Monday, March 30, 2015

STUDY: WAZAZI MNAPASWA KUDHIBITI UNENE WA WATOTO WENU........TAKWIMU ZINAONYESHA WATOTO KUNENEPA KUPITA KIASI IMEKUWA KAWAIDA MAJUMBANI

Madaktari wanasema kuwa wazazi wengi hawajui madhara ya afya kwa watoto walionenepa kupita kiasi.

Katika utafiti uliowajumuisha zaidi ya familia 2,976 nchini Uingereza ni wazazi 4 pekee waliokuwa na shauku kuwa mtoto wao alikuwa amenenepa kupita kiasi.

Madaktari wenyewe walikuwa wamewatambua watoto 369 kati yao waliokuwa na kiwango cha juu cha mafuta mwilini.

Takwimu hizo zinaonesha kuwa watoto walionenepa kupita kiasi sasa wamekuwa kawaida tu majumbani.
Watafiti hao wanaonya kuwa hili ni janga kwa afya ya jamii.

Asilimia 31% ya wazazi hawajui kutambua dalili za mtoto aliyenenepa kupita kiasi.

Aidha utafiti huo ulielezea kuwa takriban mtoto mmoja kati ya watano ambao wanaumri wa miaka 6 tayari wanauzito unaozidi kadri kwa asilimia 14%.

Kundi hilo la watafiti kutoka taasisi ya usafi ya Uingereza ''London School of Hygiene and Tropical Medicine'' lilizitembela familia 3,000 na kuwahoji iwapo watoto wao walikuwa ni wanene kupita kiasi wastani ama wembamba?
majibu yao yaliwaduwaza.

Takriban thuluthi moja 31% ya wazazi walidunisha uzani wa watoto wao.
Proffesa Russell Viner, wa chuo cha Afya ya Watoto aliiambia BBC kuwa wazazi wa kisasa wanamajukumu wengi na hivyo watoto wao hutunzwa na vijakazi asilimia kubwa ya muda ambao wazazi wako makazini mwao.

''Hili ni janga ambalo linatokota ,madhara yake yataonekana siku za usoni katika njia ya maradhi mengi tu yanayohusiani na unene'' alisema Professa Viner.

Kwa mujibu wa Daktari Dame Sally Davies, ''Afya ya watoto kwa sasa imehujumiwa na dhana kuwa japo mtu ni mnene jamii haitambagua kwani watu wengi duniani ni wanene''

"Nafikiri kwamba itatubidi tuwaelimishe wazazi kuhusiana na maswala ya afya ya watoto wao na pia kuwaeleza kuwa wanapaswa kufuatilia kwa karibu unene au sio wa watoto wao''


Anapendekeza kuwa sheria madhubuti zinapaswa kutungwa ili kuzima matangazo ya kufana ya vyakula vyenye mafuta mengi.

No comments:

Post a Comment