Leo katika mfululizo wa stori zangu za kukuwezesha kuvuka kutoka daraja ulilopo kwenda la juu nimeongea na entrepreneur Fred Kirya ambaye alikuwa mwalimu hapo kabla lakini sasa ana media company. Nikamuuliza amevukaje? Akaniambia alivyokuwa mwalimu alijishughulisha pia na kuandaa program za vijana walioathirika na mambo mbalimbali, watukutu na hata wanajeshi waliotoka vitani halafu vichwa vikavyatuka kiana. Kutoka huko baadhi wa vijana walioweza kuachana na hali hizo wakawa wanaenda kuongea kwenye vituo mbalimbali vya redio. Hapo ndipo Fred alipojenga interest na media na akafungua media company yake ambayo anarekodi nyimbo za kwaya, singles za wasanii, program za watoto na vipindi vya vijana kwenye vituo vya redio. Fred anasema kwa kufanya kazi kwenye kampuni yake mwenyewe ana furaha ya kufanya anachokipenda, kuwa makini zaidi kwa mfano matumizi na utunzaji wa vifaa vya kazi na kubwa zaidi financially amekuwa na wise spending...... Kaa standby kusoma stori nyingine itakayofuata...
Friday, September 26, 2014
usisahau kuwekea mbolea bustani yako kwenye vuli hii
Mvua za vuli zimepamba moto kabla ya kuingia kwenye masika. Ukiweka mbolea kipindi hiki ikakutana na masika yanayokuja itasaidia mno kuboresha bustani yako.
Thursday, September 25, 2014
my article for newspaper: jiko safi ukiendelea kupika
Baadhi ya siku unaweza kushangaa kama kupika kunalipa kwa nguvu
yote inayotumika. Kweli, unaweza kuweka mlo kabambe mezani, lakini jiko lako
likaishia kuwa chafu mno kwa, mrundikano wa vyombo vichafu. Unaweza ukawaza kuwa
inaenda kuchukua muda mwingi kusafisha kuliko kula!
Kanuni kuu ya jiko kuwa safi wakati ukiendelea kupika, ni kuanza
na jiko safi. Kwa njia hii uchafu unaokuogopesha ni ule unaotengeneza wakati wa
kupika tu. Kwa mazoea wengi wanajitahidi kuacha jiko safi kabla ya kwenda
kitandani kila ifikapo usiku. Vyombo visafi vinawekwa kabatini, vile vichafu
vinaoshwa, viporo vinawekwa kwenye vikontena na kuwekwa ndani ya jokofu, ndoo
ya uchafu inamwagwa na kwa namna hiyo hakuna uchafu unaobaki jikoni.
.
Siri ya kufanya jiko liwe safi wakati unapoendelea kupika ni
kuosha kadri vinavyochafuka. Nadhani hakuna njia nzuri zaidi ya kusisitiza hili.
Kama wali unaendelea kuiva kwa dakika 20, una muda wa kusafisha. Kama kuna muda
wa kusubiria chakula kiive, basi kuna muda wa kusafisha. Inashangaza jinsi
tunavyodharau hizi dakika 10 (au zaidi!) ambazo zingeweza kurahisisha kazi yetu
ya kusafisha hapo baadaye. Safisha kwanza, na utakuwa na muda wa kupumzika na
kufurahia chakula chako baadaye.
Pimia vyakula ndani ya sinki, na rudisha kila kitu mahali pake
baada ya kukitumia ili kaunta isishamiri vitu. Jitihidi kuwa unafanya
maandalizi yanayotakiwa kabla ya kuwasha jiko. Kama unatumia kikombe au kijiko
cha kupimia, hakikisha unakisuuza papo kwa hapo mara baada ya kukitumia. Futa
vyakula kwenye kaunta kila vinapowagika, hii itasaidia kuzifanya kaunta zako
zisiwe vululu vululu na kukusababishia kazi kubwa ya kusafisha baadaye. Hii pia
inasaidia kuwa na eneo la kutosha kufanyia kazi. Nyanya ndio kiungo
kinachochafua zaidi kaunta. Haiepukiki kupata matone ya nyanya ukutani na hata
juu ya stovu. Kufuta punde kwa kitambaa cha unyevu kunasafisha mara moja, kwa
ajili tone halijakomaa. Kwa chakula ama kiungo chochote kile kilichomwagika
jikoni mwako safisha kabla hayijakaukia kwenye eneo husika. Itasaidia kuokoa
muda na machukizo baadaye.
Hifadhi vifaa na vyakula unavotumia mara kwa mara maeneo ya
karibu na safisha makabati yako ya jikoni na jokofu kwa msimu. Kwa namna hii
hutakuwa na haja ya kuondoa vitu vyote kabatini kwa ajili ya kutafuta kitu
kimoja unachohitaji.
Wakati unapopika tumia vyombo vichache. Kwa mfano, wakati
unapotaka kumenya viazi badala ya
kumenyea maganda kwenye chombo, tumia mfuko au gazeti mbapo utabeba na kutupa
moja kwa moja kwenye ndoo ya taka na hivyo kupungukiwa na chombo cha kuosha.
Kwa siku zile ambazo una muda mchache sana, pika vyakula rahisi
ambavyo havihitaji kutumia sufuria na vikaangio vingi. Fanya mapishi ambayo
chakula zaidi ya kimoja kinapikiwa kwenye sufuria moja, mifano ni mchemsho na
mbogamboga.
Endapo utakuwa na mapishi kwa ajili ya wageni kadhaa nyumbani,
basi gawa kazi yako. Fikiria ni nini unaweza kuandaa usiku mmoja kabla ya ugeni
wako. Hii itasaidia kufanya maandalizi na kujikuta baada ya tukio ukiwa na
vyombo vichache vya kusafisha. Kama utapika maharage kwa mfano, unaweza
kuyasafisha na kuloweka usiku. Halafu unayaacha yamekaa kwenye jokofu, hadi
kesho yake wakati wa kuyapika.
Kupunguza mrundikano kwenye kaunta inafanya wepesi wa kusafisha
jiko lako. Unavyokuwa na vitu vingi kwenye kaunta ndivyo inavyokupasa kuvisogeza
vyote kabla ya kusafisha na hii inakupa kazi kubwa. Baadhi ya watu kanuni ni
kuwa, hakuna kifaa chochote kukaa juu ya kaunta vinginevyo kiwe ni kile tu
kinachotumika kila siku kwa mfano kipashio cha chakula. Vingine vyote kama
visagio na kadhalika vinahifadhiwa kabatini hadi wakati wa matumizi ndipo
vinapotolewa. Usipende vijiko na visu vyako vikae juu vikibeba mafuta mafuta na
vumbi. Viweke kwenye droo lililo karibu na stovu, ili unapovihitaji iwe rahisi
kufungua na kuchuka. Havina haja ya kuwa juu ya kaunta na kula eneo lako la
kazi.
Hizi ni baadhi ya njia za kukuwezesha kuweka jiko safi wakati
ukiendelea kupika. Je, wewe msomaji wangu ni kwa namna gani unaweka jiko lako
safi wakati ukiendelea kupika? Nitafurahi kusikia toka kwako!
