Thursday, December 31, 2015

PICHA: NYUMBA YA MAMA MCHUNGAJI RWAKATARE YAWEKEWA ALAMA YA X NA KUANDIKWA BOMOA!!

Unaona hiyo canopy ya getini mdau...ngazi mbili...full architectural
Msanifu kweli aliwekea heshima fani yake...hiki ki balcony cha juu kabisa nadhani ni cha umaridadi tu haendi mtu mule ndio maana hata hakina vizuizi. Landscaper na paving zake za rangirangi ndio usipime.

Hii nyumba inayosemekana kuwa ni ya mama Mchungaji Rwakatare ( au ni Lwakatare?) imetia fora mitandaoni leo kuwa inatakiwa kubomolewa. Kuna anayejua sababu ni nini na je, ni ukuta wa fence tu unaobomolewa au ni nyumba nzima?

Kweli ndio maana maandiko yanasema "jipeni moyo kwani ulimwenguni mnayo dhiki..."duuh unaweza kufa huku unatembea, Ee Mungu!



No comments:

Post a Comment