Sunday, April 19, 2015

WAGANGA WA TIBA MBADALA WAAMBIWA WASIFANYE MAPENZI NA WATEJA WANAOWAHUDUMIA......HATA KAMA WAMESHINDWA KILIPA GHARAMA ZA MATIBABU

SEMINA
Waganga wa tiba mbadala wilayani Iramba, Mkoani Singida wameshauriwa kutofanya mapenzi na wateja wao wanaoshindwa kulipa gharama za matibabu waliyowapatia na badala yake wafuate sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia utoaji wa huduma zao.
Mratibu wa Tiba Asilia kutoka katika Hospitali ya wilaya ya Iramba, Roda Yona alitoa ushauri huo kwa nyakati tofauti alipokuwa akitoa mada kwenye semina elekezi kwa waganga wa tiba mbadala na wakunga iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kituo cha walimu cha Ndago.

Alifafanua mratibu huyo kuwa mteja anapokwenda kwa mganga wa tiba mbadala kwa lengo la kupatiwa tiba hatakuwa ametendewa haki na mganga husika anaposhindwa kulipa gharama za matibabu aliyopata endapo atatakiwa kufanya vitendo vya ngono na mganga aliyempatia huduma za tiba yake.

“Unapokuwa na mteja wako akaja nyumbani kwako akapata huduma kwako akakosa malipo, naomba usimtumie,kama chambo cha wewe kupata mafanikio katika shughuli zako au ukamtumia yeye kama mke wako kwa sababu ameshindwa kukulipa huruhusiwi huo ni ukiukwaji wa sheria”alisisitiza mratibu huyo.

Kwa mujibu wa Roda endapo mganga yeyote yule atachukua hatua ya kufanya vitendo vya ngono na mgonjwa wake kwa kumbadili kuwa mke wake atakuwa amechukua hatua hiyo bila ridhaa ya mteja wake kwa kuwa atakuwa amekubali kuolewa kwa kukosa fedha za kulipa gharama za matibabu.

MOBLOG

No comments:

Post a Comment