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
--vuka--kutoka architect muajiriwa hadi kujiajiri
Vijana wetu wengi mara wanapomaliza chuo wanaanza kusaka ajira. Wengi wanashindwa kuamini kuwa wanaweza kujiajiri kwa kufanya kile ambacho tayari wameshakuwa na ujuzi nacho. Leo nimechat na Caleb ambaye ni architect, nikamuuliza ni kwa vip ameweza kujiajiri. Alichoniambia ni kuwa mara baada ya kumaliza chuo aliajiriwa kwa miaka miwili. Wakati huo alikuwa anafanya vikao na wateja wake binafsi nyakati za jioni baada ya kazi za mwajiri wake. Mambo yalivyochanganya akajiajiri. Nikamuuliza maana ya mambo kuchanganya ni nini? Akasema alipata mradi wa mwaka mmoja kwenye kazi yake hiyo ambapo alijiaminisha kuwa akijiairi wakati wa mradi huo itakuwa ni wakati muafaka kwani hata kwa miaka miwili mbele asingepata mradi, mwingine mkubwa bado angeweza ku survive kwa zile kazi ndogondogo. Anasema ana uhuru zaidi wa binafsi na kipesa alivyo sasa kuliko alivyokuwa ameajiriwa. Umepata cha kujifunza hapo? Nawe waweza vuka ulipo kwenda upande wa pili ulio bora zaidi.
Tuesday, September 23, 2014
-vuka---kutoka daraja la uzururaji hadi fundi mechanic
nimekutana na hii nikaipenda na nikaamini ni daraja ambalo vijana wengi wangeweza kuvukia. unaweza ukadhani walivyolifumua fumua gari wapo Japan kumbe ni hapa hapa TZ...
hii ni chasis mpya baada ya gari kufumuliwa na ile ya zamani kuondolewa. Inaoshwa ipakwe rangi ndio kijumba cha gari kipachikwe.
chasis la zamani lililoondolewa kwa ajili gari lilikuwa limepata ajali na hivyo chasis kupinda.
kijumba kikisubiri chasis ikamilike ili kipachikwe.
hii ni chasis mpya baada ya gari kufumuliwa na ile ya zamani kuondolewa. Inaoshwa ipakwe rangi ndio kijumba cha gari kipachikwe.
chasis la zamani lililoondolewa kwa ajili gari lilikuwa limepata ajali na hivyo chasis kupinda.
----vuka----
friends,
as nina spirit ya biashara nimependa kuweka "nitavukaje" ambacho ni kijisegement kitakachokupa hadithi fupi sana ya mafanikio itakayokutia moyo na hata kuweza kukupa wazo la biashara. karibu...
as nina spirit ya biashara nimependa kuweka "nitavukaje" ambacho ni kijisegement kitakachokupa hadithi fupi sana ya mafanikio itakayokutia moyo na hata kuweza kukupa wazo la biashara. karibu...
Monday, September 22, 2014
vitu hivi vitaiongezea bedroom yako mashiko...
1. ki carpet...chochote kile ili mradi miguu isipate ubaridi na ugumu
2. mito ya kumwaga...
3. sehemu ya kukaa ambayo sio kitandani
4. vitu/picha unazopenda zinazokupa kumbukumbu nzuri
5. ugiza giza...bedroom ikiwa nyeupe saana mashiko yanapungua, weka pazia ambazo zinaua mwanga kiaina
2. mito ya kumwaga...
3. sehemu ya kukaa ambayo sio kitandani
4. vitu/picha unazopenda zinazokupa kumbukumbu nzuri
5. ugiza giza...bedroom ikiwa nyeupe saana mashiko yanapungua, weka pazia ambazo zinaua mwanga kiaina
Thursday, September 18, 2014
my article for newspaper: vifaa vya msingi jiko dogo la kisasa
Huenda pengine ndio unaanza maisha ya kujitegemea au ya
ndoa, unahitaji kuwa na vifaa vya msingi jikoni vya kuanzia kwa miezi michache
ya mwanzo—hata miaka michache. Au labda ni mzazi unayetaka kumsaidia
huyo kijana wako, binti au rafiki namna ya kuanza maisha. Pia kama ni bibi
harusi mtarajiwa makala hii inakuhusu. Nimefanya kazi kubwa ya kutafiti katika
maduka ya vifaa vya jikoni na kukuandalia orodha ya vifaa vya msingi kabisa vinavyotakiwa
kuwepo jikoni kwa ajili ya kukuwezesha kuandaa chakula katika maisha yako hayo
mapya.
Nia hapa ni kuonyesha orodha ya vifaa vya kawaida kabisa
vya msingi vya jiko dogo la kisasa.
Ni rahisi kuangukia kwenye ushawishi wa
muonekano lakini kitu kimoja cha kujua kwa kweli ni kuwa hauna haja ya kuvunja
benki ili kuwa na vifaa vya jikoni vya kiwango. Orodha hii ya vifaa vya msingi jikoni inaweza
kubadilika kutokana na hitaji la mhusika. Pia vyombo vya mezani kama vile
sahani vijiko na glasi vinategemea zaidi ladha ya mtu binafsi na kwa sababu
hiyo sijaviorodhesha hapa. Kwa hivyo vifaa vya
msingi vya jiko dogo la kisasa ni kama vifuatavyo:
Visu
Kisu kikali cha mpishi ni moja kati ya
vifaa muhimu zaidi jikoni, na kama utanunua kilicho sahihi kitatumika kwa miaka
mingi. Nunua visu vya jikoni ambavyo havishiki kutu.
Ubao wa kukatia
Ubao sahihi wa kukatia utafanya visu vyako
vidumu, na rahisi kusafishika. Kuna aina nyingi za mbao hizi kama vile plastiki,
miti na hata glasi.
Kifungulia chupa na makopo
(opener)
Nunua ambayo unaweza kufungulia chupa na
makopo ya aina tofauti tofauti. Nzuri ni ile iliyo rahisi kwa matumizi.
Kisaga vyakula (Blender)
Kama kawaida nunua ambayo ni rahisi
kutumia na yenye kazi nyingi tofauti ambapo utaweza kusaga vyakula vyako na
kutengeneza juisi.
Vikaangio na masufuria
Iwe uko singo au ni wanandoa wapya kwa
kuanzia unahitaji vikaangio japo viwili na sufuria nne hadi sita. Sokoni vikaangio
na sufuria zipo zilizotengenezwa kwa material
nyingi mno. Nunua ambazo hazing’ang’aniani na chakula (nonstick).
Stovu
Watengenezaji
wengi wameunganisha stovu na tanuri ukinunua mbayo unaweza kutumia nishati
zaidi ya moja itakuwa ni busara zaidi.
Jokofu
Kwa
maeneo mengi ya nchi yetu walau inahitajika kuwa na jokofu kwa ajili ya
kuhifadhia chakula kisiharibike. Kwa kuanzia si mbaya ukawa nalo dogo kwenye
jiko lako hili la kuanzia maisha.
Kipasha chakula
(Microwave)
Hiki
kinafanya kazi kubwa ya kupashia na hata kupikia baadhi vya vyakula. Habari
njema ni kuwa zipo za bei rahisi kabisa. Ni rahisi kutumia na wengi wanapendelea
kuziweka juu ya kaunta ya jiko. Huna haja tena ya kupashia chakula kwenye
sufuria.
