Wednesday, January 7, 2015

--nitavukaje--Wajasiriamali waombwa kuchangamkia fursa

haya tena kwa wewe unayetaka kuvuka daraja hilo chukua hatua fastaaa.

Wednesday, January 7 2015, 0 : 0

WAJASIRIAMALI mbalimbali nchini wameombwa kuchangamkia fursa kwa kuchukua fomu za kushiriki programu ya shindano la ujasiriamali linalojulikana kama 'Safari Lager Wezeshwa' ili waweze kujinyakulia vitendea kazi vya aina mbalimbali ikiwemo trekta lenye thamani ya sh. milioni 220.

Wito huo ulitolewa Dar es Salaam jana na Meneja Mpya wa Bia ya Safari Lager, Edith Bebwa, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu programu hiyo ya awamu ya nne ambayo imelenga zaidi kwa wajasiriamali nchini kujitokeza kuchukua fomu hizo.

"Awali tuliwaeleza wajasiriamali kuwa na subira wakati fomu hizo zikiandaliwa lakini tunachoweza kusema ni kwamba hivi sasa fomu ziko tayari wanaweza kuzipata katika maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye mabohari ya TBL,"alisema Bebwa.

Alisema pia fomu hizo ziko kwa mawakala wa kusambaza bia, kwenye mitandao na kusema kuwa ni wakati mwafaka kwa wajasiriamali kuchukua fomu hizo na kuzijaza tayari kwa kushiriki rasmi shindano hilo.

Bebwa alisema kuwa mara baada ya wajasiriamali hao kumaliza kujaza fomu hizo ni vyema wakazirejesha kwenye vituo vilivyotajwa au maeneo walipozichukulia na kusema kuwa wajasiriamali wadogo wadogo nchini kuhakikisha wanachangamkia fursa hiyo kwani hiyo ni hazina tosha.

"Ninasema hivi kutokana na kwamba hii itarahisisha kazi kwa kuwepo kwa vitendea kazi bila ya kutumia nguvu nyingi kwao kutokana na kwamba kwa wajasiriamali ambao wamefanikiwa kushiriki na kushinda wamepata mafanikio makubwa,"alisema.

Kiongozi wa wataalam wa Ushauri wa Biashara kutoka Kampuni ya TAPBDS Joseph Migunda, alisema kuwa programu hiyo inatarajia kufanyika takribani mikoa yote ambapo itawapa fursa wajasiriamali wa aina zote fursa bila kujali fani, kabila wala jinsia bali wanatakiwa kujaza fomu kwa usahihi na umri usiopungua miaka 18-40.

Alisema kwa wale wenye nia ya kufika mbali kibiashara na wenye malengo ya kuisaidia jamii inayowazunguka wasisite kuchangamkia fursa hiyo na kwamba kwa wale watakaofanikiwa kuibuka kidedea watapata mafunzo mafupi ya awali pamoja na kukabidhiwa ruzuku zao.




No comments:

Post a Comment