Tuesday, November 10, 2015

NJIA 10 ZA KUWEKA MPANGILIO KWENYE CHUMBA KIDOGO CHA KULALA


1. Tandika kitanda. 
2. Hifadhi documents zote muhimu kwenye droo badala ya kuziacha zisambae kila mahali.

3. Tumia vizuri droo za pembeni mwa kitanda kuhifadhia, hii itakusaidia sana.

4. Hifadhi hereni bangili na vitupio sehemu moja maalum rahisi kuchukua na kutumia pale vinapohitajika. Ni ahueni kujua kila kitu na sehemu yake.

5. Chumba kidogo cha kulala kinamaanisha eneo finyu kwa kabati la nguo. Weka kitundikio rahisi . Pia ni pambo la chumba chako ukipendacho.
    Hifadhi waya na chaja za simu na kamera eneo moja. 

7.  Tumia ubao wa kutobolea documents zinazotakiwa kutendewa kazi karibuni kama vile bill ndogondogo na pia kumbukumbu za siku.

8.  Tumia vizuri kona za chumba. Mara nyingi huwa zinasahaulika. Unaweza kuweka vimeza kwenye kona na vikakupa eneo zaidi la kuhifadhia vitu kama vitabu mapambo na picha.

9. Kama bado unafikiri una vitu vingi basi tumia mvungu wa kitanda. Droo za mvunguni ni nzuri kuhifadhia vitu kama shuka na mataulo.
10. Unakumbuka wakati ilikuwa sawa kuweka picha ukutani kwa kutumia tape? Nyakati hizo zimeisha. Tumia vitundikio maalum vya picha za ukutani na itasaidia kuondoa hali ya mrundikano.



No comments:

Post a Comment