Kikausha mikate (Toaster)
Hiki nacho kwa wengi wanaopendelea kula
mikate iliyokaushwa huwa wanakiweka juu ya kauta.
Mabakuli/Vikontena
Wanasema
mapishi ni sanaa, sio? Kuwa na mabakuli na vikontena ndani ya jiko lako la
kuanzia maisha vitakusaidia katika maandalizi ya mapishi na hata vikontena
vitakusaidia kupashia na pia kuhifadhia vyakula kwenye jokofu.
Kindoo cha
uchafu
Unapoandaa
chakula na kuosha vyombo lazima utahitaji hiki kindoo kwa ajili ya kuwekea
uchafu. Ni muhimu kiwe kile cha mfuniko wa kujifunga chenyewe.
Jiko
lenye vifaa vya msingi vinavyopaswa kuwepo jikoni ni rafiki kwa mpishi.
Unapokuwa na vifaa sahihi na unajua jinsi ya kuvitumia, unaweza kuelekeza akili
yako kwenye chakula unachoandaa. Kama nilivyosema awali vifaa hivi vinaweza
kuongezeka kutegemea na mhusika na mazingira unaweza kuwa na vifaa hivi vya
msingi jikoni kwa kuanzia na baadaye ukaongeza kidogo kidogo kwa kadri ya
mahitaji yako. Mpishi mzuri anatumia vifaa tofauti tofauti na mwishoni
anapata vile hasa anavyohitaji.
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
Tuesday, September 16, 2014
pambo hili lina faida lukuki...
Pambo hili na jamii yake linafaa kuwekwa ukutani na mlangoni kwa ajili kwa umbo lake huwa linakuwa flati upande mmoja na kitumbo upande wa pili. Ndani kuna nafasi kiasi kwamba likiwa kama pambo; wakati huohuo unaweza kuhifadhi vitu vidogo dogo kwama vile dawa zilizo kwenye pakiti, uzi na kadhalika. Laa kama unataka kusisitiza pambo lako basi weka maua ya artificial badala ya vikorokoro kama huyu hapa kwenye picha alivyoweka. Lilivyotengenezwa material yake sio nzito. Unaweza kulitumia miaka nenda rudi. Linapatikana kwenye maduka yanayouzwa mapambo ya ndani. Perfecto!
Thursday, September 11, 2014
my article for newspaper: Jinsi ya kupata kizulia sahihi cha jikoni
Wengi tutakubaliana kuwa zulia la
ukuta kwa ukuta sio sahihi kuwekwa jikoni, ila kizulia cha kutupia kina faida
kadha wa kadha jikoni. Kizulia hiki kinasaidia kuepusha miguu na sakafu ya
baridi na kinaongeza rangi, hata kiwe kidogo namna gani. Yote kwa yote sababu
kuu yaweza kuwa ni kwa ajili ya burudani ya miguu na kuiepusha na baridi. Kama
unaweza kusikia baridi ya kukera kwenye nyumba yako mwenyewe basi ni ukakasi. Kuweka
kizulia jikoni kunakamilisha sakafu na mvuto wa jiko. Vinginevyo uwe unapenda
sana rangi kiasi kwamba umepaka kabati zako za jikoni rangi ya kung’aa kama
vile pinki, kijani ama nyekundu.
Kizulia cha kutupia kinaweza kuleta
rangi bila kukufanya utumie hela nyingi, kama hii ndio sababu ya kuamua kuweka
kizulia jikoni hapa basi ni dondoo chache za kukusaidia kupata kilicho sahihi.
Kuchagua kizulia sahihi kwa ajili ya
jiko, ni vyema kufahamu nia yako kuu ya kuamua kukinunua. Inaweza kuwa ni kwa
ajili ya kuepusha miguu na ubaridi wa sakafu au kuongeza staili, rangi na mvuto
kwenye sakafu ya jiko. Pia fikiria ukubwa na umbo la kizulia ambacho kitafaa
zaidi kwa nafasi iliyopo. Usisahau kuzingatia vifaa vilivyotumika kutengenezea kizulia
utakacho na kufahamu ni utunzaji kiasi gani utakaohitajika. Chagua kizulia
ambacho hakitelezi (hakikimbii sakafu) kwa ajili ya sababu za kiusalama.
Hasa kama sakafu ya jiko lako ni
laini, yakung’aa na inayoteleza, ni muhimu sana kuchagua kizulia chenye mnato/mpira
kwa chini kinaposhikana na sakafu. Mpira huo utasaidia kizulia kikae mahali
pamoja kisihame hame kinapokanyagwa, ambapo kinaweza kusababisha mtu kuanguka.
Chagua
mahali sahihi pa kuweka kizulia chako cha jikoni. Ni wapi unapotumia muda
mwingi unapokuwa jikoni? Pengine ni
mbele ya sinki, kwa hiyo ni kuwa utachagua kuweka kizulia eneo hili. Au labda
una eneo kubwa la kutembea kwenye sakafu ya jikoni. Basi angalia mahali hapo
kati unapoweza kutupia kizulia chako ili kilete burudani ya miguu maeneo
kadhaa. Vile vizulia vyembamba virefu vinafaa zaidi wa jiko lenye sakafu ndogo.
Kama lengo lako kuu la kuhitaji
kizulia jikoni ni kuondoa ubaridi na kuleta nesa nesa ya miguu, basi unene wa
kizulia unahusu. Utahitaji mbonyeo kati ya sakafu ngumu na miguu yako kwa
burudani. Ulaini wa kizulia pia unaepusha miguu yako na baridi la sakafu ya
marumaru au mbao au hata saruji. Hakuna anayetaka kuwa kwenye maumivu wakati
akiosha vyombo!
Chagua
manyonya sahihi, iwe ni sufi au pamba. Kizulia ambacho kinasafishika kirahisi
kwa sabuni na maji. Urahisi wa kusafisha ni lazima ukumbukwe kwenye kuchagua
kizulia cha jikoni, hasa kwa vile vinavyowekwa chini ya sinki au mbele ya stovu
au jokofu. Vizulia vya sufi vinaweza kuwa
chaguo sahihi kimuonekano ila kwa kawaida vinashika madoa kirahisi na vinahitaji
usafishaji wa kitaalam kwahivyo ni vyema kuweka vizulia vya aina hii kwenye
vyumba vingine nyumbani ila sio jikoni au chumba cha kulia chakula, anasema
muuzaji Aisha Mbegu. Vizulia vya kufumwa kwa mimea ya asili kama vile katani au
majani ya baharini vinaweza kuwa chaguo sahihi kwa ajili ya kuweka chini ya
meza ya kulia chakula, kwa ajili kwa kawaida ni rahsisi kuvifuta na kusafisha
hata kwa kufagia.
Haijalishi utaamua kuchagua kizulia
cha jkoni kilichotengenezwa kwa vifaa vya aina gani, kuchukua kipimo cha eneo
unalotaka kuweka kizulia ndani ya jiko lako itakusaidia kupata kilicho sahihi. Wakati
wa kuamua aina za vizulia, jitahidi kutafakari rangi, na ni kwa namna gani
ukubwa na muundo utakavyogusa muonekano
mzima wa jiko lako.
