Wednesday, January 21, 2015

MAHUSIANO: Dawa ya wanaotoka nje ya ndoa hii hapa

WASWAHILI husema kwamba siku za mwizi ni arobaini.Msemo huo sasa huenda ukafanikishwa miongoni mwa akina baba ambao huenda kinyume na ndoa zao.

Hii ni baada ya kubuniwa kwa kifaa kinachojulikana kwa jina Semenspy kilicho na uwezo wa kubaini majimaji yaliyosalia katika nguo za ndani, nguo za kulalia na katika maeneo mengine baada ya mtu kuhusika katika tendo la ngono.

Kulingana na gazeti la The Nairobian nchini Kenya, maagizo yake ni kwamba iwapo unamshuku mumeo ama mkeo tafuta majimaji hayo katika chupi ama nguo zilizotajwa hapo awali kisha uyachunguze katika kifaa hicho.

Kulingana na daktari Wachira wa DIY Solutions, kifaa hicho kimetengenezwa Marekani na imebainika kwamba wamefanikiwa kupata majibu sahihi kutoka kwa wanawake waliotaka kujua iwapo waume zao na marafiki zao wa kiume wanawadanganya katika uhusiano baada ya kuyachunguza maji maji hayo.


Mi nadhani mtu kweli kama katoka kusaliti atakuwa mkali kama mbogo sidhani hata hayo majimaji unaanza kuyapataje..

No comments:

Post a Comment