Thursday, August 20, 2015

Dondoo za kufahamu kabla hujanunua taa za mezani

Taa za mezani ni muhimu kwa kila chumba  si tu kwa ajili ya  mwanga bali pia ni moja ya pambo la kuongeza rangi na staili. Kuzinunua inabidi kuwa makini ili usipoteze hela yako na muda vile vile. Hapa nimekuandalia dondoo unazopaswa kuzingatia wakati wa kufanya manunuzi.

Fahamu kazi ya taa ya mezani unayotaka kununua. Je, ni  kwa ajili ya kusomea au ni  pambo tu au  ni kwa ajili ya wakati wa burudani? Ukishajua lengo lako la kununua taa hiyo itakusadia kufahamu vitu vya kuzingatia kama vile ukubwa, rangi ya kivuli chake na aina ya balbu inayotakiwa.

Meza utakayoweka taa yako ikoje? Kuweka juu ya meza fupi na isiyo imara sana (kwa mfano meza ya kioo chembamba) unapaswa kununua taa nyepesi na yenye mlingoti mwembamba. Vilevile taa ya kuweka kwenye meza ndefu inafaa iwe fupi na yenye mlingoti mnene.

Kwa upande wa balbu kama taa ni kwa ajili ya mapambo unatakiwa ununue balbu ya mwanga hafifu, na kama ni ya kusomea ni kinyume chake ili kuleta mwanga mwingi. Mara zote weka balbu ya kuendana na lengo la taa yako.

Nunua taa za mezani kwa kuzingatia mapambo mengine ya ndani mwako ili kuleta mandari yenye uwiano.

Taa za mezani si bei ndogo kwa uchumi wa sasa, kwahivyo hakikisha unafanya manunuzi sahihi na nunua kwenye duka la kuaminika ubora wa vifaa vyake. Ili taa yako iwe na muonekano wa upya kwa muda mrefu.


No comments:

Post a Comment