Thursday, May 21, 2015

Umaarufu ni shida, mateso - UPENDO NKONE

MWIMBAJI mahiri wa nyimbo za injili, Upendo Nkone, amesema umaarufu kwa wasanii ni mateso kwa kuwa humjengea woga msanii kufanya jambo lolote popote hata kama moyo wake unapenda.

Upendo alieleza kwamba, msanii maarufu anapofanya jambo tofauti jamii humchukulia tofauti hali inayofanya ashindwe ama afikie mafanikio kwa mateso makubwa ya kutafuta kimya kimya.

“Umaarufu kwa msanii ni mzuri lakini ni mateso, uzuri ni kwa kuwa unarahisisha kazi zako lakini ni mateso kwa namna nyingine unatakiwa utende mema tu usikosee kama malaika,” alisema Nkone.

MTANZANIA

No comments:

Post a Comment