Wacha kizulia chako kitengeneze
stori. Chagua ambacho kitaongeza uzuri kwenye jiko lako. Sakafu za jiko huwa
zinapooza, kizulia kinaweza kuongeza uchangamfu na ladha binafsi kwa kuunganisha
rangi za jiko pamoja. Kama nilivyosema kabla, chagua kizulia kitakachoongeza
rangi, ambapo ni rahisi kubadilisha kizulia ili kuondoa muonekano wa jiko utakapochoka
zile rangi zake za kudumu ulizozizoea.
Hongera kwa kufanya eneo kla sakafu
ya jiko lako kuwa na mvuto, nesanesa na budurani! Utakapoweka kizulia cha
jikoni hutatamani kukiacha.
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
Wednesday, September 10, 2014
kwanini ni muhimu kufua carpet kwa sabauni na maji ya pressure
ninapata amazing deal ya kufua mazulia ya manyoya kwa ajili wateja wengi wanayaleta kutokana na kuwa yananuka vibaya. Carpet linapokuwa na harufu mbaya kwa kuwa labda limemwagikiwa vimiminika pengine ni wakati wa sherehe au maisha ya kawaida ya kila siku na pilika za watoto, kusafisha kwa vacuum cleaner au form cleaner haitawezekana kuondoa harufu mbaya ya zulia la manyoya likiloa linavyonuka.
Kinachotakiwa kufanyika ni kuniletea carpet lako kwa kuwa tuna pressure washer ya kuweza kulipiga maji, kuweka detergent na kulisugua hadi mabaki yote ya vyakula (eg ubwabwa wa sikukuu) na vimiminika vyote vitoke. Baada ya hapo tunaanika kwenye jua kali kwa siku mbili na zulia lako linakuwa tayari kama jipya. Kuamua kufua zulia kwa maji inaweza kuchangiwa pia na uchafu mwingine wowote kama vile vumbi na tope.
Karibu sana ian car wash tung'arishe tena carpets zako. Tuwasiliane 0755200023
Kinachotakiwa kufanyika ni kuniletea carpet lako kwa kuwa tuna pressure washer ya kuweza kulipiga maji, kuweka detergent na kulisugua hadi mabaki yote ya vyakula (eg ubwabwa wa sikukuu) na vimiminika vyote vitoke. Baada ya hapo tunaanika kwenye jua kali kwa siku mbili na zulia lako linakuwa tayari kama jipya. Kuamua kufua zulia kwa maji inaweza kuchangiwa pia na uchafu mwingine wowote kama vile vumbi na tope.
Karibu sana ian car wash tung'arishe tena carpets zako. Tuwasiliane 0755200023
| carpets zilizofuliwa, kukauka na kukunjwa |
| mteja yuko tayari kupelekewa carpets zake kwenye gari |
| hizi nazo ni za mteja mwingine zinamsubiri |
| hizi hazijakaula hivyo tumetandaza ndani tuanike tena kesho |
Monday, September 8, 2014
---vitu vizuri---getting better with age
Friday, September 5, 2014
Thursday, September 4, 2014
my article for newspaper: kuepusha wadudu ndani ya nyumba
Wakati baadhi ya watu wanaogopa wadudu, wengine wanaweza kuwa wanavutiwa
nao. Lakini kitu kimoja ambacho wengi tutakubaliana ni kuwa wadudu makazi yao
sio ndani ya nyumba. Si tu kuwa wanaleta mazingira hatarishi kiafaya, bali pia,
ni rahisi tu ya kuwa wanaudhi, kuanzia mbu wanaokupigia mziki masikioni mwako,
kukuuma na kukusababishia maradhi hadi kwa nyigu anayeweza kukusababishia
kidonda.
Hata yule mende wa kawaida anaweza akasababisha mzio hasa kwa watoto, anasema dokta Emil.
Kuepusha wadudu ndani ya nyumba inaweza kuwa ni vita vilivyoshindikana. Bahati nzuri ni kuwa, kwa kufahamu ni nini kinachovutia wadudu ndani ya nyumba yako, unaweza kuanza kufanya mabadiliko ambayo yatawakimbiza kimya kimya.
Kama vile mlango uliolokiwa unavyoweza kuwaweka wavamizi nje, mlango uliozibwa sahihi unaweza kuwazuia wadudu wasiingie ndani. Kuepusha wadudu wanaotambaa kuingia ndani kwa kupitia sehemu ya wazi mlangoni, weka kizuizi cha mpira au brashi chini ya mlango. Vizuizi hivi vinapatikana kwenye maduka ya vifaa vya ujenzi, anasema mseremala Simon.
Kumbuka kuwa mbinu zote hizi za kuziba chini ya mlango hazitafanikiwa kama mlango wenyewe utaachwa wazi. Kama una watoto ambao wanasahau kufunga mlango, fikiria kusimika vifunga mlango.
Wenye nyumba wengi wanategemea hewa safi ya nje iingie ndani kupitia milangoni na madirishani. Hii inaweza kuwa majaribu hasa wakati wa kiangazi. Bahati mbaya ni kuwa kiangazi ni wakati mbaya kwa vile mbu na wadudu wengine wengi wanavamia ndani ya nyumba. Kufurahia raha ya hewa safi bila kupata bughudha ya wadudu weka wavu wa kuzuia wadudu kama mbu kwenye madirisha na milango.
Eneo la nje ya nyumba linaweza kuwa linasababisha wingi wa wadudu ndani ya nyumba yako. Endapo mioto ya asili ni mingi na iko karibu sana na ukuta wa nyumba basi tegemea kuwa na mazalia makubwa ya wadudu na hivyo uwezekano wa wengi kujaribu kukimbilia ndani. Hii pia itakufanya hata wewe mwenye nyumba kushindwa kufurahia kukaa kuburudika nje ya nyumba yako, kwa hivyo njia nzuri ya kuepusha wadudu ndani ya nyumba ni kuhakikisha wanaondoka pia kwenye maeneo ya nje ya nyumba.
Majani yaliyorundikwa, matofali yaliyopangwa kwenye yadi yako na hayatumiki tena na mashimo ya maji taka yanafanya makazi ya wadudu mbalimbali. Maeneo haya ni sehemu za kujificha kwa wadudu kama mende nyoka na wengine wengi na hata panya. Mashimo ya maji taka yawe na mifuniko iliyoziba vizuri na mrundikano mwingine wowote uondolewe na utashangazwa ni kwa jinsi gani wadudu watakimbia na mazingira yako yatakavyovutia.
Hata yule mende wa kawaida anaweza akasababisha mzio hasa kwa watoto, anasema dokta Emil.
Kuepusha wadudu ndani ya nyumba inaweza kuwa ni vita vilivyoshindikana. Bahati nzuri ni kuwa, kwa kufahamu ni nini kinachovutia wadudu ndani ya nyumba yako, unaweza kuanza kufanya mabadiliko ambayo yatawakimbiza kimya kimya.
Kama
ilivyo kwa binadamu, wadudu nao wanahitaji chakula, maji na makazi ili kuishi.
