Monday, March 23, 2015

MSIMU MPYA WA TUZO ZA MUZIKI ZA KTMA UMEZINDULIWA RASMI LEO

Kampuni ya bia ya Kilimanjaro ambayo ndiyo mdhamini mkuu wa mashindano ya tuzo za Kilimanjaro Music Awards wamezindua msimu mpya wa tuzo za Kilimanjaro Music Awards zinazofahamika kama KTMA2015.
Msimu mpya wa tuzo umezinduliwa rasmi leo na kuwa na maboresho kadhaa ikiwepo njia zitakazotumika kupendekeza wasanii na nyimbo kushiriki katika mchakato huo ambapo kwa mwaka huu kutakuwa na njia tatu tofauti na mwaka jana ambapo kulikuwa na njia mbili za kupendekeza na kupiga kura kupata washindi wa tuzo hizo.

Kwa mwaka kuu kuna maboresho katika mapendekezo hivyo mashabiki wanaweza kupendekeza nyimbo au msanii kupitia tovuti,SMS pamoja na Whatsapp.

"Mashabiki watapewa nafasi ya kupendekeza majina ya nyimbo na wasanii wanaostahili kuingia katika kinyang'anyiro na Njia za kupendekeza ni kupitia: Tovuti, Whatsapp na SMS,Mashabiki watapewa nafasi ya kupendekeza majina ya nyimbo na wasanii wanaostahili kuingia katika kinyang'anyiro"


Lakini pia wadhamini hao wakuu wa Tuzo za Kilimanjaro Music Awadrs wamesema kuwa zoezi la kupendekeza msanii na nyimbo yataanza rasmi Machi 30 hadi April 19 huo ndio muda wa mashabiki kupendekeza majina ya nyimbo na wasanii wanaostahili kuingia katika tuzo. Chanzo EATV

No comments:

Post a Comment