zaidi.

No comments:

Post a Comment