Kwa kukata usambazaji wa chakula chao na kuvuruga maeneo yao ya kujifisha,
unaweza kupunguza tatizo la kuwa na wadudu ndani ya nyumba yako. Kata chanzo
chao cha chakula kwa kuhakikisha kuwa vyakula vyote vinawekwa kwenye kontena
zilizofungwa vizuri. Mabaki ya vyakula ndani ya nyumba yatupwe eneo moja tu
ambalo ni ndoo ya uchafu yenye mfuniko wa
kujifunga wenyewe iliyopo jikoni. Ndoo hii imwagwe na kusafishwa kila siku baada
ya kuosha vyombo vya chakula cha usiku. Futa michuzi na mabaki yoyote yanayoweza
kuwepo maeneo ya wazi ndani ya nyumba. Osha vyombo punde mara baada ya kutumika. Pipa linalomwagwa uchafu nje nalo liwe na mfuniko.
Usisahau vyakula vya wanyama waliopo
nyumbani kwako. Kwa mfano unafuga mbwa na una vyakula vyake vya unga umehifadhi
stoo, unga huu unaweza kuvuta mende na sisimizi. Unaweza kuweka dawa za kuzuia
wadudu kwenye stoo yako ya chakula cha wanyama unaofuga.
Vifaa vyote vya kuhifadhia mabaki ya
vyakula ndani na nje ya nyumba viwe vinasafishwa kwa dawa za kuua wadudu mara
kwa mara.
Kama vile mlango uliolokiwa unavyoweza kuwaweka wavamizi nje, mlango uliozibwa sahihi unaweza kuwazuia wadudu wasiingie ndani. Kuepusha wadudu wanaotambaa kuingia ndani kwa kupitia sehemu ya wazi mlangoni, weka kizuizi cha mpira au brashi chini ya mlango. Vizuizi hivi vinapatikana kwenye maduka ya vifaa vya ujenzi, anasema mseremala Simon.
Kumbuka kuwa mbinu zote hizi za kuziba chini ya mlango hazitafanikiwa kama mlango wenyewe utaachwa wazi. Kama una watoto ambao wanasahau kufunga mlango, fikiria kusimika vifunga mlango.
Wenye nyumba wengi wanategemea hewa safi ya nje iingie ndani kupitia milangoni na madirishani. Hii inaweza kuwa majaribu hasa wakati wa kiangazi. Bahati mbaya ni kuwa kiangazi ni wakati mbaya kwa vile mbu na wadudu wengine wengi wanavamia ndani ya nyumba. Kufurahia raha ya hewa safi bila kupata bughudha ya wadudu weka wavu wa kuzuia wadudu kama mbu kwenye madirisha na milango.
Eneo la nje ya nyumba linaweza kuwa linasababisha wingi wa wadudu ndani ya nyumba yako. Endapo mioto ya asili ni mingi na iko karibu sana na ukuta wa nyumba basi tegemea kuwa na mazalia makubwa ya wadudu na hivyo uwezekano wa wengi kujaribu kukimbilia ndani. Hii pia itakufanya hata wewe mwenye nyumba kushindwa kufurahia kukaa kuburudika nje ya nyumba yako, kwa hivyo njia nzuri ya kuepusha wadudu ndani ya nyumba ni kuhakikisha wanaondoka pia kwenye maeneo ya nje ya nyumba.
Majani yaliyorundikwa, matofali yaliyopangwa kwenye yadi yako na hayatumiki tena na mashimo ya maji taka yanafanya makazi ya wadudu mbalimbali. Maeneo haya ni sehemu za kujificha kwa wadudu kama mende nyoka na wengine wengi na hata panya. Mashimo ya maji taka yawe na mifuniko iliyoziba vizuri na mrundikano mwingine wowote uondolewe na utashangazwa ni kwa jinsi gani wadudu watakimbia na mazingira yako yatakavyovutia.
Baadhi ya wenye nyumba wanapendelea
kutumia dawa za kupulizia kwa ajili ya kuua wadudu kama mbu na mende. Haijalishi
ni njia ipi unatumia ili kuepusha wadudu kufanya makao ndani ya nyumba yako;
njia kuu ya kuwafanya wakimbie ni kukata “mirija” wa kile kinachowavutia. Hii
inamaanisha ni pamoja na kuondoa mrundikano, vyakula na vyanzo vya maji. Bila
kuwa na rasilimali hizi, wadudu watakimbia kwako kuelekea nyumba ya pili na
kukuacha ukiwa na amani.
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
Monday, August 25, 2014
...marvelous monday...
marafiki zangu wa kweli wamerudi shule...
ukiniuliza best skill yangu ni ipi nitakujibu cleaning..yani iko moyoni. i love to make things and places spotless...
ukiniuliza best skill yangu ni ipi nitakujibu cleaning..yani iko moyoni. i love to make things and places spotless...
Thursday, August 21, 2014
my article for newspaper: makosa wakati wa kununua sofa
Makosa makubwa ya kuepuka wakati wa kununua sofa
Moja ya umuhimu wa makala kama hii ni kusaidia wadau kuchagua kilicho chema kwa ajili ya nyumba zao. Sofa ni fenicha ambayo muda mwingi wa maisha ya nyumbani unakuwa pale hivyo inatakiwa ikidhi viwango vya nyumba na maisha unayoishi. Kuhakikisha unapata sofa sahihi, epuka makosa haya makubwa unayoweza kufanya wakati wa kuinunua. Habari njema ni kuwa makosa haya yanaweza kuepukwa kama kutafanyika maandalizi kabla ya manunuzi. Makosa haya makubwa basi, ni yapi ambayo mara kwa mara wanunuzi wanayarudia?
Kusahau kupima ukubwa wa sebule yako
Unatakiwa
kujua ukubwa wa chumba kabla ya kukua sofa ili kuwa na uhakika kuwa fenicha
hiyo mpya itafiti. Usikimbilie kununua fenicha kabla ya kuwa na uhakika wa
ukubwa wa chumba, zingatia itakavyokaa kwa kujali milango na madirisha.
Kama
eneo husika kuna mwanga mwingi unaoingia zingatia rangi ya kitambaa kwani vipo
vinavyopaushwa na jua. Sofa inatakiwa iendane na ukubwa wa chumba, isiwe kubwa
sana wala kiduchu. Usitegemee kumbukumbu wakati ukiwa kwenye chumba cha
maonyesho ya sofa, huwa inadanganya kuona kuwa sofa ni ndogo kwenye chumba hicho
kwani eneo ni kubwa, pia sofa iwe na uwiano na fenicha nyingine sebuleni.
Kutokuwa makini
na rangi
Je
unafahamu kuwa rangi ya sofa inayoonekana kutokuwa na nguvu kwenye chumba cha
maonyesho inaweza kuwa kinyume kwenye sebule yako? Nenda na mto wa sofa
unaoupenda na kuutupia kwenye sofa unayotaka kununua ili kuona itakuwaje ndani
mwako.
Mvinyo mwekundu unaenda kumwagika kwenye sofa zako, kama una wanyama wa ndani kama paka nao wanaenda kufanya mambo kwenye sofa yako, mwenza na watoto wanaenda kula bisi kwenye sofa zako; hata uwakataze mara ngapi. Kwa kuwa maisha halisi yanaendelea kila siku, unahitaji sofa ya kuweza kubeba madhila yote haya.
