Friday, December 18, 2015

PICHA: HIVI UZUNGUNI KWANINI HAWAOKOTAGI KWENYE BUSTANI

Hii picha nzuri mpya ni rasmi iliyotoka ya familia ya mwana mfalme wa Uingereza kwa ajili ya kutoa heri ya sikukuu. Ila mazingira ya hii picha kama unavyoyaoona bustani imedondokewa na majani mengi makavu na hayajaondolewa. 

Na ni mara nyingi naona picha za hivi za bustani huko ughaibuni. Huwa najiuliza kwanini hawasafishi hizi bustani kwa kuondoa haya majani makavu? Wenye exposure zenu hebu semeni neno why inakuwa hivi?..

2 comments:

  1. Mmmh! lakini wenzetu bustani zao zinastawi zaidi kwasababu ya hali ya hewa. Kwa bongo kuwa na bustani kama hii na maji ya DAWASA na jua linavyowaka yahitaji moyo...labda Arusha na Mbeya!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ila kama unapenda bustani unatafuta jinsi kama vile kuchimba kisima. Hata kiwe na maji ya chumvi kuna baadhi ya majani kwa mfano haya ya siku hizi ya canadian ni rafiki mkubwa wa maji ya chumvi na ukiyamwagilia utadhania umeweka mbolea jinsi yanavyoshamiri.

      Delete