Monday, March 7, 2016

Dondoo za namna ya kuchagua fimbo za pazia


Ni rahisi kutozingatia namna pazia na fimbo zake zinavyofanya chumba kionekane. Ila pale unatapoziondoa ndipo unagundua umuhimu wake. Zifuatazo ni dondoo chache za namna ya kuchagua fimbo kwa ajili ya pazia unazotaka kutundika.

Weka fimbo ambazo zinaendana na mapambo mengine ya chumba husika. Hapa ni muhimu kuangalia rangi ya fimbo. Usijeukanunua fimbo za rangi ya dhahabu kwa mfano, isioane na
chochote hapo chumbani na  ikawa kama kitu kisicho mahali pake.

Zingatia muonekano wa mwisho uliotumika  kupendezesha  fimbo hizo. Utagundua kuwa fimbo zenye muonekano usio wa kung’aa wa mati unatengeneza mandhari tulivu kuliko ule wa kung’aa wa polishi.

Malighafi iliyotumika kutengenezea fimbo sio muhimu sana kwani pazia ni zilezile hakuna zenye uzito mkubwa wa kutisha useme kwamba fimbo za malighafi fulani ni imara zaidi kushikilia pazia lako. Kwa hapa hifadhi pesa yako huna haja ya kununua fimbo za gharama kubwa, zote kazi yake moja. 

Cha muhimu ni kuzingatia urahisi wa kufunga na kufungua pazia ikiwa imetundikwa kwenye fimbo hiyo. Kwa mfano kuna baadhi ya fimbo haziko laini kuteleza kirahisi wakati wa kufungua na kufunga pazia ambapo inakubidi kulazimisha. 

Uzuri ni kwamba wauzaji wengi wa fimbo hizi huwa wanauza na mapazia, usiogope kujaribisha. Ukiona fimbo haiku laini haikufai kwani hutaweza kufungua pazia zako hadi mwisho kwa uzuri na pia kulazimisha kila wakati itapelekea fimbo kung’oka.

Angalia ua au tunaita pia vifuniko vya miisho ya fimbo. Endapo vina muonekano wa mbao (hata kama sio mbao halisi) vitaendana na fenicha nyingi ambazo huenda unazo chumbani. Chochote utakachochagua cha muhimu ni kuhakikisha kinaoana na vitu na mapambo ya chumba kizima.

Fahamu muundo wa fimbo unazohitaji. Je, ni zile zilizoko kwenye seti kwa ajili ya kutundikia pazia mbili, moja nzito na nyingine nyepesi kwenye dirisha moja au ni zile fimbo zilizoko moja moja kwa ajili ya pazia moja nzito tuu? Unapaswa kufahamu hilo.

Furaha yangu ni kukuwezesha kupendezesha nyumba yako. piga/whatsapp 0755 200023

No comments:

Post a Comment