Kuchagua aina mbaya ya kitambaa cha sofa ni kosa la gharama. Chagua rangi na aina ya kitambaa kutokana na jinsi sofa inavyoenda kutumika. Kama sebule inatumika sana na ukanunua sofa ya kitambaa laini au rangi za mwanga, inaenda kuharibiwa hata kabla hujaifurahia. Rangi ya sofa iendane na fenicha, samani, rangi ya ukuta na taa.
Rangi nyeupe, maziwa au nyingine ya mwanga isiwe chaguao lako kama kwenye makazi yako kuna uwezekano wa tope na mikono michafu kufikia sofa. Siku zote chagua rangi ambayo unaipenda na unaweza kuishi nayo, usichague kwa kuangalia mitindo ya nyakati. Utaishi na hiyo rangi uliyochagua kwa miaka.
“Siwezi kukuambia ni mara ngapi nimefanya kazi na wateja ambao wanataka kubadili kitambaa cha sofa zao ambacho bado kiko vizuri bali ni kwa sababu tu wameichoka rangi yake”, anasema mtengeneza sofa Hamis Rajabu. Bahati mabaya ni kuwa haichukui muda kuchoka vitambaa vya maua maua, vyenye mistari mikali na vile vya rangi za giza, anasema Hamis. Ushauri wangu ni kuwa, chagua rangi ya kitambaa ambayo itashirikiana na rangi nyingi. Kama unapenda rangi nilizosema zinachosha mapema basi weka japo kwenye kiti kimoja cha pembeni lakini siyo kwa sofa nzima, anashauri Hamis
Kutokuomba ushauri
kwa wauzaji
Ongea
na watu wanaouza watakupa mawazo ambayo yatakupelekea kufanya maamuzi ya busara.
Hata hivyo unamuizi wa mwisho ni wako ila unapenda kuwauliza wataalam usikie
wanasemaje.
Kutofikiria sofa
ina burudiko kiasi gani
Utakubaliana
na mimi kuwa mara nyingi unaweza kushindwa kupata usingizi kitandani, ila ukija
kwenye sofa ukaegesha aidha ukiangalia muvi au kusoma kitabu haraka sana
unapata usingizi. Ni muhimu kuwa sofa unayotaka kununua ikawa ya matumizi na
burudani.
Kununua sofa
kabla ya kuijaribu
Kama
ambavyo sofa haitakiwi kuwa ndogo sana au kubwa sana kwenye chumba, vilevile
isiwe ndogo sana au kubwa sana kwako. Kama ni mrefu, hakikisha ukikaa miguu
yako itakaa vizuri. Kamwe usinunue sofa kabla ya kuijaribu, ikalie, ilalie,
ijaribu kwa kila namna ambayo utaitumia nyumbani. Kama unapenda kupata usingizi
wa mchana kwenye sofa hakikisha mikono yako iko vizuri kwenye sofa unayotaka
kununua.
Haya ni makosa makubwa ya kuepukwa wakati wa kunua sofa. Endapo utafanya makosa haya utaishia kutoridhika na sofa uliyonunua.
Tukutane wiki ijayo!
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
Tuesday, August 19, 2014
Sunday, August 17, 2014
Thursday, August 14, 2014
my article for newspaper: maeneo tunayosahau kusafisha
Wakati ukiwa unasafisha makazi yako
mwishoni mwa wiki hii, kumbuka kufanya usafi wa uhakika. Mara nyingi huwa
tunasafisha maeneo na vitu vinavyoonekana. Makala hii itakujuza baadhi ya
sehemu na vitu ambavyo kwa wengi ni rahisi kusahaulika kusafishwa na mwishoni
utasema, ee kweli hapa huwa sisafishi.
Tunakumbuka kusafisha ndani ya
jokofu, lakini je juu na chini yake? Ndani ni kwasababu huenda kila
tunapofungua mlango wa jokofu harufu mbaya na macho yanatuashiria kuwa sasa ni
wakati wa kusafisha. Juu ya jokofu kunabeba vumbi ambalo sio rahisi kuliona
vinginevyo uwe ni mrefu sana. Nyuma na chini ya jokofu vile vile kunaweza kuwa
kumebeba vumbi sawa na lile la juu. Na chini sio vumbi tu hata mabaki ya vyakula
vinavyodondoka kwenye sakafu ya jikoni. Kinachotakiwa ni kusimama juu ya kiti
na kusafisha juu wakati kwa chini
unachotakiwa ni kuomba mtu wa kukusaidia kulisogeza ili usiharibu sakafu yako
kwa kuburuza. Jokofu likishakuwa limesogezwa, ni kiasi cha kufagia na kudeki. Baada ya hapo lirudishe mahali pake.
Tunategemea
feni majumbani mwetu kwa ajili ya kuleta mpepea wa ubaridi. Kwa kadri feni
inavyotumika, ndivyo inavyojaa vumbi. Feni hasa za darini ni maarufu kwa kujaza
tabaka la vumbi. Njia rahisi ya kuzisafisha ni kufuta kwa kutumia ufagio uwe wa
kawaida au wa buibui uliofungiwa kitaulo kilicholoa kwenye brashi zake.
Kulingana na majira na matumizi, feni zisafishwe walau mara moja hadi mbili kwa
mwezi .
Ni
kichekesho cha muda mrefu kuwa ndani ya nyumba sofa ndio eneo linalomeza vitu
vidogodogo. Kwa sababu hii mito ya sofa (ile ya kukalia na kuegemea) inapaswa kuondolewa
na ndani ya sofa kusafishwe. Japo kwa nyumba nyingi ndani ya sofa ni rahisi
kusahaulika kusafishwa hadi pale vitu kama hereni, kalamu ama opener inapopotea
ndio eneo hili linakumbukwa kua huenda mtoto kaficha humo. Kulingana na aina na
ukubwa wa familia yako pengine huhitajiki kusafisha ndani ya sofa mara kwa
mara. Usafi huu ujumuishe na kufua foronya za mito, ni kazi rahisi japo huwa inasahaulika.
Ndoo
za taka za ndani ya nyumba zinaashiria kuwa zinahitajika kusafishwa ila pipa la
nje linakosa kiashiria hiki kutokana na eneo lililopo. Ukiona jirani anaanza
kuguna kila unapofungua pipa lako la nje la taka basi ni wakati wa kufikiria
kulisafisha kiaina. Kwa kawaida mapipa ya taka ya nje yanahitaji kutupiwa jicho
la usafi zaidi wakati wa kiangazi kuliko wa masika.
Kama una taa za vivuli ndani ya nyumba yako, kumbuka kusafisha kile kifaa kinachosababisha kivuli. Kuendana na jinsi kilivyotengenezwa iwe ni kwa kitambaa, kioo au plastiki zinaweza kusahaulika kufunguliwa na kusafishwa.
Majani ya mimea iliyooteshwa ndani ya nyumba husahaulika kufutwa vumbi. Haishangazi kukuta mmea wa ndani iwe ni nyumbani au mgahawani ukiwa na majani yaliyojaa vumbi.
