Monday, September 26, 2016

Dondoo nne za kuzingatia unapotaka kununua duveti


Kwa wengi wenye makazi ya kisasa duveti limekuwa sehemu muhimu ya matandiko yao. Sio tu linapendezesha kitanda na chumba kwa ujumla, lakini pia linamsaidia mlalaji kupata uzingizi murua. Unapotaka kununua duveti utashangazwa na aina nyingi na za kuvutia zilizopo sokoni ikiwa ni pamoja na mapya na ya mitumba ambapo inaweza kukuchanganya kuwa ni lipi hasa ununue.

Bi Eve Moshi wa kampuni ya Eve Beddings Mwenge simu namba 0713 681 261 ambao ni
wauzaji wa mashuka na maduveti anatujuza kuwa maduveti yanakuja kwa mitindo mbalimbali, ukubwa, rangi, uzito, malighafi ya kitambaaa ambavyo vyote hivi vinachangia kwenye kupata lililo sahihi. Mnunuzi usisahau kuzingatia yote haya wakati unapochagua duveti la kununua kabla hujafikia uamuzi wa mwisho.

Ukubwa
Siku zote unapotaka kununua tandiko hasa duveti, ukubwa ni kitu muhimu mno cha kuzingatia. Duveti la ukubwa sahihi kwa kitanda sahihi unakupa usingizi sahihi kwani linakupa ukubwa sahihi wa kuufunika mwili wako wote. Eve anasema mara zote inatakiwa kuchagua duveti ambalo ni kubwa kuliko ukubwa wa kitanda unachoenda kulitandika. Inalipa kitanda muonekano safi na nadhifu.

Kitambaa
Kitambaa kinachukua nafasi muhimu katika utengenezaji wa duveti. Aina ya malighafi iliyotumika inaamua hisia ya mvuto kati ya ngozi ya mlalaji na duveti.  Ni ukweli kuwa maduveti yaliyotengenezwa kwa kitambaa chenye kiwango kikubwa cha pamba yanapendwa zaidi japo kuna ya vitambaa vingine pia kama hariri na mchangayiko wa hariri na pamba. Ingawa maduveti yenye kitambaa cha pamba ndio yako juu haimaanishi kuwa huwezi kununua ya vitambaa vingine kwani nayo yana faida zake. Kwa mfano, duveti la hariri linakauka mapema zaidi kuliko la pamba. Kwahivyo hapa ni wewe uamue mwenyewe baada ya kufahamu haya.

Uzito
Maduveti yaliyojazwa malighafi za ndani kwa jinsi ambayo yanaonekana ni manene yanapendwa kuliko yale yaliyo nyepesi. Wanunuzi wengi hawaonekani kujali kama ni mazingira ya baridi au joto wao wanachotaka ni duveti liwe zito na hisia za kunesa kiasi.

Rangi na michoro
Wakati wowote unapotaka kununua duveti ni vyema uzingatie mandhari ya chumba unachotaka kuliweka ili michoro na rangi iendane na ya vitu vingine ili kukifanya chumba kivutie. Pia katika dondoo hii fahamu kuwa kuna maduveti yenye michoro ambayo yanafaa zaidi kwenye vyumba vya watoto wadogo kuliko vya watu wazima.  Vilevile rangi na michoro mbali na nia ya kuongeza mvuto wa chumba, ni kwa swala la usafi endapo kimiminika chochote kitadondokea kitandani kwa bahati mbaya. Sasa kutokana na maisha yako ndipo unaamua rangi na michoro fulani ndio itakufaa zaidi.


Mara zote unapotaka kununua duveti zingatia mambo hayo manne ili usijekuchagua ambalo ni la kiwango cha chini ukawa umetumia vibaya hela yako.

No comments:

Post a Comment