Saturday, November 19, 2016

Wazo la kuwa na bustani kavu


Naomba ingia instagram @mtotomagazine u like picha hii hapa chini ili ishinde. Asante sana

Maji ni rasilimali muhimu kitaifa na kimataifa. Wazo la kuwa na bustani kavu ni zuri hasa kwa walio maeneo yenye ukame, wasio na maji ya kutosha kumwagilia, na pia  wenye pilika nyingi. Hawana muda mwingi wa kutumia katika kutunza bustani, ingawa wanapenda iwe na muonekano mzuri. Kama ndivyo basi suluhisho ni
bustani kavu.

Bustani kavu ni bustani ambayo sehemu kubwa ya ardhi yake ina mawe badala ya ukoka na kwa upande wa maua na miti imeoteshwa ile ya kuweza kuhimili ukame. Ni vyema, kwako wewe unayepanda wazo la bustani kavu kufahamu haya.

Bustani kavu inakuwa na maua machache ambayo nayo yana uwezo mkubwa wa kustahimili maji kidogo. Kwahivyo wakati unapotaka kuianziasha, inakupasa kuchagua aina ya maua na mimea ambayo haihita maji mara kwa mara. Kiasi kwamba unaweza ukayamwagili angalau mara moja tu kwa wiki au hata baada ya wiki mbili. Unachagua mimea sahihi inayoweza kukabiliana na tabia nchi. Mabadiliko ya tabia nchi yana uwezekano mkubwa  wa kuleta joto na kiangazi cha muda mrefu kwa maeneo mengi ya nchi., kwahivyo ni vyema kuwa na mpango madhubuti wa angalau kuweza kuifanya bustani yako ihimili hali hiyo.

Kuna mimea na maua mengi ambayo yananawiri kwenye udongo mkavu na kuwa na muonekano wa kuvutia mno. Mimea na maua haya mingi ni ile yenye majani manene kama jamii ya kaktasi na aloevera na pia ile yenye majani membamba kama sindano ambayo yana eneo dogo la kupotezea maji juani. Vilevile ipo yenye majani yaliyojisokota na hii inasaidia kupunguza ukubwa wa eneo linalochomwa na jua kwahivyo kuepuka mmea kupoteza maji mengi juani. Wauzaji watakuelekeza kabisa kuwa mmea, mti au ua hili linashamiri kwenye jua kali na halihitaji maji mengi.

Miti ambayo kamwe haipotezi kijani chake katika majira yote ya mwaka, kwa mfano miti inayojulikana kama ya Dodoma ni kiungo muhimu kwenye bustani kavu. Vichaka na miti ya namna hii inavutia na ni muhimu kuleta upepo tulivu bustanini.

Sehemu ya ardhi ya bustani kavu inakuwa na mawe badala ya ukoka kama zilivyo bustani nyingi tulizozoea. Faida ya haya mawe ni kuipa bustani kavu muonekano wa mvuto na kuepusha vumbi. Unaweza pia kuchagua aina ya mawe asili, kwa mfano meupe au ya kijivu.


Bustani kavu ina faida  pengine kuliko aina nyingine zote za bustani, kwa ubunifu wa kutumia mawe, mimea michache, ruhusu ubunifu wako ufanye kazi ili kurahisisha maisha yako huku ukifurahia kupata unachokipenda. Bustani kavu iliyooteshwa mimea na maua ya kuchaguliwa kwa umakini pamoja na mawe yake inawezekana kuwa na muonekano mzuri sana. Na kwa kutengeneza ya kwako hutakosa amani ya kuingia gharama kubwa ya maji katika majira ambayo hakuna mvua.

Mawe haya yanapatikana KAYIKAYA HOME FURNITURE & DECOR
Simu 0745 970 044

No comments:

Post a Comment