Vipasha vyakula (microwave) vinachafuka sana ndani kwa kuwa wengi wanapasha vyakula ambavuo havijafunikwa. Uchafu huu wa matone ya michuzi unaorukia kwenye kuta za microwave hubaki na kukaukiana na ajili unapata moto kila vyakula vingine vinapopashwa. Haishangazi kukuta microwave ambayo kwa jinsi ilivyo ndani unapata ukakasi kupashia chakula.
Ingawa wengi hawana taabu ya kukumbuka kusafisha vioo iwe ni vya madirisha au vya kujitazama, kioo cha luninga ni eneo ambalo kwa wengi linasahaulika kusafishwa. Endapo luning hii inatumiwa na watoto wadogo ni rahisi kuona alama za vidole kwenye kioo pale inapokuwa imezimwa. Chukua muda kufuta vumbi luninga yako weekend hii ili kufanya kioo king’ae tena.
Vumbi linajikita kwenye vitabu. Chukua dasta kufuta vumbi vitabu vyako.
Ingawa tunaweza tusione uchafu na utando ulio kwenye vitasa vya milango ya nyumba zetu lakini upo. Na tunapovisafisha tunaweza tusihisi tofauti, lakini unajisikia vizuri kushika kitasa kisafi. Na zaidi ya yote kukinga nyumba yako na vijidudu vinavyotoka kwenye mikono michafu inayofungua milango kwa kushika vitasa hivi.
Ni nini na wapi unapofikiri watu wengi wanasahau kusafisha? Je kuna popote nimesahau?
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
Wednesday, August 13, 2014
Friday, August 8, 2014
house tour: Here's the $20M SoCal Mansion Kim and Kanye Just Bought
hebu tusafishe macho mdau tuone mambo hapa...
wenye nyumba, kim & kanye
ukifungua geti unakutana na muonekano huu wa mbele
yasemekana ina vyumba 8 vya kulala
vegetable garden nayo haijakosekana
floor ni ya mbao...huenda baby north atalala hapa
kanye naye atakuwa anajilia raha za kisamaki hapa kwenye hii pool
Thursday, August 7, 2014
my article for newspaper: kusafisha vifaa vya kusafishia
Jinsi ya
kusafisha vifaa vya kufanyia usafi
Hatusafishi
vifaa vyetu vya kusafishia sio? Hata ukikataa, kubali tuu kuwa wengi
hawasafishi. Wengi tunajua umuhimu wa kusafisha na kutunza vitu….ila vifaa
vyetu vya kusafishia mara nyingi vinasahaulika. Haijalishi wewe ni msafi kiasi
gani, haiwezekani kuweka nyumba safi kama vifaa vyako vya kusafishia
havisafishwi! Makazi ya vijidudu vingi ni kwenye maeneo machafu. Angamiza
vijidudu kwa kusafisha sponji na vifaa vyako vingine vya kusafishia!
Kwa
sababu tu kinatumika kusafishia sio kuwa kinajisafisha chenyewe. Kiukweli vifaa
vya kusafishia vinaweza kuwa makao ya uchafu, vijidudu, tope na harufu kama
havitunzwi vizuri. Jinsi vifaa vinavyotunzwa ndivyo hela yako ya kununua vipya
itakavyobaki mfukoni. Ufagio mchafu unachafua zaidi sakafu na pia uchafu huo
unaweza kukwaruza sakafu yako. Mashine ya kusafishia kwa upepo ambayo haijasafishwa
haifanyi kazi yake vizuri. Weka vifaa vyako katika hali ya usafi ili kuwa na
matokeo mazuri.
Kuna ule usafi wa kawaida wa kusafisha vifaa vya kusafishia japo kwa sabuni
na maji na kuviacha vikiwa safi tayari kwa kuanza usafi mwingine. Brashi za
kusafishia bafuni zishafishwe kwa dawa za kuua vijidudu japo mara moja kwa
mwezi. Brashi za kusugulia zaweza kusafishwa kwa maji na sabuni ya kawaida. Brashi
zenye taka zilizojishikilia waweza kuchukua kijiti na kuondoa taratibu taka
zote ziwe ni tope au nyuzi nyuzi.
Ndoo
zako za kupigia deki usiziache zikiwa na uchafu wa aina yoyote hata kama ni
maji yaliyotumika tayari. Ziache zikiwa kavu aidha kwa kuzigeuza juu chini.
Sponji
la kuoshea vyombo uwe unaliosha kwa maji ya moto walau kila juma. Ikiwezekana
hata kulichemsha jikoni itakubwa bora zaidi, wengine wanaenda hatua ya mbali
zaidi ya kuliweka kwenye kipasha vyakula (microwave).
Ila kama utafanya hivi hakikisha sponji
limeloa chepechepe kabla ya kuliweka kwenye microwave.
“Asimilia 70 ya bacteria huishi kwenye sponji chafu”, anasema dokta Mbuya.
Tokea
ukiwa mdogo, kulikuwa na kitambaa cha kufutia vumbi nyumbani. Ukichukua kitabu
chenye vumbi unachukua kitambaa unakifuta. Vitambaa hivi vya kufutia vyumbi
ambavyo wengi wetu wanaviita dasta
vinapaswa kufuliwa kiumakini kama tunavyofungua nguo nyingine. Tofautisha kati
ya vile vyenye uchafu mkubwa wa kudiriki kutengeneza utando na vile vyenye
uchafu mwepesi.
Vichwa
vya mop na madekio mengine vinapaswa
kusuuzwa baada ya kufanyika usafi na kuachwa vikauke. Kabla ya kusuuza
hakikisha kuwa unaondoa udongo wote, mchanga na hata majani yanayoweza kuwa
yamejishikilia ndani. Sio sawa baadhi walivyozoea kuacha dekio linakanyagiwa
mlangoni. Pale ni sehemu ya kuweka tandiko la mlangoni na sio dekio. Sabuni ya
kawaida ya kufulia inatosha, huhitaji kuweka dawa za kusafishia kwenye vifaa
hivi. Ila ni muhimu vikuke kwani vinaweza kutoa harufu ya uvundo.
Kusafisha
mifagio..mmh ni wachache wanaofikiria kufanya hivyo! Unaweza kufungua ile
sehemu ya brashi ukaitenganisha na fimbo na ukaiweka kwenye ndoo ukasafisha na
brashi zako nyingine za kusafishia. Jambo la kuzingatia ni kuondoa matope
kwanza kwa kuwa sehemu ya ufagio ya brashi ni maarufu kwa tope na uchafu
uliojizunguishia kwenye vibrashi vyake.
Mashine
za kusafishia kwa upepo zinatofautiana kiumuundo ila kuna dondoo kadhaa za
kukuwezesha kuisafisha. Tafuta kama una kitabu ulichonunulia kitakuongoza jinsi
ya kuisafisha. Hakikisha unamwaga mfuko wa kukusanya vumbi mara kwa mara. Kutegemea
na jinsi unavyotumia mashine yako fua mfuko wa vumbi kila baada ya miezi
mitatu. Uanike ili ukauke kabisa kwani ukiiurudisha ukiwa na unyevu
utasababisha vumbi kufanya tope na hivyo kuiharibu mota kwa kuilazimisha ifanye
kazi kubwa ya kusukuma kushindana na ukuta wa tope. Kama unasikia harufu ya
vumbi inatoka ndani ya mashine yako ni kwa kuwa mfuko wa vumbi umejaa.
