Tuesday, March 31, 2015

Unajiuliza uanzie wapi?.......HATUA 3 ZA KUPAMBA CHUMBA

Baadhi yetu tunahamia nyumba mpya au chumba ambacho hakina chochote ndani au hata kimepambwa tayari lakini unataka kubadilisha muonekano. Sasa mtu anajiuliza hapa naanzia wapi kuki design. Napenda changamoto hii kwa ajili
mimi ni homelover kwahivyo ninachojua kuhusu nyumba napenda kuwashirikisha na wengine. Sasa ni kwa namna gani unaweza kuleta muonekano wa kuvutia na kwa ladha yako chumbani. Hapa ni hatua tatu according to mimi:

Kwanza, fikiria vitu na rangi zinazokuvutia wewe binafsi.
Wengi wana rangi/vitu wanavyopendelea, kwa mfano, yupo anayependelea wanyamawanyama, yupo wa mauamaua, yupo wa pundamilia, yupo wa rangi plain labda brown, maroon, cream nk. Hapo ndipo pa kuanzia pale unapotaka kupamba chumba.

Baada ya hapo amua ni nini kinaingia/kinabaki na ni nini kinaondoka kati ya vitu unavyotaka viwepo hapo chumbani iwe ni sofa kitanda, zulia, sanaa ya ukutani nk. Sasa anza kuviingiza kuvipanga kuanzia chini kwenda juu, maana yake ni kwamba tuseme unataka kuweka carpet, usianze na meza kabla hujalitandika, ndio maana ya kuanzia chini/sakafuni kwenda juu. 

Ukishamaliza sakafu kifuatacho ni kuanza kuingiza fenicha kubwa kwanza, kama ni sofa au kitanda au meza..zile ndogondogo zitafuata baadae.

Halafu weka vitupio kama mito, maua na taa za mezani.


Sasa hapa ni kama chumba kimeshakamilika na unaona vizuri kila kitu kivyokaa. Malizia kwa kutundika pazia, picha, fremu na sanaa zozote za ukutani za ladha yako. Kwa mawazo yangu chumba hakijakamilika kupambwa kama ukuta ni mtupu.

Kwa dondoo nyingine ya muonekano wa nyumba tukutane kesho, hapahapa.

No comments:

Post a Comment