Tuesday, December 31, 2013

je unabaki nyumbani usiku huu?

kwa mawazo yangu nadhani ni vyema kubaki nyumbani usiku huu ukawa na familia yako usiku wa mwaka mpya. na sababu zangu hizi hapa:
1. huna haja ya kwenda kuliwa na mbu au kupigwa na baridi kama uko maeneo yenye kati ya vitu hivyo viwili
2. hutalazimika kulipia kinywaji kwa gharama kubwa huko kwenye mabaa kwa ajili ya usiku huu
3. unaweza kuvaa mavazi utakayojisikia burudani ukiwa nyumbani badala ya kujilazimika kuvaa kiusiku usiku kimtoko
4. kama una watoto hutakuwa na wasiwasi wa mtu wa kuwaacha nao
5. hutakuwa na risk zitokanazo na heka heka za kuupokea mwaka mpya
6. unaweka kulala kwa raha zako

kwa sababu hizi kwangu ni vizuri zaidi kuupokea mwaka mpya ukiwa nyumbani.

Happy New Year!

No comments:

Post a Comment