Ingawa hutumii mashine yako ya kufulia kwa kitu kingine zaidi ya nguo bado kuna wakati inakubidi ufungulie maji kuisafisha yenyewe bila kuweka nguo ndani.
Tumejuzana
namna ya kusafisha vifaa vya usafi ambavyo tunatumia mara kwa mara nyumbani.
Inaweza kuwa shughuli sahihi ya kufanya kwa muda wowote wa ziada ulio nao weekend hii!
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
alhamisi ya rasha rasha...
rasha rasha za leo za hapa na pale za kupunguza vumbi kwa tuliopo mazingira ya vumbi. hali ya hewa si joto wala baridi ni safi kabisa...
Thursday, July 31, 2014
my article for newspaper: kusafisha bafuni
Hakuna anayetaka kusafisha bafuni, lakini ukisafisha
kila unapotumia, kazi inakuwa na maumivu kidogo kuliko kuacha hadi wakati wa
usafi mkubwa. Makala hii itakujuza ni jinsi ya kuweka kuta, bafu, sinki, bomba,
eneo la kuogea na bakuli la choo nadhifu kila wakati.
Unapoanza kusafisha bafuni, kwanza ondoa vitu vyote
vya kuhamishika kama vile vizulia, tenga la nguo chafu, kimeza au kikabati na
kindoo cha taka.
Baada ya hapo ondoa buibui kwenye
kona za dari ikifuatiwa na kufuta vumbi mlango kwa nje na ndani. Kwa ujumla
wakati wa kusafisha chumba anzia juu kushuka chini. Ruhusu taka za vumbi na
buibui zimwagike sakafuni kwa ajili utasafisha mwishoni. Kitambaa cha kufutia
kinafaa sana kwa kazi hii japo pia waweza kutumia fagio.
Mimina blichi ama sabuni za
kusafishia kwenye bakuli la choo na iache iondoe uchafu taratibu.
Weka dawa ya unga wa kusafishia zile sehemu ambazo
zina uchafu. Kama kuna uchafu umejijenga kwenye lile eneo la kuogea, sinki ama
pembeni na bomba weka unga wa kusafishia halafu sugua taratibu kwa brashi.
Ukiacha unga huu ukae kati ya dakika 10 hadi 15 wakati ukifanya jambo jingine itaruhusu
kulainisha uchafu. Hakikisha unasoma maelezo ya dawa ya kusafishia ili kuwa na
uhakika unatumia kiasi sahihi ambacho hakitaharibu maeneo yako. Pia ni vyema
kujaribu dawa eneo dogo kabla ya kusafishia eneo kubwa.
Paka sabuni au dawa nyingine za kusafishia kwenye kuta
za bafu kama ni za marumaru. Kwa kutumia sponji ama brashi sugua sehemu uliyoweka
sabuni. Isuuze vizuri kuondoa michirizi yoyote michafu na kama ukuta ni wa
karibia na sinki ama bakuli la choo ukaushe kwa taulo. Ukuta wa sehemu ya
kuogea unaweza kuuacha bila kuukausha. Ni vyema kuvaa glovu wakati wa kusugua
kwani baadhi ya madawa na sabuni zinaweza kuchubua ngozi.
Safisha bomba la kuogea ambalo sio siri kuwa
wasafishajiwengi huwa hawakumbuki kusafisha. Bomba inatumika tu kusafishia
kwingine ila yenyewe inasahaulika kusafishwa. Ni kama msemo wa mshumaa kujiunguza
kumulikia wengine! Kwa sababu hiyo utakuta kwenye bomba na vichwa vyake
kunakuwa na uchafu wa sabuni zilizogandian. Hali huu huweza ikasababisha makazi
ya vijidudu.
Pazia la bafuni huwa linaandamwa na ukungu eneo
linalogusana na sakafu. Ni vizuri zaidi ukalifungua na kulifua kwenye maji ya
moto kwa kiasi kidogo cha sabuni na blichi. Kumbuka adui nambari moja wa ukungu
ni blichi. Kiasi kidogo kitaondoa uchafu bila hata kusugua.
Angalia eneo la sinki na sugua mabaki ya sabuni na
dawa za mswaki kwa sabuni kidogo pamoja na sponji au brashi. Mswaki wa zamani
unaweza kutumika kuondoa uchafu kutoka eneo la kati ya bomba na mishikio yake. Kuwa makini kuwa brashi
la kusugulia bakuli la choo lisitumike kusugulia sinki. Hii inaweza kusambaza maradhi kwa
kuruhusu vijidudu vya kwenye choo kuingia kwenye sinki la mswaki. Kuzuia hali
hii isitokee, brashi la bakuli la choo liwe la peke yake. Ni muhimu kutumia
blichi kusafishia bafuni ili kusaidia kuua vijidudu.
Safisha kioo kwa kutumia ama maji na taulo au dawa
ya kusafishia vioo na taulo.
Safisha nje ya choo ukianza na ile sehemu ya juu ya
kuvuta maji, taratibu endelea kusafisha eneo lote la nje ya choo ambalo ni
pamoja na mfuniko na eneo la chini ya pale pa kukalia na futa kwa taulo. Kumbuka
kitaulo hiki kimetengwa kwa kusafishia choo pekee.
Sugua ndani ya bakuli la choo kwa brashi yake halafu
vuta maji. Huna haja ya kusugua kwa nguvu nyingi. Acha sabuni na dawa ya
kusafishia ikufanyia kazi hiyo.
Sasa ni wakati wa kusafisha sakafu ukinanzia na zile
sehemu zilizojifisha hadi zile za wazi. Safisha mavumbi yote na uchafu wote
ulio chini na pale eneo la choo lilipounganika na sakafu. Eneo hili kwa kawaida
huwa ni chafu sana na lile bomba la nyuma linajaa mavumbi. Malizia kwa kusuuza kwa
maji masafi kuondoa sabuni itakayoweza kubaki na kusababisha utelezi.
Subiri kidogo sakafu ikauke ndipo urudishe vile vitu
ulivyoondoa awali.
Ili kuweka bafu lako katika hali ya usafi na
kupunguza kutumia nguvu kubwa ya kusafisha unatakiwa uwe unasafisha maeneo
mbalimbali ya bafu mara baada ya kuyatumia. Kwa mfano safisha bakuli la choo
kila baada ya kulitumia, vile vile eneo la kuogea pamoja na sinki. Hata kama
sehemu hizi hazionekani kuchafuka safisha tu kwani madini yaliyoko kwenye maji
nayo yaweza kufanya alama. Kama utafanya hivi, usafi mkubwa utakuwa na maumivu
kidogo kwani uchafu hautakuwa umejijenga.
Makala hii
imeandaliwa na Vivi Machange ambaye ana mapenzi makubwa juu ya muonekano wa
makazi na pia ni mjasiriamali wa usafi wa magari, mazulia na nguo. Kwa maoni au
maswali tuma kwenda 0755 200023 au christines.daughter@yahoo.com
Subscribe to:
Posts (Atom)













