Tuesday, December 29, 2015

BARBEQUE (CHOMA CHOMA) NI NJIA RAHISI KULIKO ZOTE YA KUANDAA SHEREHE NYUMBANI

Haijalishi kama hutakubaliana na mimi ila nakuhakikishia kuwa choma choma ndio njia ya gharama nafuu na ya haraka na isiyo na mlolongo mrefu kama una kijimnuso nyumbani. Na kama tujuavyo sherehe za nyumbani sio za umati.

Sababu hizi hapa:

1. Maandalizi ni mafupi sana. Yaani tuseme unachoma kuku, ni kiasi cha kuweka nyama zako viungo, kusubiri kwa muda na kuanza kuchoma.

2. Unaweza kuchoma wewe mwenyewe na hapa ndio penye bana matumizi kwani huhitaji mambo ya caterer.

3. Unaweza kuchomea popote nje ya nyumba. Hata kwenye garden upande wa majani kwakuwa jiko la kuchomea halidondoshi moto au majivu ya moto chini useme yataunguza majani na maua.

4. Nyama choma zinaendana na ndizi za kukaanga (za kuchoma zina usumbufu) na kachumbari, ambapo wewe na familia yako mnaandaa tu fasta.

5. Rasilimali zinazotumika, kwa mfano mkaa ni kidogo sana

Kama huwa unapenda kuburudisha nyumbani niambie njia rahisi unayotumia ili tujifunze kutoka kwako pia. Simu/Whatsapp 0755 200023

No comments:

Post a Comment