Monday, October 6, 2014

--nitavukaje--kutoka muajiriwa kwenye NGO hadi ufugaji

Bw. Peter ana masters ya kilimo toka SUA, nimechat naye mawili matatu kuhusu kuvuka kwake toka kuwa mwajiriwa hadi kujiajiri. Ananiambia alikuwa ameajiriwa kwenye NGO lakini alifika mahali akajiuliza kuwa kwa nini asitumie elimu yake kujiajiri. Na hii ilitokana zaidi na rusha roho ya wafadhali ku withdraw na hivyo kutokuwa na uhakika wa ajira. Ameamua kutumia elimu yake ya kilimo kwa kufuga kuku, kwale, bata mzinga na bikini kwenye sehemu ya shamba lake la heka 2 alilonunua mpiji magohe ambapo ameligawa viwanja vinne. Kimoja ameweka makazi yake, cha pili ameweka nyumba za wapangaji, cha tatu ameweka mifugo yake (ambapo anasema kutokana na uzio anafuga free range system) na cha nne ameweka ofisi yake. Nikamuuliza kwale ni nini, akaniambia ni ndege wadogo ambao mayai yake yanatafutwa na wazazi wengi kwa ajili ya kuwapa watoto wao kuongeza grey matter ya kwenye brain, mayai hayo pia ni dawa na huwa yanaongeza hata kiwango cha CD4 kwa waathirika wa Ukimwi. Anasema yai moja la kwale ni sh 600. Anajivunia kujiajiri kwenye kilimo kwani anasema amekuwa na uhakika na kipato kwa mfano bata mzinga mmoja anamuuza hadi sh 100,000 wakati bikini ni sh 250,000.

Umehamasika na stori hii? Kaa standy kwa itakayofuata kukuwezesha  kukuvukisha au pengine kukupa wazo la biashara...

No comments:

Post a Comment